Kikwete kilimo kwanza, Lowassa elimu kwanza!

Kikwete kilimo kwanza, Lowassa elimu kwanza!

kazi kweli nchi hii naiona ni nchi malaya kila linalokuja pokea sijui itakuwaje kuwa na viongozi wanaopigana mwisho wake si jui ni nini
 
Right on Lowassa. Elimu ya kweli kwa kila mtanzania ni sawa formula ya "Dettol detergent" iliyoongezwa nguvu mara tatu zaidi. Hii itafanya "sanitation" ya vijidudu vyote ndani ya TAKUKURU, OFISI YA MWANASHERIA MKUU,DPP,IGP,Wizara zote, nk kufa na hiyo kinachobaki ni kwenda mbele tu.

Huyu jamaa anafaa kuwa manager mkuu wa nchi hii.Atabadilisha Tanzania sana tofauti na jinsi wengi wanvyofikiria. Hata kama kweli ni mwizi au anafisadika kama udaku ulio mwingi unavyosema nadhani style yake ni kama ya wa ya wazungu. Mzungu ukimpa kazi ya kuzalisha tani mia za sukari atazalisha mia na hamsini halafu anaweza kucheza na tani thelathini(yaani akazifanyia magumashi). Halafu ukija anakwambia kazalisha tani 120,yaani kazidi lengo kwa tani 20 halfu utampa bonus na kumsifu. Ila mpe mswahili kazi ya kuzalisha tani mia.We! Hata tani moja hutaiona.Kisa? Sababu atakupa nyingi sana. Dawa tulionunua hukuwa nzuri,hivyo wadudu waliharibu miwa zaidi ya robo tatu,na ile kidogo tuliyovuna tumeuza na fedha tunaendeshea kiwanda kwa sasa. Lakini bujeti ya kuendeshea kiwanda si ilikuwapo? Mwishowe utamfukuza kazi. Lakini kumbe alizalisha tani mia akaiba zote,fedha kenda kujenga Hotel Johanesburg na kununua apartment London na NewYork. Wazungu ni wezi na wanafisdika kama waswahili ila tofauti ni kuwa wao wanafanya kile kinachowawezesha kuiba kuzalisha kwa wingi. Wizi wao ni endelevu, wa hapa kwetu tunaiba hadi mbegu!

Hiyo ndio tafsiri yangu kwa Lowassa anayesemwa kuwa ni fisadi
 
Ndugu wana JF suala la elimu ni muhimu mno. Elimu ni msingi wa kuweza kuelewa mengi. Kilimo ni taaluma ya kisayansi na kijamii. Kisayansi wakulima wanahitaji elimu ili waweze kuendana na sayansi ya kilimo inavyosonga mbele kama taaluma nyingine zilivyo. Wakulima wetu na wafugaji kwa kiasi kikubwa uzalishaji wao bado uko katika mwendelezo wa kilimo/ufugaji wa mazoea au kimfumo jamii kutegemea mahali walipo.

Elimu ingekuwa imepewa umuhimu wakulima wetu wasingekuwa hapo walipo katika hali ya umaskini wa kutupwa. Tanzania ni lazima iwekeze kwa kiasi kikubwa katika elimu ili kuwakwamua wananchi waishio vijijini na umasikini uliokithiri. Elimu itawafanya wafunguke zaidi na hata kushiriki katika kilimo kwa ufanisi zaidi kwa kuwa na uelewa wa kisayansi na kutumia misingi yake katika kuzalisha zaidi kwa mwelekeo endelevu.

Kuwekeza katika elimu tutakuwa na wakulima/wafugaji waelewa. Dhana ya KILIMO KWANZA itafanikiwa zaidi. Elimu na rasilimali kilimo zilizoko Tanzania, zikitumika vema tutakuwa wazalishaji wakubwa wa chakula na kuwa kapu la chakula/food basket katika ukanda wa Afrika Mashariki na kwingineko. Huko tuendako chakula kitakuwa silaha kubwa. Elimu ni muhimu haijalishi ni CDM au CCM wanaiisisitiza.
 
mbowe alianza na elimu kwanza juzi jamani. huyu jamaa, embu angalieni hii clip ya youtube. ilikua ndo Agenda na priority ya nchi hii.. siku izi naona priority ni kusafiri kwenda nnje wakati walimu wanagoma.. :loco:
Edward Lowassa - YouTube
 
  • Thanks
Reactions: kix
ameshakuwa gwanda huyo,ulimsikia mbowe juzi serena hotel?kipaumbele cha kwanza elimu,cha pili elimu,cha tatu elimu!kaaaaaaaazi kwelikweli!

yeah, if you can't fight them, join them. Kwa siku za karibuni hajatucritisaiz.
 
Kuna kitu nyuma ya lowasa na plan zake. Kama sio CDM basi ADC. Ngoja tusubiri. Waiterrrrrrrr. Barrrrid hapa mara moja.
 
Katika kile kinachoonekana kama ni kudharau au kupuuza kauli mbiu ya waziri mkuu PINDA, WM mstaafu Edward Lowassa akizungumza na jamii ya wafugaji Ifakara mkoani Morogoro, alisema waachane na kauli mbiu ya kilimo kwanza na wawekeze kwny ELIMU. TBC.

Ifakara amekwenda kwa tiketi ya nani kama si kuvuruga mikutano ya M4C. Hv bado huyu baba ana ndoto na ule ugonjwa wa kutaka kuwa rais wa nchi hii?
 
sasa hawa wanasiasa walikuwa wapi mpaka wakaja na kilimo kwanza?wakati wakijua kilimo pia kinahitaji elimu,au mlilewa madaraka?thats y huwa najiuliza huwa tunaongozwa na tunashindwa kujiongoza
 
Jana nimesikia kwenye Taarifa ya habari Rwanda wameagiza matrekta ambayo watatoa kwa mikopo kwa wakulima nikaangalia na nchi yetu imetangaza kilimo kwanza lakini matrekta yamejazana mwenge yanasubiri wanunuzi wakati tunajua kabisa uwezo wa wakulima wetu ukoje.Kama kweli tungekuwa tunataka kuinua kilimo tungemjengea mkulima uwezo(kumwezesha) kwa kumkopesha zana kama matrekta na pia kumuhakikishia soko la uhakika la mazao yake
Kwa kifupi kilimo kwanza kimejaa porojo ndio maana kila siku tunasikia Rais anaita wawekezaji nje badala ya kuwezesha wananchi wake
 
Point ya LOWASA ni nzuri lakini ni MWIZI ndo maana ana uwezo wa kutoa milioni 100 kanisani wakati yeye ni mhudumu wa Serikali
 
Katika bajeti ya Tanzania, tunaambiwa Elimu inaongoza kwa kupewa fedha zaidi ktk bajeti, hapa napata wazo la Elimu Kwanza (ili hali ubora bado duni), lakini upande wa pili, viongozi wetu wa juu serikalini wanatuhubiri Kilimo kwanza, hapa tena napata wazo la Kilimo kwanza (ili hali bado kilimo kinategemea mvua)
Mkanganyiko huu wa nini hasa ni priority number one, unatuchanganya na tunashindwa kujua nini hasa ni "Kwanza" hapa Tanzania, na wapi hasa wananchi waelekeze nguvu na rasilimali zao! Hii inapelekea kushindwa kuonesha ufanisi. Ni vizuri PRIORITY NUMBER ONE, ikaelezwa na vitendo endelevu vikafanywa!
Bajeti inaonesha Elimu ni ya Kwanza. Viongozi wanahubiri Kilimo Kwanza, Mtanzania anakoseshwa msimamo!

Nenetwa, kumbuka Wabongo tu nambari wani duniani kwa kutunga kaulimbiu: 'kilimo kwanza', "elimu kwanza', sijui nini "kwanza" ni kaulimbiu tu za kisiasa (political slogans) na sio sera (policy). Kwa hivyo ni nyimbo tu kama zile za bongofleva: zinasaidia kutuliwaza tukiwa katika dimbwi la shida na msongo wa mawazo!!!
 
lowasa ile miaka miwili mziki wake tuliuona,sasa ajisafishe kwa lipi?wenye macho waliona na wenye maskio. wali
 
Kipao mbele cha taifa kinatakiwa kuwa afya kwanza then elimu na sio kilimo kwanza, kwani bila afya uwez kulima, kusoma, kuomba miongozo bungeni n.k ~ Prof Mark Mwandosya

V
SENGEREMA
Hakuna Afya Bila Chakula!Na Chakula kinatoka Shamba!
 
Waziri mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya RICHMOND, ametamka kwamba hakubaliani na sera ya kilimo kwanza. Anasema sera hii angeikubali kama ingekuwa kilimo kwanza - elimu kabla!... Je, alipokuwa waziri mkuu alikuwa anaisimamiaje sera asiyoikubali? .....Nini Tofauti ya kauli hizi? - KILIMO KWANZA - ELIMU KABLA!...........SOURCE: Dkk 45 ITV
 
Hii ni kauli ambayo mh. Lowasa amekuwa akiitoa mara kwa mara. Maana halisi ni elimu kwanza na kilimo ndipo kinafuata. Nadhani ameamua kutoa kauli hii ili asionekane kuipinga sera ya moja kwa moja ya serikali iliyopo madarakani. Nimeipenda hiyo.

Pia amenifurahisha kusema kuwa kauli nyingi za viongozi wa kubwa wa nchi hazionekani katika matendo.

Huyu jamaa ana tuhuma nyingi za kifisadi lakini tukumbuke "Baniani mbaya, kiatu chake dawa", "mnyonge mnyongeni lakini haki yake tuumpe" kwa namna flan ndugu Lowasa ni jembe katika maswala ya kiuongozi na maamuzi kwa ujumla. "hapepesi macho katika kauli zake".

Huu ni mtazamo wangu tu wadau!
 
[h=3]Former Prime Minister, Edward Ngoyai Lowassa who is also Monduli Province MP has said his party knows that he doesn’t agree with the Agriculture First (Kilimo Kwanza) policy.[/h]
Edward-Lowassa1.jpg


Former Prime Minister and Monduli Province legislator, Edward Lowassa who has advised the government to invest in education sector before focusing in agriculture.

Lowassa said that as he was speaking in ‘Dakika 45’ program interview aired by ITV on Monday night at 21:00 hrs.
He criticized the policy saying that it is not possible to achieve in agriculture if Tanzanian farmers and other citizens have lower level of education.
“I don’t I agree with the idea that you can implement successfully agriculture while your farmers have low level of education or are illiterate. They must go to school in order to use modern ways of cultivating.”
Lowassa said always he believes in education hence suggesting it could be Education First; “Or we can call Education before, Agriculture First” meaning that education should start before focusing in agricultural sector.
He cited many countries such as Middle East around the world insisting that they all invested in education before looking into other sectors. So they came up with experts who were used in projects established.
 
Hivi hatuna priorities kama nchi maana kama kila mtu anakuja na ya kwake, wale watu wa mipango wapo pale wanafanya nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom