Elitwege
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 5,154
- 10,809
Habari wadau.
Kuna video inasambaa mitandaoni ikimuonyesha Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Kikwete akimuelezea aliyekuwa Rais wa tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli kuwa tangu akiwa waziri alikuwa adui mkubwa wa wanafiki, wazembe na wababaishaji kazini. Kikwete amesema watu hao hawakumpenda akiwa waziri na hata alipokuwa Rais na ikizingatiwa kuwa nchi yetu inakabiliwa na wimbi kubwa la watu kuwa wazalendo mdomoni lakini kwa vitendo wanafanya mambo tofauti kabisa.(MIGA)
Kikwete kwenye hiyo video amefafanua kuwa wakati akiwa Rais jembe lake alikuwa waziri Dkt. Magufuli na alimpa kazi ya kuunganisha mikoa yote kwa barabara za lami na kweli mpaka anaondoka madarakani mwaka 2015 walikuwa wamefanikiwa kuunganisha mikoa yote isipokuwa katavi tu.
Kikwete amesema bila ubunifu na kujituma kwa Dkt. Magufuli isingewezekana.
Kuna video inasambaa mitandaoni ikimuonyesha Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Kikwete akimuelezea aliyekuwa Rais wa tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli kuwa tangu akiwa waziri alikuwa adui mkubwa wa wanafiki, wazembe na wababaishaji kazini. Kikwete amesema watu hao hawakumpenda akiwa waziri na hata alipokuwa Rais na ikizingatiwa kuwa nchi yetu inakabiliwa na wimbi kubwa la watu kuwa wazalendo mdomoni lakini kwa vitendo wanafanya mambo tofauti kabisa.(MIGA)
Kikwete kwenye hiyo video amefafanua kuwa wakati akiwa Rais jembe lake alikuwa waziri Dkt. Magufuli na alimpa kazi ya kuunganisha mikoa yote kwa barabara za lami na kweli mpaka anaondoka madarakani mwaka 2015 walikuwa wamefanikiwa kuunganisha mikoa yote isipokuwa katavi tu.
Kikwete amesema bila ubunifu na kujituma kwa Dkt. Magufuli isingewezekana.