Kikwete mrudishe ROM asaidie kuokoa jahazi Zanzibar

Mkuu Mwanakijiji, just take note, kama ROM ulimaanisha, Ramadhani Omari Mapuri, please be carefuli, asije kuwa ni baba mtu!, yeye jina lake ni Omari, Ramadhani ni la Baba yake na Mapuri ni la ukoo!.

Wazanzibari, hupenda kutumia majina matatu, yale mawili ni ya baba zao, mfano, Abedi Amani Karume, alimzaa Amani Abedi Karume, ili utenganishe Karume baba na Karume mtoto, ni lazima majina mawili ya mwanzo, yakae kwenye the right sequence, yaani Amani Abedi, na Abedi Amani, hivyo unaweza kukuta huyo ROM kwa maana ya Omari Ramadhani unaweza kukuta ndie baba yake kama alivyo Thabit Mohamed Kombo na mwanae Mohamed Thabit Kombo ila umeeleweka!.

Wengine ni Ali Mohamed Shein na mwanae Mohamed Ali Shein,
Mohamed Ghalib Bilal na mwanae Ghalib Mohamed Bilal
Seif Shariff Hamad, na mwanae Hamad Seif Shariff etc etc.
 
Jambo la msingi ni kutatua kasoro zilizopo
ndani ya muungano,ili kuliweka katika msingi
bora wa sheria na uhalali wake.
Kero hizi zilikuwepo tangu uanzishwaji wake na
watu wengi wa zanzibar wamechukua kama ajenda
ya kuthubutu kuuvunja muungano.Nawahakikishia m
wazanzibari wote pamoja na UAMSHO kuwa MUUNGANO
Utadumu milele na wao wataondoka zao waende wanakotaka
kwenye kuishi,kama hawaamini basi wasubiri tume ya katiba imalize kazi yake.
PERIOD.

Ikiwa wewe ndo yule Mungu aitwae (Allah) maneno yako ni kweli, la ikiwa ni binadamu basi unacheza kamari na majambazi wenye silaha hapo cjui kama hata ukashinda utapewa au,,,,,,,,,,,,,,???
 
Hivi huu muungano ni kwa faida ya nani?

Huu Muungano Ulikuwa ni wa kusitirisha COLD WAR kuzuia Mapigano kati ya USA na USSR na CHINA usifanyike kwenye

Pembe hii; lakini COLD WAR is no MORE; na nadhani MUUNGANO hauna Umuhimu... Nadhani Upo tu kwasababu ya CCM

Kama CCM ikiteremka Madarakani na Muungano Unakimbia ... kwahiyo Subira huvuta kheri 2015 itawezekana kabisaaa

Zanzibar itaondoka na kuanza kufurahia Mafuta yake; na Tanganyika Itaondokana na Manunung'unizi kuhuzu Z'BAR
 
Omari Ramadhani Mapuri ni miongoni mwa wahafidhina huko Zenji ambao walijengwa na Komandoo. Mwingine ni yule aliyekuwa Naibu Waziri Kiongozi wa awamu iliyopita Bw. Shamuhuna. Hakika hawa wamepitwa na wakati na siasa za Zanzibar. Hawa walikuwa miongoni mwa watu wsioamini na wasiotaka mtu toka kisiwa cha Pembe aitawale Zanzibar; sasa imekuwa na siasa za uhasama Zanzibar zimepungua kwa kiasi kikubwa wakipewa hatamu hawa waungwana tutarudi tulikokuwa ambapo watu walikuwa hawashirikiani hata misibani.
 
Namzungumzia Ramadhani Omar Mapuri...do u guys still remember him!?

Bila shaka namkumbuka ROM. Mara ya mwisho kabla hajaondoka nchini alikuwa ni waziri wa mambo ya ndani na kama sijakosea alikuwa pia ni katibu mwenezi wa CCM yaani NAPE wa wakati huo. Alikorofishana na waandishi baada ya kushabikia kipigo cha waandishi wa habari waliopigwa na askari magereza. Baada ya maneno yake ya kashfa kwa waandishi alitakiwa aombe radhi lakini aligoma. Matokeo yake vyombo vyote vya habari viliamua kumsusia habari zake zote na huo ukawa mwishi wa ukatibu mwenezi wa CCM ana hatimaye uwaziri.
 
Alikuwa na vyeo vyote kwa wakati mmoja?
Bila shaka namkumbuka ROM. Mara ya mwisho kabla hajaondoka nchini alikuwa ni waziri wa mambo ya ndani na kama sijakosea alikuwa pia ni katibu mwenezi wa CCM yaani NAPE wa wakati huo. Alikorofishana na waandishi baada ya kushabikia kipigo cha waandishi wa habari waliopigwa na askari magereza. Baada ya maneno yake ya kashfa kwa waandishi alitakiwa aombe radhi lakini aligoma. Matokeo yake vyombo vyote vya habari viliamua kumsusia habari zake zote na huo ukawa mwishi wa ukatibu mwenezi wa CCM ana hatimaye uwaziri.
 
Hatuwezi kuwaacha wazanzibar waende zao bure,kamwe haliwezekani hili
kama kuna mambo ya kutisha na ya hatari kutokea hapa Jamhuri ya muungano
wa Tanzania ,TANGANYIKA NA ZANZIBAR(UNGUJA NA PEMBA) basi ni hili la kuwaacha
wazanzibar waende zao.
Sintakubali hata kwa neno moja kukubali kutengana na zanzibar.Ni dhambi kubwa sana.tunaongea kwa
kwa maneno rahisi sana lakini hatujui implications zake,hatujui effects zake,hatujui nini kitatokea baada ya
mfarakano huu.Hakuna anayejua nini kitatokea,
Wa-Tanzania tuungane kwa nguvu zote kuhakikisha MUUNGANO unadumu milele daima na kizazi chetu kinaukuta.
Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Africa
Mungu Bariki Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
naunga mkono hoja
P
 
Siku moja nimemtumia mtu ( mtu anayeweza kuwa na jibu)text msg mtu,namuuliza,"Ni nani yule mwanasiasa wa Zanzibar, Ramadhani OthmanMapuri? Bado yupo Serikalini"?.
Akanijibu,"Ni Balozi wa Tanzania China."
 
Wewe Mzee una siasa kali za kihafidhina siku zote japo huwa unajipambana unapenda mageuzi lakini sio kweli.
Zanzibar ndani ya muungano wetu huu adhimu ni the minority, kwenye muungano yote the minority ndio huwa wanasumbua kama ilivyo kwenye ndoa za mitala, mke mdogo ndio mwanzo WA chokochoko. Hivyo being a very sensitive to handle, isipokuwa mhafidhina mke mdogo atakupeleka puta!.

Tulipoungana , tulikubaliana tunaunda nchi moja ya JMT, na Zanzibar kuwa na mamlaka yake ya ndani kwa mambo ambayo siyo ya muungano. Zanzibar ilikuwa inachangia gharama za uendeshaji wa muungano, wimbo wa taifa na bendera moja.

Mara ghafla akagoma, mara naomba wimbo, bendera, katiba, sasa anajiita nchi. Kwa vile mtu kapenda kwa dhati, kila atakacho bi mdogo atapewa, na hata afanye vitimbi vipi, talaka hapewi!.
P
 
Zanzibar ndani ya muungano wetu huu adhimu ni the minority, kwenye muungano yote the minority ndio huwa wanasumbua kama ilivyo kwenye ndoa za mitala, mke mdogo ndio mwanzo WA chokochoko. Hivyo being a very sensitive to handle, isipokuwa mhafidhina mke mdogo atakupeleka puta!.

Tulipoungana , tulikubaliana tunaunda nchi moja ya JMT, na Zanzibar kuwa na mamlaka yake ya ndani kwa mambo ambayo siyo ya muungano. Zanzibar ilikuwa inachangia gharama za uendeshaji wa muungano, wimbo wa taifa na bendera moja.

Mara ghafla akagoma, mara naomba wimbo, bendera, katiba, sasa anajiita nchi. Kwa vile mtu kapenda kwa dhati, kila atakacho bi mdogo atapewa, na hata afanye vitimbi vipi, talaka hapewi!.
P
Paskali bwana. Watu watafoka hii analysis yako kama vichaa
 
Mhhhm
Omari Ramadhani Mapuri ni miongoni mwa wahafidhina huko Zenji ambao walijengwa na Komandoo. Mwingine ni yule aliyekuwa Naibu Waziri Kiongozi wa awamu iliyopita Bw. Shamuhuna. Hakika hawa wamepitwa na wakati na siasa za Zanzibar. Hawa walikuwa miongoni mwa watu wsioamini na wasiotaka mtu toka kisiwa cha Pembe aitawale Zanzibar; sasa imekuwa na siasa za uhasama Zanzibar zimepungua kwa kiasi kikubwa wakipewa hatamu hawa waungwana tutarudi tulikokuwa ambapo watu walikuwa hawashirikiani hata misibani.
Mhhh
 
Back
Top Bottom