Ngurubhe
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 1,840
- 1,049
Hivi wizara hii ya uchukuzi ilikuwa na kasoro kiasi kwamba Mwakyembe alitakiwa kunyakuliwa kwenye wizara ya uchukuzi na kisha kupelekwa wizara nyingne?!!?!, au ndio kuwa mwakyembe akipelekwa huko sifa aliyokuwa nayo itafifia!!!?
Mzee huyu huwa akiamua anafanya kazi hata huko EAC tutamskia tu!!!
Mzee huyu huwa akiamua anafanya kazi hata huko EAC tutamskia tu!!!
Dr Harison Mwakyembe alikuwa ni Waziri wa uchukuzi Wizara ambayo imekuwa na matatizo makubwa sana kiutendaji.
Kuanzia Dr Mwakiyembe alipokabidhiwa Wizara hiyo amefanya mambo makubwa sana kuhakikisha Sekta ya uchukuzi inafanya vizuri.
Moja ya mambo ambayo ameyashughulikia kwa nguvu zote ni usafirishaji kwa njia ya Reli ambayo ndio sababu kubwa ya yeye kuondolewa.
Ikumbukwe kuwa Viongozi wengi ndio wenye Makampuni ya usafirishaji kwa njia ya Barabara na kitendo cha kufuafua usafiri wa Reli ni pigo kubwa kwa watu wenye malori.
Ikumbukwe kuwa Viongozi wengi wanamiliki Malori mamia kwa mamia na wao ndio wenye tenda ya kubeba mizigo kutoka Viwandani kusambaza mikoani na nje ya Nchi.
Kwa mfano kipindi cha nyuma Cement kutoka Tanga kuja Arusha ilikuwa inasafirishwa kwa njia ya Reli kwa bei nafuu. Lakini sasa hivi ukienda Railway Station utaona Magari ndio yanayo shusha mizigo pale badala ya Train.
Sasa inamaanisha kuwa spidi ya Mwakyembe kufufua Reli ingekuwa ni pigo kwa wasafirishaji wa Malori kwani Train inasafirisha Mizigo kwa bei rahisi sana.
Kuchaguliwa kwa Samwel Sitta ni kuharibu System yote ambayo Dr aliweka kuhakikisha Sekta ya usafirishaji inakua.
Kama Sitta alivyoharibu Mchakato wa Katiba ndivyo atakavyo haribu Wizara ya Uchukuzi na Watanzania tusitegemee jipya ktk Wizara ya Uchukuzi.
Kuondolewa kwa Makyembe ni kwa faida ya Vigogo na Familia zao.