Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 988
***************************************
SOURCE: TANZANIA DAIMA
DATE: DECEMBER 08, 2011 (Today)
PAGE: FRONT PAGE
SUBHEADINGS: Wahofia kuvunjika amani, Washangazwa na Uamuzi wa Bunge, Wasema Nyerere amesahaulika
***************************************
Kanisa Katoliki nchini (TEC) limeshtushwa na hatua ya Rais Jakaya Kikwete kusaini Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011, harakharaka kwa kuwa kunaweza kuipeleka nchi pabaya.
Akizungumza jijini juzi na TANZANIA DAIMA muda mfupi baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa kitabu cha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara, kilichoandikwa na John Kasembo, Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Askofu Mkuuu Jude Thadaeus RuwaIchi alisema Watanzania wengi walitaka muswada huo usisaniwe, na kwamba mkuu huyo wa nchi alipaswa kusikiliza mawazo ya wananchi wake, na si kuwahi kusaini na kuwa sheria, Rais huyo wa TEC alisema kitendo cha Serikali kukusanya maoni mikoa ya Dodoma, Dar-Es-Salaam na Zanzibar peke yake, haitoshi kujenga hoja ya kusaini ama kupitisha muswada huo wa Katiba.
Askofu RuwaIchi alisema suala la kuundwa kwa Katiba mpya si hiari ya Rais wala kikundi na tabaka Fulani bali ni la watanzania wote.
Rais huyo wa TEC ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza alisema hatua ya kulipeleka suala la Katiba mbindembinde linaweza kuipeleka nchi kubaya na Kanisa Katoliki halitaki Watanzania wafike huko.
Alisema walitegemea Kikwete angethamini na kujali maoni ya wadau wengine, lakini katika namna ya ajabu hakuonekana kujali chochote. RuwaIchi ambaye alikuwa miongoni mwa wageni waalikwa katika uzinduzi wa kitabu hicho, alieleza kushangazwa na kitendo cha Bunge kupitisha harakaharaka muswada huo.
Hivi Bunge linashughulika na maslahi ya nani? Wabunge wamepewa dhamana na wananchi, hivyo ni lazima wawasikilize wanachotaka, halafu ndicho wakifanyie kazi, na si kuonekana kama ushabiki fulani, alisema Askofu Mkuu RuwaIchi.
Alipoulizwa kuhusu suala la udini linaloonekana kutumiwa na baadhi ya wanasiasa nchini, Askofu RuwaIchi alikiri kuwapo kwa jinamizi hilo, na kusema ajenda ya udini kwa sasa imekuwa kama kichaka cha watu Fulani kuficha maovu yao.
Alionya kwamba iwapo serikali itaruhusu mijadala ya dini kutawala nchini, basi taifa lipo hatarinikupoteza ustawi wake, na akataka watu wasitumie mgongo wa dini kuficha madhambi yao.
Katika hatua nyingine, TEC imesema mambo yote mema yaliyotendwa na Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere yametupiliwa mbali, na sasa kila mtu anatenda lolote linaloonekana kuwa na manufaa kwake.
SOURCE: TANZANIA DAIMA
DATE: DECEMBER 08, 2011 (Today)
PAGE: FRONT PAGE
SUBHEADINGS: Wahofia kuvunjika amani, Washangazwa na Uamuzi wa Bunge, Wasema Nyerere amesahaulika
***************************************
Kanisa Katoliki nchini (TEC) limeshtushwa na hatua ya Rais Jakaya Kikwete kusaini Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011, harakharaka kwa kuwa kunaweza kuipeleka nchi pabaya.
Akizungumza jijini juzi na TANZANIA DAIMA muda mfupi baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa kitabu cha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara, kilichoandikwa na John Kasembo, Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Askofu Mkuuu Jude Thadaeus RuwaIchi alisema Watanzania wengi walitaka muswada huo usisaniwe, na kwamba mkuu huyo wa nchi alipaswa kusikiliza mawazo ya wananchi wake, na si kuwahi kusaini na kuwa sheria, Rais huyo wa TEC alisema kitendo cha Serikali kukusanya maoni mikoa ya Dodoma, Dar-Es-Salaam na Zanzibar peke yake, haitoshi kujenga hoja ya kusaini ama kupitisha muswada huo wa Katiba.
Askofu RuwaIchi alisema suala la kuundwa kwa Katiba mpya si hiari ya Rais wala kikundi na tabaka Fulani bali ni la watanzania wote.
Rais huyo wa TEC ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza alisema hatua ya kulipeleka suala la Katiba mbindembinde linaweza kuipeleka nchi kubaya na Kanisa Katoliki halitaki Watanzania wafike huko.
Alisema walitegemea Kikwete angethamini na kujali maoni ya wadau wengine, lakini katika namna ya ajabu hakuonekana kujali chochote. RuwaIchi ambaye alikuwa miongoni mwa wageni waalikwa katika uzinduzi wa kitabu hicho, alieleza kushangazwa na kitendo cha Bunge kupitisha harakaharaka muswada huo.
Hivi Bunge linashughulika na maslahi ya nani? Wabunge wamepewa dhamana na wananchi, hivyo ni lazima wawasikilize wanachotaka, halafu ndicho wakifanyie kazi, na si kuonekana kama ushabiki fulani, alisema Askofu Mkuu RuwaIchi.
Alipoulizwa kuhusu suala la udini linaloonekana kutumiwa na baadhi ya wanasiasa nchini, Askofu RuwaIchi alikiri kuwapo kwa jinamizi hilo, na kusema ajenda ya udini kwa sasa imekuwa kama kichaka cha watu Fulani kuficha maovu yao.
Alionya kwamba iwapo serikali itaruhusu mijadala ya dini kutawala nchini, basi taifa lipo hatarinikupoteza ustawi wake, na akataka watu wasitumie mgongo wa dini kuficha madhambi yao.
Katika hatua nyingine, TEC imesema mambo yote mema yaliyotendwa na Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere yametupiliwa mbali, na sasa kila mtu anatenda lolote linaloonekana kuwa na manufaa kwake.