Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,792
- 1,846
Mbio za muungano zilifikia kilele chake pale JK alipoamua kuuvulia njugaMuungano, na kuahidi kuupatia ufumbuzi wa kisiasa. Muungano ulijengwa na JK(Kambarage) na kusua sua bila mafanikio, na ukatafutiwa ufumbuzi na JK (Kikwete). Maraisi wote waliopita hawakuisha kuwaita wadai haki zao kuwa ni wahuni.
Mwaka 2000 mara baada ya uchaguzi mkuu Wazanzibari zaidi ya 200 waliuliwa na bunduki na helkopta zilizonunuliwa kwa fedha ya walipa kodi, kwa amri ya Mkapa. Na wote waliouwawa aliwaita wahuni, huku akimtafuta muhuni mkuu, Sheikh Sharif na Prof Lipumba. Na baada ya muda si mrefu nao wakashikwa na kutiwa ndani. Kwa upande wangu huo ndio ulikuwa mwisho wa demokrasia, na mwanzo wa udikteta. Hata wale aliyewauwa Mwebechai nao walikuwa wahuni tu, na sheikh ponda ndio kiongozi wa wahuni. Ilionekana kana kwamba Mkapa alikuwa Rais wa wananchi wahuni nchi nzima.
JK wakati huo akiwa katika serikali ya Mkapa, na kwa ujumla alikuwepo ktk serikali zote zilizopita, aliyaona mapungufu yaliyosababisha matatizo hususan, Zanzibar. Na ndio maana alipoingia madarakani miaka mitano iliyopita alikuwa ni Raisi wa kwanza kukiri kuwa Zanzibar kuna mpasuko wa kisiasa. Kauli hii ilifurahiwa na wengi, na kuandikwa karibu katika magazeti yote TZ. Kwani kuutatua mgogoro wa zaidi ya miaka 40, si lelemama.
Baada ya miaka takriban mitano toka aingia madarakani, yaonyesha dalili nzuri ya kutimizwa kwa ahadi yake. Siri kubwa ya kufanikiwa katika kutatua tatizo hilo, ni kuwaachia Wazanzibar wenyewe kuwa wachezaji wakuu, naye ni kam,a mtazamaji na mshauri. Viongozi wa Zanzibar wakaamua Serikali ya mseto, na baadae suala likatupwa kwa wananchi kupitia kura ya maoni, 66% wakapitisha pendekezo. Na baada ya hapo ikahitajika kufanyiwa marekebisho katika katiba, nayo yakapitishwa kwa kishindo na Baraza la wawakilishi. Kwa kipindi hiki chote hakuuwawa hata mtu mmoja, kana kwamba wahuni waliondoka alipostaafu Mkapa.
Kilichonishangaza mimi ni kuwaona wasomi, wanasheria, magazeti na hata hapa JamiiForums, kupiga kelele sana hasa pale Katiba ilipoguswa. Na wengine kukiita kitendi hicho kama ni cha Kihaini, na hoja hiyo ikaungwa mkono na Watanganyika wengi tu. Sasa najiuliza wataundaje serikali ya mseto bila kugusa katiba? Au JK alipoonyesha dhamira ya kutatua mgogoro wa kisiasa Zanzibar walielewa nini? Au kulikuwa na mpaka katika ufumbuzi huo? Kama kulikuwa na mpaka ni nani aliouweka huo mpaka? N i maswali ambayo kila siku najiuliza toka kura ya maoni ipigwe na katiba kupitishwa bila majibu. Na ninapokaribia kupata jibu, basi ni jibu gumu sana, kuwa hawa watu ni watu wa shari hawataki amani.
Na kama hivyo ndivyo, basi kundi hili liwe NGO au la kidini ndilo lililokuwa likifaidika na Muungano kwa njia moja au nyingine. Ninasikitika kusema kuwa kundi hili halina nafasi katika Tanzania ya sasa, na si tu kuwa limepotea njia bali litakufa kifo kibaya. Sioni haja yeyote ile ya kuulinda Muungano au kipengele cha katiba hata kwa kuuwa wananchi kwa kutumia madaraka vibaya. Vikundi kama hivi havifai kabisa katika jamii, na popote tunapokutana navyo ni lazima tuvionye na kuvitokomeza.
Ninapigwa na bumbuwazi zaidi pale ambapo hoja zinazotolewa ni za kulaumu tu. Ningefurahi kama wangekuja na maelezo makini juu ya mapendekezo ya utatuaji wa mgogoro huo. Bado mnayonafasi ya kutoa hoja zenu, ni vipi mlihitaji mgogoro huo utatuliwe ili wananchi wa pande zote mbili zinazohusika huko Zanzibar wakarithika nazo. Msipoweza kutoa hoja basi malalamiko yenu hayana msingi kabisa.
Lazima ikumbukwe kuwa polisi waliokuwa wanatumwa Zanzibar, ni makomandoo wa jeshi waliokuwa mafunzoni wakvishwa mavazi ya polisi. Watu hawa hawakujifunza kutuliza ghasia, bali kuuwa na hivyo ndivyo walivyofanya huko Zanzibar. Si hivyo tu bali vile vile wali wabaka watoto wa kike mbele ya wazazi wao. Kweli tuko tayari kuulunda muungano kwa dhamani hii? Hapana hii si Tanzania bali ni SOWETO. Hata mkinukuu maneno ya mwalimu ya mwaka 1964, bado si tiketi ya kuulinda muungano kwa dhamani hii.
Hapa alipofikia Kikwete anahitaji pongezi, kwa hali yeyote ile si rahisi kuutatua mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 40 kwa amani kama tulivyoshuhudia. Hii ni sawa kama Rais Obama akafanikiwa kuutatua mgogoro wa Israel- Palestina. Ni nini anachoweza kupewa zaidi ya zawadi ya Nobel. Tumsifu JK kwa hapa alipotufikisha, na tuelewe kuwa ukuzaji wa uchumi unategemea sana amani ya nchi. Hongera Kikwete!!
Mwaka 2000 mara baada ya uchaguzi mkuu Wazanzibari zaidi ya 200 waliuliwa na bunduki na helkopta zilizonunuliwa kwa fedha ya walipa kodi, kwa amri ya Mkapa. Na wote waliouwawa aliwaita wahuni, huku akimtafuta muhuni mkuu, Sheikh Sharif na Prof Lipumba. Na baada ya muda si mrefu nao wakashikwa na kutiwa ndani. Kwa upande wangu huo ndio ulikuwa mwisho wa demokrasia, na mwanzo wa udikteta. Hata wale aliyewauwa Mwebechai nao walikuwa wahuni tu, na sheikh ponda ndio kiongozi wa wahuni. Ilionekana kana kwamba Mkapa alikuwa Rais wa wananchi wahuni nchi nzima.
JK wakati huo akiwa katika serikali ya Mkapa, na kwa ujumla alikuwepo ktk serikali zote zilizopita, aliyaona mapungufu yaliyosababisha matatizo hususan, Zanzibar. Na ndio maana alipoingia madarakani miaka mitano iliyopita alikuwa ni Raisi wa kwanza kukiri kuwa Zanzibar kuna mpasuko wa kisiasa. Kauli hii ilifurahiwa na wengi, na kuandikwa karibu katika magazeti yote TZ. Kwani kuutatua mgogoro wa zaidi ya miaka 40, si lelemama.
Baada ya miaka takriban mitano toka aingia madarakani, yaonyesha dalili nzuri ya kutimizwa kwa ahadi yake. Siri kubwa ya kufanikiwa katika kutatua tatizo hilo, ni kuwaachia Wazanzibar wenyewe kuwa wachezaji wakuu, naye ni kam,a mtazamaji na mshauri. Viongozi wa Zanzibar wakaamua Serikali ya mseto, na baadae suala likatupwa kwa wananchi kupitia kura ya maoni, 66% wakapitisha pendekezo. Na baada ya hapo ikahitajika kufanyiwa marekebisho katika katiba, nayo yakapitishwa kwa kishindo na Baraza la wawakilishi. Kwa kipindi hiki chote hakuuwawa hata mtu mmoja, kana kwamba wahuni waliondoka alipostaafu Mkapa.
Kilichonishangaza mimi ni kuwaona wasomi, wanasheria, magazeti na hata hapa JamiiForums, kupiga kelele sana hasa pale Katiba ilipoguswa. Na wengine kukiita kitendi hicho kama ni cha Kihaini, na hoja hiyo ikaungwa mkono na Watanganyika wengi tu. Sasa najiuliza wataundaje serikali ya mseto bila kugusa katiba? Au JK alipoonyesha dhamira ya kutatua mgogoro wa kisiasa Zanzibar walielewa nini? Au kulikuwa na mpaka katika ufumbuzi huo? Kama kulikuwa na mpaka ni nani aliouweka huo mpaka? N i maswali ambayo kila siku najiuliza toka kura ya maoni ipigwe na katiba kupitishwa bila majibu. Na ninapokaribia kupata jibu, basi ni jibu gumu sana, kuwa hawa watu ni watu wa shari hawataki amani.
Na kama hivyo ndivyo, basi kundi hili liwe NGO au la kidini ndilo lililokuwa likifaidika na Muungano kwa njia moja au nyingine. Ninasikitika kusema kuwa kundi hili halina nafasi katika Tanzania ya sasa, na si tu kuwa limepotea njia bali litakufa kifo kibaya. Sioni haja yeyote ile ya kuulinda Muungano au kipengele cha katiba hata kwa kuuwa wananchi kwa kutumia madaraka vibaya. Vikundi kama hivi havifai kabisa katika jamii, na popote tunapokutana navyo ni lazima tuvionye na kuvitokomeza.
Ninapigwa na bumbuwazi zaidi pale ambapo hoja zinazotolewa ni za kulaumu tu. Ningefurahi kama wangekuja na maelezo makini juu ya mapendekezo ya utatuaji wa mgogoro huo. Bado mnayonafasi ya kutoa hoja zenu, ni vipi mlihitaji mgogoro huo utatuliwe ili wananchi wa pande zote mbili zinazohusika huko Zanzibar wakarithika nazo. Msipoweza kutoa hoja basi malalamiko yenu hayana msingi kabisa.
Lazima ikumbukwe kuwa polisi waliokuwa wanatumwa Zanzibar, ni makomandoo wa jeshi waliokuwa mafunzoni wakvishwa mavazi ya polisi. Watu hawa hawakujifunza kutuliza ghasia, bali kuuwa na hivyo ndivyo walivyofanya huko Zanzibar. Si hivyo tu bali vile vile wali wabaka watoto wa kike mbele ya wazazi wao. Kweli tuko tayari kuulunda muungano kwa dhamani hii? Hapana hii si Tanzania bali ni SOWETO. Hata mkinukuu maneno ya mwalimu ya mwaka 1964, bado si tiketi ya kuulinda muungano kwa dhamani hii.
Hapa alipofikia Kikwete anahitaji pongezi, kwa hali yeyote ile si rahisi kuutatua mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 40 kwa amani kama tulivyoshuhudia. Hii ni sawa kama Rais Obama akafanikiwa kuutatua mgogoro wa Israel- Palestina. Ni nini anachoweza kupewa zaidi ya zawadi ya Nobel. Tumsifu JK kwa hapa alipotufikisha, na tuelewe kuwa ukuzaji wa uchumi unategemea sana amani ya nchi. Hongera Kikwete!!