Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,045
Hii sinema inaelekea episode za mwisho mwisho. Na utabiri wangu ni kuwa pamoja na harufu za damu za wenye kuhisi kumiliki chama; pia CDM itakumbwa na mtikisiko mwingine mkubwa kupiti viongozi wake wa juu. Zitto na Mbowe watakuwa upande mmoja kupokea misaada ya EL na genge lake huku wakimficha Dr. Slaa. Dr. Slaa ataishia kupewa mabomu akalipue huku "wakuu" wakinufaika na kutoa makazi na uwanja wa kurushia makombora kuelekea ccm. Haya ni maono yangu tu!
Hii hapa chini Raia Mwema wamehemea hapo juu
CHADEMA yakana kubeba mafisadi
"Taarifa zinasema katika moja ya sura za mkakati huo, Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk. Wilbroad Slaa, anatajwa kutumiwa bila kujua na baadhi ya viongozi wenzake ndani ya CHADEMA, walio karibu na Lowassa, kutekeleza malengo ya watuhumiwa hao wa CCM."