Nimejaribu kufuatilia Uzi huu ili nione Lumumba wataegemea kwa Magu au baba lao la usanii nimegundua wako njia panda.
Kama kweli Magi alimjibu hivyo tena kwa ujasiri JK nampongeza sana kwani ndio majibu sahihi alipaswa kumpa.
Ila Magu ashauriwe kuwa kwa vile vikao vya kamati kuu yeye anaenda kama mwalikwa kutokana na cheo chake aanze kuvikacha. Kila kikipangwa naye awe na ratiba nyingine, awaache wapige majungu yao yeye achape kazi na kwenye ujinga awashughulikie.
Tumegundua kuwa Uchaguzi wa mameya wowote ukiokuwa na matatizo chanzo ni uongozi wa juu wa ccm
Sioni sababu ya Magu kuwakacha, aendelee nao tu na penye ujinga awape live, hawawezi mfanya kitu.
Ukweli ni kuwa JK kwa muda wote wa utawala wake amesuka nyavu za kila aina ya utapeli katika siasa ambazo yeye mwenyewe pekee anaujua msingi wa kutufanyia hivi Watanzania. Sasa hapa anajaribu kufanya mambo ambayo yeye anayainjinia ili mwisho wa siku Magu aonekane mbaya, mnafiki sana. Alivyofaulu kupiga unafki kwa rafiki yake Lowassa amefanya km kamchezo kutaka kumnafikisha kila anayemwona anatakakumharibia kariba yake anayodhani bado anayo, hataki kuona mtu anakuja mbele yake anafanya vitu ambavyo vinawafanya Watanzania waone kuwa walikuwa wakichezewa akili pale wanapouakisi utawala wa JK.
Kwa bahati mbaya pia anajinafikisha ktk namna ambayo anataka aonekane mzuri ktk chama bila kujali tena Watanzania wanaathirikaje na maamuzi yake kutoka chamani, namshukuru rais kwa kuonesha msimamo mapema.
Inasikitisha sana kwa kiongozi kutanguliza maslahi ya chama badala ya Tanzania kwanza.
JK anajiona yeye na makanjanja wenzake ndio wenye chama na chama ndio kila kitu , wananchi baadae.
Hatari nyingine ni kasumba ya viongozi wa vyama kujenga dhana kuwa pale chama kinapofanikisha ushindi kwa mwanachama wake ktk ngazi yyte ya uongozi kinaona kwamba kimempa zawadi huyo mtu, hapo ndio mwanzo wa matatizo yetu makubwa unapoanzia.
Wakati wengine wanaona dhana ya uongozi ni uzalendo unaoongozwa na dhamira ya kutaka kuwasaidia watu kuondokana na matatizo yanayowakabili na kupiga hatua za kimaendeleo, wengine wanaona ni zawadi, hapo usishangae kiongozi wa chama akiwaambia viongozi wa serikali 'kisingekuwa chama wasingepata huo uwaziri na urais' si ajabu kuona watu wanatumia fedha na kila aina ya hila kutaka kupata uongozi, wakati USA wanatumia fedha na mitandao ya watu kupata uongozi kimsingi wanatafuta nafasi kwa dhati ya kuwatumikia watu wao ili kutokana na kazi hiyo wapate heshima yao, ni nafasi ya kutafta heshima na si mali km ilivyo kwa wengi wa viongozi wetu.