Kikwete: Hayati Dkt. Magufuli alikuwa adui mkubwa wa wanafiki na wababaishaji

Habari wadau.

Kuna video inasambaa mitandaoni ikimuonyesha Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Kikwete akimuelezea aliyekuwa Rais wa tano wa Tanzania hayati Dkt. Magufuli kuwa tangu akiwa waziri alikuwa adui mkubwa wa wanafiki, wazembe na wababaishaji kazini. Kikwete amesema watu hao hawakumpenda akiwa waziri na hata alipokuwa Rais na ikizingatiwa kuwa nchi yetu inakabiliwa na wimbi kubwa la watu kuwa wazalendo mdomoni lakini kwa vitendo wanafanya mambo tofauti kabisa.(MIGA)

Kikwete kwenye hiyo video amefafanua kuwa wakati akiwa Rais jembe lake alikuwa waziri Dkt. Magufuli na alimpa kazi ya kuunganisha mikoa yote kwa barabara za lami na kweli mpaka anaondoka madarakani mwaka 2015 walikuwa wamefanikiwa kuunganisha mikoa yote isipokuwa katavi tu.

Kikwete amesema bila ubunifu na kujituma kwa Dkt. Magufuli isingewezekana.
Amesema kweli kabisa
 
hayati magufuli alikuwa mtu mzuri sana sema tu ni ule ujinga wake wa kuua nzi kwa bunduki ndio unamdmfanya aonekane jitu moja katili kwelikweli ambalo sehemu pekee linakoweza kukaa ni kaburini
 
hayati magufuli alikuwa mtu mzuri sana sema tu ni ule ujinga wake wa kuua nzi kwa bunduki ndio unamdmfanya aonekane jitu moja katili kwelikweli ambalo sehemu pekee linakoweza kukaa ni kaburini
Kwani wewe mbw hutakaa kaburini!?
 
Yaan usije ukafanya kosa kubwa kumuanin kikwete huyu ni master wa vita ya kisaikolojia anakulaghai huku mwenyewe ukishangilia kwa kupiga makofi kwa mikono na sio miguu kama zuzu .ninamifano miwili ya kwanza ishu ya katiba mpya aluliwaita ikulu wapinzan akawapa chai na mandaz na juis juu na kusikiliza hoja zao kisha kukubaliana nazo na kuunda tume ya katiba mpya haraka sana na akaaaid kabla hajaondoka katiba mpya itapatikana tume ikapewa hela ikaanza kaz wapinzan wakaona mtu ndio huyu mwaka mmoja kabla ya kuondoka madarakan akawajibu kua suala hilo aliwez limenshinda wasahau ,

Pili kipind cha uchaguz wa mgombea urais wa ccm lowasa alikua na nguvu na kuungwa mkono na wajumbe wote ilikua bila lowasa kupita mkutano uvunjike na yeye aliliona hilo bas bwana yule wakat anaingia ukumbin akakutana na hamasa na shauku ya wana ccm wakisisitiza tunamtakalowasa tu huku wakiimba mbele ya mwenyekit na mwenyekiti akaanza kuimba nao wakaona mpaka. Mwenyekit anaimba nas suala limeisha hilooo kilichokuja kutokea kila mjumbe alipigwa na butwaaaa lowasa alichinjwa gafla bin vuuu
Kikwete kawiva kisiasa haswa.
Anakuchinja huku anacheka.
Lakini utawala wa Magufuli hata kwake ulikuwa mtihani mgumu.
Ni dhahiri Magufuli hakuwa chaguo la Kikwete 2015, alikuwa chaguo la Mkapa, na Mgufuli alikuwa anamsikiliza Che Nkapa tu kwa ushauri wa mwisho.

Tunasikia mambo yaliyokuwa yanaendelea chini chini kati ya Membe, Kikwete na Mkapa yalikuwa mengi, lakini mshituko ulioingia kwa kifo kisichotegemewa cha Mkapa, kilikuwa kikubwa.

Hapo baada ya Mkapa kufariki Magufuli akapata mkono wa chuma, na kwa vile hashauriki akaanza kufanya mambo kivyake vyake.
Tume ya uchaguzi ikapata maagizo nani aingie bungeni na nani atoke.
CCM nayo ikawa inaendeshwa harijojo, mawazo ya Mwenyekiti, final.

Wakaenguliwa vigogo walioonekana kumkwaza Mwenyekiti.
The bigger picture ikaonekana wazi, Magufuli lazima arudi madarakani 2nd term.
Na kwa majority ya wabunge waliochaguliwa na Magufuli na Bashiru, 75% majority bungeni ingeweza kubadili katiba, Rais aongezewe 3rd term au awe Rais wa milele.

Mahakama nazo zikawa in tow.
Viongozi wotewalikuwa hand picked, na waliahidiwa funding kubwa na marupurupu mengi kama watatii amri.

Huku nyuma, Kikwete na mtandao wake hawakuwa wamelala, nwakawa mambo yao kimya kimya.
Magufuli alilijua hilo, na woga ukawa umemwingia.
Kila baada ya wiki tatu au nne akawa anarudi kwao, Chato, ambako ni rahisi kujua anayemfuatilia vile vile.

Mambo yakawa magumu zaidi, sasa na jeshi ilibidi kuingia ulinzi wa Rais kwa helikopta kila aendako.

Je ilikuwa ni paranoia?
Yaliyoendelea baada ya hapo kila mtu ana hadithi yake.
Never write off JK.
 
Back
Top Bottom