MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,185
- 24,055
Wakati akifungua kikao cha NEC kilichopokea mapendekezo ya Kamati Kuu kuhusu Rais John Magufuli kuwa Mwenyekiti mpya, Jakaya Kikwete alisema kuna propaganda za wafitini ambao walifikia hatua ya kuandika kwenye gazeti hivi karibuni habari inayosema “Uteuzi wa Magufuli kupingwa NEC”.
Alisema habari hiyo ni potofu, kwa sababu hakuna kitu kama hicho na hakikutokea na kwamba walioiandika, inaonesha wana mtambo wa kufyatua uongo.
“Kuna watu wana viwanda na mitambo ya kufyatua uongo. Hawa wanazalisha bidhaa mpya zenye uongo na uzushi kila siku,” alisema.
Aidha, alisema wapo watu hawalali na wana taabu mno, wanapoona CCM ina nguvu na inaendelea kuwa imara. Alisisitiza kuwa CCM haibabaishwi na uongo na uzushi wa watu hao; kwani mara zote kama kuna jambo ndani ya CCM, hupelekwa katika vikao husika, kisha hujadiliwa na kufikia maafikiano.
Alisema habari hiyo ni potofu, kwa sababu hakuna kitu kama hicho na hakikutokea na kwamba walioiandika, inaonesha wana mtambo wa kufyatua uongo.
“Kuna watu wana viwanda na mitambo ya kufyatua uongo. Hawa wanazalisha bidhaa mpya zenye uongo na uzushi kila siku,” alisema.
Aidha, alisema wapo watu hawalali na wana taabu mno, wanapoona CCM ina nguvu na inaendelea kuwa imara. Alisisitiza kuwa CCM haibabaishwi na uongo na uzushi wa watu hao; kwani mara zote kama kuna jambo ndani ya CCM, hupelekwa katika vikao husika, kisha hujadiliwa na kufikia maafikiano.