Kikwete na familia yako na Kamati ya Maadili hamtaikimbia aibu hii mliyoitengeneza

Kitu cha pili, Urais sio Chama, Urais ni MTU ndio mana hata Kikwete awamu ya kwanza alishinda kwa zaidi ya asilimia 80% kwa sababu watu walimpenda mtu na sio chama kadharika kwa jambo hili watu walimpenda Lowasa sio CCM.
.

Masahihisho kwenye red: Urais TAASISI......
 
Sasa mwendo ni Lowassa kwenda Upinzani, tutampigia kura tu... au awape support UKAWA...

Tumeichoka CCM, ni hasara na uonevu mtupu...!!! UKAWA washachukua nchi haraka kabisa...!!!
 
Nyie binadamu mna roho ngumu ,Bado mnaamini mtu wenu atakuja kushika nchi hii .!
halafi hawa kina Fandre ni wale watu wanaojifanya wanaijua sana mistari ya vitabu vitakatifu lakini wameumbuka
attachment.php

leo wanabariki wakikosa kesho wanatoa laana
Nina Imani Safari ya Matumaini ya Mzee Lowasa haitakufa mpaka malengo yake yatimie
ukiangalia mchakato mzima JK mtuwake hayupo na Lowassa sasa yamekwisha ameungana na wenzake
lakini hawa wachumia tumbo RUKSA kumshawishi mamvi ahamie ACT ili aje apambane na magufuli na Dr Slaa km ana safari ya Matumaini
 

Attachments

  • Mwamasika bado askofu.jpg
    Mwamasika bado askofu.jpg
    43.6 KB · Views: 505
Dr. Magufuli mara moja anatakiwa apate watu waaminifu watakaomwongoza kutengeneza timu yake, avunjilie mbali iliyopo iliyokuwa imejiandaa kuongozwa na remote kutoka nje ya Ikulu
 
We ndo mzushi kuliko wote, yaani ulitaka membe aingie iwe kama nyumba yao ikulu au...mwambie ndugu yako membe kuwa.......ikulu si ya kaka,ako

wewe bonge la boya yaani ulitaka hii nchi wapeane kama walivyokubaliana mwaka 2005 hili sio shamba la bibi hii ni tz yetu sote
 
Bado nazingoja siku chache sana kwa baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi akiwemo Mwenyekiti wao kukutwa na aibu kubwa ambayo hawataweza kuizuia.

Ndugu zangu jambo hili halihitaji uwe na macho sita au vichwa viwili au kilo 100 za ubongo au uwe una kipaji maalum ndipo utambue kwani jibu lolote la UBAYA mwishowe huwa ni AIBU.

Kama kigezo cha URAIS ni USAFI na UADILIFU basi CCM hakuna hata mmoja ambaye angepita kati ya majina yote yale LAKINI kwakua viliwekwa vigezo vingine vingi saidizi nina imani Mzee Lowasa aliwazidi wengine wote na hilo limejidhihirisha jana mbele kabisa ya Halmashauri Kuu baada ya wajumbe wote kuimba kwa kumsifia Lowasa mbali na kuwa jina lake halikuteuliwa katika Tano Bora.

Dhambi hii ya usaliti wa Kikwete kwa rafiki zake itamtafuna daima kwa uoga wa kuwajibishwa kwa maovu yao mengi waliyoitendea nchi yetu pamoja na watanzania.

Nina Imani Safari ya Matumaini ya Mzee Lowasa haitakufa mpaka malengo yake yatimie na jambo hili ni wazi kwa sababu tayari mzee huyu alikwisha pokelewa na kukubaliwa na watanzania.

Hapa nayakumbuka maneno ya kiongozi mmoja wa dini alisema...."Mungu akitaka kumuangusha mti humtia uchizi ili asione pale anapokosea na mwishowe kuanguka"
Nami leo nimeuona uchizi uliowekwa ndani ya CC, Kamati ya Maadili na kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na kwa hiyo wataanguka tu mbele ya Lowasa siku si nyingi.

Kama malengo ya Lowasa ni kutatua shida za watanzania, kuwatumikia na kuwainulia maisha yao kwa kuongeza kasi ya kukua kwa Uchumi Mdogo na ule Mkubwa basi nia hii bado inaweza kutekelezeka ama ndani ya CCM ama nje ya CCM kisha akina Kikwete watakuja kutuambia kwanini walikua wanamuogopa Lowasa!

Ni jambo la kweli, Magufuli Urais alikua anajaribu tu na hakua amejiandaa kwa namna yeyote ile kuwa kiongozi wa juu wa Taifa na jambo hili litamfanya kuwa Rais atakayeburuzwa na maamuzi ya watu wengine kuliko hata Rais aliyekwisha mtangulia na hapa ndipo alipokua anasema Lowasa anahitajika Rais mwenye maamuzi magumu.

Kitu cha pili, Urais sio Chama, Urais ni MTU ndio mana hata Kikwete awamu ya kwanza alishinda kwa zaidi ya asilimia 80% kwa sababu watu walimpenda mtu na sio chama kadharika kwa jambo hili watu walimpenda Lowasa sio CCM.

Ndugu zangu, AIBU HII isiyokwepeka itamkuta kila unayemjua amepindisha na kumharibia aliyestahili kuwa mgombea kupitia CCM na kuwa Rais wa Tz kwa awamu ya Tano.

Hivi karibuni sana mambo haya yatajiri...

Rafiki Mnafiki na mwenye wivu ni hatari sana zaidi hata ya shetani.

Hebu ondokeni huko Dodoma sasa mkaone familia zenu. Dili limebutuka.
 
Sijajuaga km jamaa ana roho mbaya kiasi kile hv Wakwere ndo roho zao zilivyo kuanzia Leo ntakuwa nawaogopa sana.
 
Jamani kubalini tu matokeo tayari imeshatokea!!
Tatizo watu mlishapanga mshindi ni nani ndio maana kila kitu mnaona kimekosewa na mmeonewa!Watu mlishajenga matokeo yenu kichwani ndio maana mnaona haki haikutendeka!Ushindani ni lazima mmoja ashinde na wengine washindwe!ni nini ambacho hamtaki kukubali??tufanyeje labda sasa kama imeshatokea?
 
lowasa mwenyewe kashakubaliana na hali halisi ya kilichotokea jamani
 
Fandre, game imeshaisha hii. Endeleeni na maisha yenu sasa.

Somo moja kwa wanasiasa wa CCM wenye ambition ya kugombea uRais huko mbele: kamwe usikubali uteuzi wa kuwa Waziri Mkuu. Hakuna Waziri Mkuu wa Tanzania atakayekuja kuuonja uRais
 
Mtoa mada Lowassa kawazidi vitu gani hao wengine?wewe ni mpambe wa siasa na hujui kitu...Lowassa ni mlafi wa madaraka na hana jipya na hatutaki kiongozi ambaye anapitishwa na mtu kwa sababu ya urafiki wala udugu.
 
kaka hua naheshimu commentaar zako ila humjui magufuli,Magufuli ni corrupt kuliko mnavyodhani,utakumbuka maneno yangu,Ccm wako smart sana,

Mimi sio big fan wa Magufuli na niko on the record humu kumpinga mambo mengi
but Lowassa ni mbovu zaidi...

Lowasa kamfanya Magufuli aonekane 'malaika'
na sasa wana CCM washaamua
 
Back
Top Bottom