Kikwete unamuogopa Mwakyembe

Kikwete unamuogopa Mwakyembe

Ngurubhe

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2014
Posts
1,840
Reaction score
1,049
Hivi wizara hii ya uchukuzi ilikuwa na kasoro kiasi kwamba Mwakyembe alitakiwa kunyakuliwa kwenye wizara ya uchukuzi na kisha kupelekwa wizara nyingne?!!?!, au ndio kuwa mwakyembe akipelekwa huko sifa aliyokuwa nayo itafifia!!!?
Mzee huyu huwa akiamua anafanya kazi hata huko EAC tutamskia tu!!!

Dr Harison Mwakyembe alikuwa ni Waziri wa uchukuzi Wizara ambayo imekuwa na matatizo makubwa sana kiutendaji.

Kuanzia Dr Mwakiyembe alipokabidhiwa Wizara hiyo amefanya mambo makubwa sana kuhakikisha Sekta ya uchukuzi inafanya vizuri.

Moja ya mambo ambayo ameyashughulikia kwa nguvu zote ni usafirishaji kwa njia ya Reli ambayo ndio sababu kubwa ya yeye kuondolewa.

Ikumbukwe kuwa Viongozi wengi ndio wenye Makampuni ya usafirishaji kwa njia ya Barabara na kitendo cha kufuafua usafiri wa Reli ni pigo kubwa kwa watu wenye malori.

Ikumbukwe kuwa Viongozi wengi wanamiliki Malori mamia kwa mamia na wao ndio wenye tenda ya kubeba mizigo kutoka Viwandani kusambaza mikoani na nje ya Nchi.

Kwa mfano kipindi cha nyuma Cement kutoka Tanga kuja Arusha ilikuwa inasafirishwa kwa njia ya Reli kwa bei nafuu. Lakini sasa hivi ukienda Railway Station utaona Magari ndio yanayo shusha mizigo pale badala ya Train.

Sasa inamaanisha kuwa spidi ya Mwakyembe kufufua Reli ingekuwa ni pigo kwa wasafirishaji wa Malori kwani Train inasafirisha Mizigo kwa bei rahisi sana.

Kuchaguliwa kwa Samwel Sitta ni kuharibu System yote ambayo Dr aliweka kuhakikisha Sekta ya usafirishaji inakua.

Kama Sitta alivyoharibu Mchakato wa Katiba ndivyo atakavyo haribu Wizara ya Uchukuzi na Watanzania tusitegemee jipya ktk Wizara ya Uchukuzi.

Kuondolewa kwa Makyembe ni kwa faida ya Vigogo na Familia zao.
 
Hata mimi nimejaribu kuliangalia hili,nimeona kama kuna kupotezeana vile!!!!

Hivi umtoe Mwakyembe wizara ya uchukuzi halafu umlete msanii wa bongo muvi Sitta!!?


Huku si kuwatania watanzania!!?

Wanajitahidi sana kumpoteza kisiasa!!!, sijui wanamhofia nini!?!!!
 
Hivi wizara hii ya uchukuzi ilikuwa na kasoro kiasi kwamba mwakyembe alitakiwa kunyakuliwa kwenye wizara ya uchuguzi?!,B-) au ndio kuwa mwakyembe akipelekwa huko sifa aliyokuwa nayo utafifia!!!?
Mzee huyu huwa akiamua anafanya kazi hata huko EAC tutamskia tu!!!

Hapa ndipo ubaya wa nguvu nyingi za Rais unapoonekana, hivi hatuwezi kuweka kipengele kwenye katiba, kiwe kinawapa Wananchi nguvu ya kupinga mabadiliko yasiyo na tija kwa viongozi kama hili?. Huko nyuma tuliona vile Dr Magufuli alivyopelekwa kwenye vitoweo na kwenye barabara tukaweka mtu mwingine, tukamzungusha, baadae tukamrudisha tena ujenzi, hatuoni kwamba tunapoteza mtiririko wa kazi,sababu kila anayekuja, anaanza upya.

Sipingi mabadiliko,ila mengine ni hovyo kabisa, hivi hata huyu aliyepelekwa Ardhi, hivi kweli tuko makini na matatizo yaliyoko kule ardhi mpaka tunapeleka wanasiasa kule?
 
Hakuna cha nani wala nani , tanzania ni usanii mtupu.
 
Hata mimi nimejaribu kuliangalia hili,nimeona kama kuna kupotezeana vile!!!!

Hivi umtoe Mwakyembe wizara ya uchukuzi halafu umlete msanii wa bongo muvi Sitta!!?


Huku si kuwatania watanzania!!?

Kazawadiwa for being a good boy during KATIBA, wataalamu wa uchunguzi mtuambie kwa nini Mwakyembe kahamishwa.
 
Hapa ndipo ubaya wa nguvu nyingi za Rais unapoonekana, hivi hatuwezi kuweka kipengele kwenye katiba, kiwe kinawapa Wananchi nguvu ya kupinga mabadiliko yasiyo na tija kwa viongozi kama hili?. Huko nyuma tuliona vile Dr Magufuli alivyopelekwa kwenye vitoweo na kwenye barabara tukaweka mtu mwingine, tukamzungusha, baadae tukamrudisha tena ujenzi, hatuoni kwamba tunapoteza mtiririko wa kazi,sababu kila anayekuja, anaanza upya.

Sipingi mabadiliko,ila mengine ni hovyo kabisa, hivi hata huyu aliyepelekwa Ardhi, hivi kweli tuko makini na matatizo yaliyoko kule ardhi mpaka tunapeleka wanasiasa kule?

Jamaa haangalii ufanisi yeye anaangalia namna anavyoweza kuwafurahisha anaohisi ni watu wake,yaani eti wanapeana ulaji zamu kwa zamu🙂!!!!,,,
 
Kazawadiwa for being a good boy during KATIBA, wataalamu wa uchunguzi mtuambie kwa nini Mwakyembe kahamishwa.

Me wizara hizo nyingine siwezi sema mengi lakini hii ya mwakyembe ,nadhani kuna hira ba uvundo ndani yake yaaani kuna vitu mwakyembe haendani na kikwete yeye kama yeye au nawashauri wake wa karbu na pengine wakiwa wanahofia baadhi ya vitu,ukumbuke sita alitupwa huko EAC,baada ya kuwa anaikosoa sana safu ya uongozi wa juu na hasa reaction alizoonesha baada ta kukosa uspeaker.
Sasa basi makyembe amekuwa amejizolea umaarufu na alikuwa amepambana na uozo ulikuwa umejificha hko bandarini na kna watu hadi leo wanapga makofi na yamkini watardushwa tena kwani mwakyembe katoka!!!
 
Jamaa haangalii ufanisi yeye anaangalia namna anavyoweza kuwafurahisha anaohisi ni watu wake,yaani eti wanapeana ulaji zamu kwa zamu🙂!!!!,,,
Issue sio kufurahishana...hiyo ni strategic move ya kuweka mtu dhaifu ili mafisadi waweze kupiga hela na kusaidia uchaguzi uende vizuri mwaka huu...bandarini kuna hela ya kutupa na mwakyembe alikuwa mwiba mkubwa..lazima atoke ili mambo yaende vizuri ....
 
Me wizara hizo nyingine siwezi sema mengi lakini hii ya mwakyembe ,nadhani kuna hira ba uvundo ndani yake yaaani kuna vitu mwakyembe haendani na kikwete yeye kama yeye au nawashauri wake wa karbu na pengine wakiwa wanahofia baadhi ya vitu,ukumbuke sita alitupwa huko EAC,baada ya kuwa anaikosoa sana safu ya uongozi wa juu na hasa reaction alizoonesha baada ta kukosa uspeaker.
Sasa basi makyembe amekuwa amejizolea umaarufu na alikuwa amepambana na uozo ulikuwa umejificha hko bandarini na kna watu hadi leo wanapga makofi na yamkini watardushwa tena kwani mwakyembe katoka!!!

Hayo maneno
 
Kazawadiwa for being a good boy during KATIBA, wataalamu wa uchunguzi mtuambie kwa nini Mwakyembe kahamishwa.

mim nina mtazamo tofauti kidogo naona jakaya amefanya mahamuzi sahihi,sababu kule afrca masharik kuna makubaliano mengi tutayofanya hasa ya mambo hayo ya uchukuzi na mambo mengine ,nadhani mwakyembe amefanya mazuri hapa ndani,kule afrca mashariki panahitaji mtu chakarmu like mwakyembe.welldone mr kikwete.
 
Wanajitahidi sana kumpoteza kisiasa!!!, sijui wanamhofia nini!?!!!

Tatizo la mwakyembe ni papara halafu ana ndoto za kufanya biashara. Ni hatari sana kupewa wizara zenye miradi..ni mpigaji kama wengine wala msijidanganye. Huyo hatakiwi hata kuwa waziri abaki kuwa mbunge tu aendelee kupiga kelele
 
mwakyembe alikuwa anawabana sasa unga utakuwa unapita free.
 
Hivi aliyekuwa anashughulikia sana madawa ya kulevya ni nani.......?.......nashawishika kuamini kwamba.......Mwakyembe ameziba mengi hivyo funika kombe mwanaharamu apite.........
wamalize muda wao waondoke........washatuchosha..........aaaaaghh ........
 
Tatizo la mwakyembe ni papara halafu ana ndoto za kufanya biashara. Ni hatari sana kupewa wizara zenye miradi..ni mpigaji kama wengine wala msijidanganye. Huyo hatakiwi hata kuwa waziri abaki kuwa mbunge tu aendelee kupiga kelele
msijali sasa mtapitisha unga bure sasa.
 
wananchi wa jimbo la kyela tulipata faraja kubwa baada ya kukabidhiwa wizara hii, umeshindwa kuiga kwa mawaziri wenzio,
 
Hivi aliyekuwa anashughulikia sana madawa ya kulevya ni nani.......?.......nashawishika kuamini kwamba.......Mwakyembe ameziba mengi hivyo funika kombe mwanaharamu apite.........
wamalize muda wao waondoke........washatuchosha..........aaaaaghh ........
ccm wamefanya hujuma kumwamisha mwakyembe ili wapige dili zao
 
Hakuna cha nani wala nani , tanzania ni usanii mtupu.

Ndio usanii upo lakini hata wale wanaothubutu angalau kukemea maovu hata kwa kuigiza nao wanahamishwa uhmmmm kikwete,ama kweli fanya haraka uondoke;-)
 
Back
Top Bottom