Kikwete: Uvumilivu sasa basi...

Kikwete: Uvumilivu sasa basi...

Kamati kuu ya CDM iliadhimia kuwa 2013 ni mwaka wa Nguvu ya UMMA
 
Yah naungana nawe bethlehem basi iwanufaishe wanakijiji panapochimbwa gesi ama wilaya ya mtwara vijijin ilipo msimbati mana msikurupuke kujifanya watetez bila kuangalia hasara zake,mpuuz mwingine anasema eti isubiri hata miaka 25 iljayo hadi viwanda vitakavyohitaji gesi vitakapojengwa,what a fool.ukanda wenu hauwez halalishwa na kujidai watetez wa mtwara.
 
Haya maneno alishawahi kuzungumza Kova. Nakumbuka wakati anawatia mbaroni wale waliofanya uharibifu wa makanisa na yule Ustaadhi Ponda, alisema, eti jeshi la polisi limevumilia sana na sasa inatosha!
 
Rais wetu ni mwingi wa kuongea tu, si mtekelezaji. Tangu ianze migogoro ya kidini amefanya nini? Makanisa mangapi yameshachomwa moto? To be honest, migogoro ya kidini ina baraka za viongozi wa juu kabisa serikalini!
 
this is silly; amejuaje zinatosha? Walikuwa na kiwango walichotaka kufikia au kulikuwa na kiasi ambacho kilikuwa kinaweza kuvumilika na sasa kimepitilizwa?
nyerere aliposema "tumekandamizwa vya kutosha,tumeonewa vya kutosha na tumenyanyaswa vya kutosha " ulimwelewa? Au naye hukumuelewa kama ambavyo hapa umeshindwa kuelewa?
 
Real Silly, eti vurugu za kidini zilitaka kulitia doa taifa mwaka jana...kwa hiyo kuchomwa kote kule makanisa na watu kupigwa risasi bado sio doa?? Au alitaka na misikiti ichomwe moto ndio aone ni doa?? Halafu Sefue anakuja anasema kupunguza madaraka ya Rais ni hatari, kwa ujinga huu? Hembu kafie mbali huko, mmeishiwa hata kufikiri?? Shame on you!!
 
Ni lazima Jk aseme hivi kwa sababu tayari ameshsapokea 10% ya gas ameificha kwenye bank za uswiss.
 
nyerere aliposema "tumekandamizwa vya kutosha,tumeonewa vya kutosha na tumenyanyaswa vya kutosha " ulimwelewa? Au naye hukumuelewa kama ambavyo hapa umeshindwa kuelewa?

iyo comparative analysis unayoifanya hapa haihusiki wala haina mantiki.

:focus::focus:
 

iyo comparative analysis unayoifanya hapa haihusiki wala haina mantiki.

:focus::focus:
nilitegemea ajibu ambaye hakuelewa au na wewe hukuelewa?sasa kama nawe hukuelewa ile basi eleza kama hiyo ya nyerere uliielewa na kama uliielewa;kwa nini unashindwa kuielewa hii ya kikwete.
 
Haya ndio maamuzi magumu atakayofanya jk mwaka huu? Udini na ukabila si vimeanzishwa na serikali yake? Na ataufanyaje upinzani? He is wimp already, and we know it. Aanze na magamba
 
SERIKALI imesema haitavumilia kwa namna yeyote ile vurugu za kidini, kikanda na ukabila ambazo baadhi yake zilitaka kulitia doa taifa mwaka jana.



Pia imesisitiza kwamba haitawavumilia wanasiasa wanaotumia rasilimali za taifa kujitafutia umaarufu kwa gharama za kuligawa taifa.

Akizungumza na mabalozi kwa nyakati tofauti Ikulu, Dar es Salaam; kwanza katika sherehe ya kuukaribisha Mwaka Mpya iliyofanyika juzi na alipokuwa akiagana na Balozi wa Uingereza nchini, Dianne Corner jana, Rais Jakaya Kikwete alisema vurugu zilizotaka kujitokeza mwaka jana zinatosha.

“Serikali haitavumilia vurugu wala ukabila kwa namna yoyote ile…. Mwaka 2012 vurugu zenye sura ya kidini zilianza kujitokeza ila sasa nasema kwamba hatutazivumilia kwa namna yeyote ile, inatosha,” alisema Rais Kikwete.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kiongozi wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi waJamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Juma Mpango alisema jumuiya ya mabalozi imefurahishwa na namna ambavyo Serikali imekuwa ikishughulikia vurugu za kidini ambazo zilitaka kujitokeza bila kusababisha madhara kwa wananchi.

“Tumeridhishwa na namna ambavyo Serikali imekuwa inashughulikia mambo yakevizuri. Tunaomba mwendelee kushughulikia amani ya nchi hii maana ndiyo mhimili wa nchi za Maziwa Makuu,” alisema Balozi Mpango.

Kuhusu gesi
Rais Kikwete alizungumzia suala la rasilimali za taifa na kusisitiza kuwa pia hatavumilia kuona wanasiasa wakitumia suala la gesi kujitafutia umaarufu.

Wakati Rais Kikwete akitoa kauli hiyo jana, habari kutoka Mtwara zilidai kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene amewekewa magogo barabarani kumzuia asiende kwenye kijiji kinachozalisha gesi hiyo, huku Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo akizomewa.

Hata hivyo, polisi walikiri wananchi kuweka magogo barabarani kwa lengo lakumzuia waziri huyo, lakini ikaeleza kuwa gari lililozuiwa siyo la Simbachawene.

Akizungumza na Balozi Corner, Rais Kikwete alikemea tabia ya baadhi ya viongozi wa kisiasa kutumia suala la rasilimali za taifa, ikiwamo gesi asilia kujitafutia umaarufu wa kisiasa na kuwapotosha wananchi.

“Ni jambo la hatari na lisilo na tija kwa wanasiasa kujaribu kuigawa nchi vipandevipande kwa sababu ya kujitafutia umaarufu kwa kutumia rasilimali zataifa,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:

“Unawezaje kuwa na nchi moja na taifa moja wakati kila mmoja anadai rasilimali kutoka kwenye eneo moja ibakie na kunufaisha watu wa eneo hilo tu. Huwezi kuwa na nchi moja na yenye umoja wakati kuna nchi ya gesi asilia kule Mtwara, kuna nchi ya kahawa kule Kilimanjaro, kuna nchi ya chai na ndizi kule Bukoba,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:

“Kwa sababu kama gesi asilia inatakiwa kubakia na kunufaisha watu wa Mtwara tu, basi wenye haki zaidi ya kudai jambo hili siyo watu wa Mtwara, bali ni watu wa Msimbati ambako ndiko ilipogunduliwa gesi ambako ni maili 60 kutoka Mtwara, kilomita 200 kutoka Newala.”

Source: Mwananchi
Tafadhali msiwapuuze hawa watu wa Mtwara huenda wana sababu zao kubwa na za msingi wanatakiwa kusikilizwa na kuridhishwa hakuna kitakachoshindikana siyo vichaa hawa wana jambo lao la msingi na serikali inawapuuza ndiyo sababu wanaandamana na kusemea serikali mbovumbovu naamini kabisa wana sababu tena kubwa tu.

Naweza kusema moja tu ambalo linaweza kuudhi sana ikiwa hata ni wewe kwa mfano ni barabara ngapi za lami na kilometa ngapi zimejengwa nchini toka ile barabara ya lami kwenda Mtwara ilipoanza kujengwa? na ni kwanini haimaliziwi hadi sasa tena kilometa 60 tu masika yao kiangazi yao,wakati barabara nyingine za nyuma zimekamilika?mfano ile ya Dodoma hadi Mwanza na mengine mengi tu ya maudhi naamini yapo, nasisitiza tusiwapuuze tuwasikilize.naamini hakuna uchochezi sanasana ni hisia mbaya tu imejengeka katika vichwa vyao kwamba wanapuuzwa.
 
Hapa naona JK hajawaelewa watu wa Mtwara au kama kawaida yake amepotoshwa na wasaidizi wake. Na sioni atawazuia vipi Chadema kuzungumzia suala hili la gesi maana linaweza kuelezewa kwenye sera yao ya majimbo.
 
Vita kubwa itakayotokea muda si mrefu ndani ya Tanzania ni vita vya kidini. Uchochezi ulipofikia si rahisi kuurekebisha, na ninashindwa kuelewa hawa wachochezi wanapata wapi pesa za kuendeshea shughuli zao?. Kuwasafirisha waumini wa kiislamu toka mikoani kuja Dar kwenye mkutano Diamond Jubilee kwa siku tatu, hiyo pesa wanapata wapi?, na ni nani anayewapa vibali hivyo?. Na kibaya zaidi mpaka TV inaonesha hizo kashfa na kejeli Live. Jamani tunakwenda wapi?.
 
Real Silly, eti vurugu za kidini zilitaka kulitia doa taifa mwaka jana...kwa hiyo kuchomwa kote kule makanisa na watu kupigwa risasi bado sio doa?? Au alitaka na misikiti ichomwe moto ndio aone ni doa?? Halafu Sefue anakuja anasema kupunguza madaraka ya Rais ni hatari, kwa ujinga huu? Hembu kafie mbali huko, mmeishiwa hata kufikiri?? Shame on you!!
Wewe hujamwelewa! Taifa lingetiwa doa iwapo tu misikiti ingechomwa moto. Lakini kwa sababu vurugu ziliathiri makanisa, siyo mbaya sana, kwa maelezo hayo. Watanzania tuna kazi kwelikweli!
 
Mkuu amesha sema inatosha, uhuru alio wapa mliuchezea sasa ni wakati wa kuwapeleka ki mkapa mkapa, na hao wapinzani wanaoleta choko choko basi watakiona,hakuna cha nguvu ya umma wala mahakama za kimataifa, umefika wakati wa kuwa weka kwenye mstari.
 
Ndiyo kazi ya serkali ya maCCM zao ni kushughulikia matokeo ya matatizo na sio vyanzo.
 
Upotoshaji huu. Watu wa Mtwara hawazuii gesi kuja Dar, wanataka kujua baada ya kusafirisha gesi wao watabaki na nini? Au ndio yale ya Ogone kule Niger Delta. Hatukubali!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Lazima JK uwahakikishie wanaMtwara juu ya manufaa watakayopata wao. Tazama Barabara ya Mtwara inajengwa kwa muda wa miaka saba, mrahaba wa gesi ya Songosongo walikuwa wakilipwa Manispaa ya Ilala. Hivi tuamini tu kuwa serikali ina nia njema kwa watu wa Mtwara. Pamoja na kejeli za akina Muhogo? WE CANT BWANAAA!!!!!!!!
 
“Serikali haitavumilia vurugu wala ukabila kwa namna yoyote ile…. Mwaka 2012 vurugu zenye sura ya kidini zilianza kujitokeza ila sasa nasema kwamba hatutazivumilia kwa namna yeyote ile, inatosha,” alisema Rais Kikwete. HIVI ANAYESEMA HAYA ALIKUWA WAPI ASICHUKUE HATUA PALE YALIPOJITOKEZA HAYA?KWANINI TUSIAMINI YY NI DHAIFU?
 
Back
Top Bottom