Kikwete: Uvumilivu sasa basi...

Kikwete: Uvumilivu sasa basi...

this is silly; amejuaje zinatosha? walikuwa na kiwango walichotaka kufikia au kulikuwa na kiasi ambacho kilikuwa kinaweza kuvumilika na sasa kimepitilizwa?

Swali zuri na gumu MMM. Ila kwa kanuni ya JK ya udhaifu + unafiki, ni maumivu tu.
 

“Kwa sababu kama gesi asilia inatakiwa kubakia na kunufaisha watu wa Mtwara tu, basi wenye haki zaidi ya kudai jambo hili siyo watu wa Mtwara bali ni watu wa Msimbati ambako ndiko ilipogunduliwa gesi ambako ni maili 60 kutoka Mtwara, kilomita 200 kutoka Newala.”

Mh. Jakaya Mrisho Kikwete,

  1. Mbona unakosa busara na uelewa wa jambo dogo kama hili walilokuletea wananchi? Vitisho ni vya nini tena kwa wananchi wanaoomba kipande chao cha keki ya taifa?
  2. Hata kama kuna wanasiasa waliochochea hao wananchi kujitokeza kwa wingi, kuna ubaya gani kama matakwa yao ni ya msingi? Hivi huoni kuwa vilio vyao ni vya msingi?
  3. Hivi ni uungwana kwa maendeleo yote kulimbikiziwa Dar es salaam peke yake na wengine kuwa wakulima tu wasio na hata barabara?
  4. Kama nia kuu ya Taifa kwa sasa hivi ni kutumia gesi kuzalisha umeme, huoni kuwa ni vema kwa jenereta zikawekwa huko karibu na sehemu ya uzalishaji gesi ili kupunguza gharama za kuisukuma (pumping) hiyo gesi mpaka Dar kwa madhumuni hayo hayo ya kuzalisha umeme?
​
Mh, binafsi ninafikiri labda
yafuatayo yamekukumba;

  • (a) Labda una washauri wabaya
  • (b) Labda wewe binafsi hivi sasa ni mchovu wa kufikiria/kutakafari
  • (c) Labda wewe pamoja na wnaokuzunguka mmekuwa wavivu wa kupambanua
Ningekushauri utafute washauri wengine halafu upitishe uamuzi wa haraka kuwa mengi ya yanayowezekana yafanyikie huko huko gesi iliko ili maendeleo na ajira viweze kusambaa nchi nzima.
 
kwanini aseme leo hali yakale? Uogamwingine bwana!hiyo ndio janja yake ya kuukaribisha Wawekezaji! Mkuru bwana mweee!
 
Alihubili vurugu za kidini kwa kuweka kiwango sasa ameona kimevuka alipokusudia.
Uzuri Tanzania hatuna wachambuzi wa kuweza kuchambua kauli za viongozi kama JK.
 
Ninavyojua mimi raisi na serikali yetu ni vumilivu sana, wanatutisha tu na kwa haya yote watatuvumilia kwa kuwa hawana jibu zuri la kutupa, kama mafisadi, waeka hela nje, waliochukua rushwa na kutoa katika uchaguzi wa ccm walivumiliwa kwa nini na sisi tusivumiliwe iatkuwa ni kutuonea, tunakuomba mheshimiwa utuvumilie kama ulivyowavumilia watanzania wenzetu uliodhani wamaekukosea
 
Nimjeridhisha kuwa Kikwete kama Shonza, walizikwaa nafasi za juu kisiasa ili-hali hawastahili wala kujitambua! A very sad fact.

Tanzania ni ajabu la 8 duniani!
 
I conquer with H.E Jakaya the govt should now flex its muscles and stem out all sorts of hooliganisms coming in the forms of religious and resources activism.

Was it necesary to tell the ambasador all these gabbages? It would make a bit of sense if it was addresed to ccm members
 
Kuwaambia mabalozi, kwani mabalozi ndio wafadhili wa fujo? Kwanza angeanza na Mwigulu/Nape
 
Baba JK, lakini haya yote umeyalea wewe hasa ya udini. Umewaahidi waislamu Mahakama ya kadhi, kitu ambacho katiba inakikataa wazi wazi bila ya trouble ya constitutional interpretation! Maaskofu wamekueleza kuwa hakuna mfumo Kristo wakati madaraka yote ya juu nchi hii umewaweka wenzako wa dini yako! This is not a coincidence but a deliberate move. Baba JK, tafakari, chukua hatua!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kutokana na hili la gesi kuguswa nilijua asingekaa kimya. Si unajua ni mojawapo ya kilichobadilishwa na maisha ya Ridhiwani?

Kinyume na hapo ungekuta kuna historia ya hayati Riz 1
 
Mkuu amesha sema inatosha, uhuru alio wapa mliuchezea sasa ni wakati wa kuwapeleka ki mkapa mkapa, na hao wapinzani wanaoleta choko choko basi watakiona,hakuna cha nguvu ya umma wala mahakama za kimataifa, umefika wakati wa kuwa weka kwenye mstari.

Hakuna uhuru wowote aliotupa JK............... haya mambo yalianza wakati wa huyo Mkapa unayemsema. Kabla ya JF kulikuwa na BCS ambayo inamiliki majira. Baada ya kuona cheche, Nyaulawa (RIP) akaifunga ili agombee ubunge huko kwao. Then zikailbuka nyingine kabla ya kuseetle huku.

Kwa taarifa yako JK amefungia magazeti mengi kwa kipindi yake hiki kifupi kuliko Mkapa. Wanahabari wamekamatwa au kufa zaidi kipindi hiki. Tofauti ya Mkapa na JK ni kwamba Mkapa alikuwa haongei yeye anapiga mzigo tu bila kujali wananchi wanasema nini the mwisho wa siku tunapima matokeo. But this one anasikiliza maneno zaidi.
 
Kwa hiyo kumbe walikuwa wanavumilia vile vitendo vya kuwagawa watanzania na kuviona vya kawaida?
'Eti ina tosha' ina maana walipima kiwango cha uvunjifu wa amani na kuona kimetosha na amejuaje?

Kwa maneno hayo ya jk inaonesha wazi serikali imekuwa ikifumbia macho hivyo vitendo ndio maana vimekuwa vikitokea kila leo.

Na swala la gas bado hakujibu hoja za wanamtwara kama kawaida yake maji yakimfika shingoni ana watupia wanasiasa lawama badala ya kuwajibika!
 
Rais kaongea jambo zuri.rasilimali za taifa zinufaishe watu wote kama taifa na si kila mkoa udai rasilimali zake na kama ni suala la kila kwenye irasilimali zitumike palepale tu; sasa kwa nini tunafikiri katika level ya mkoa na isiwe level ya kata,kijiji au mtaa n.k bali mkoa?

Hakuna aliyesema rasilimali zitumike palepale tu, naona nyie ccm mna tatizo la kuelewa au mna dhamira ya makusudi kwa maslahi binafsi.

Uzuri ni kuwa hao mnaojaribu kuwahadaa nao ni wajanja, kumbukeni wanaweza pia kutumia sansuku la kura effectively.
 
Aseme ni nani alioanzisha udini kama si......y...y...? Aseme kama si mwanae aliyesema raisi ajae hatatoka kaskazini ng'oooooo? Aseme kama si mwanae aliyeshikwa na.........................hapa ni mtu kajiamlia tu kusema yakwake. Pia watuambie watekaji wa ulimboka, wauaji wa raia wote na waandishi wa habari????hizi hazikuwa vurugu??? na zile za polisi kuua raia kwenye maandamano ya arusha? si aanze na wale polisi wote wanafahamika awapeleke mahakamani???:majani7:
 
Back
Top Bottom