Hawa watu hawajawahi kuwa pamoja siku zote za umaarufu wao. Kumbuka wakati JK alipoingia madarakani alimfanya nini Magufuli. Pamoja na malalamiko kama si maombi anuai ya watu kwamba apewe wizara ya ujenzi ama uwaziri mkuu, ndivyo kasi,ari na nguvu zaidi ya kumdidimiza kwa lengo la kumpotezea kabisa ilivyoshika kasi ingawa jamaa alikomaa kila alikosukumiwa.
Kumrudisha wizara ya miundombinu ilikuwa ni aibu tu kutokana na fedheha zilizokuwa zikifanywa na wateule wa jk.
Kwenye uchaguzi wa mgombea wa ccm kila mtu anajua hata hawa wawili wanajua kwamba JPM hakuwahi kuwa chaguo la Jk hata katika tatu bora hakuwemo. Upepo wa anguko la kishindo la ccm ndio uliomsukumia embe JPM lakini hakuna asiyefahamu kwamba hakuwa mlengwa.
Tofauti zilionekana wazi hata wakati wa kampeni. Morogoro wakati JK akijisifia kwamba amelitoa taifa mbali na hadi kulifikisha hapa kafany akazi kubwa, mgombea uraisi alisimama na Ku crush kwa nguvu kwamba tumefika hapa sababu ya ufisadi tu!.
Anachokifanya JK kwa sasa ni unafiki kama asili ilivyo ili kujaribu kujivalisha kinga ya kutumbuliwa kwake, familia yake na watu wake wa karibu kitu ambacho naona kama kinatoa harufu ya kufanikiwa. Lakini leo ikitokea Mkwere au mmoja wa watu wake akawa raisi, mtaona JPM atakavyofanywa!. Msisahau jamaa anaendeshwa na utashi wa visasi na vinyongo, vikipaliliwa na ubaguzi na upendeleo. Kama Saddam vile!.
Kusema wameanza leo kutofautiana ni kujaribu kufupisha historia kwa kuondoa mizizi.
Filamu ndiyo inaanza. Hapa niutangulizi. Kwa undani zaidi, stay connected!
Ciao!.