Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
TAARIFA YA
MHESHIMIWA DKT.
JAKAYA MRISHO
KIKWETE, RAIS WA
JAMHURI YA
MUUNGANO WA
TANZANIA,
KUFUATIA AJALI YA
KUZAMA KWA MELI
YA MV SKAGIT
ILIYOTOKEA TAREHE
18 JULAI, 2012,
CHUMBE, ZANZIBAR
Jana tarehe 18 Julai,
2012, majira ya alasiri
kumetokea ajali ya
kuzama kwa meli ya
MV SKAGIT katika
eneo la Chumbe,
Zanzibar. Meli hiyo
iliyokuwa ikitokea Dar
es Salaam kueleka
Zanzibar ilikuwa
imebeba watu 290.
Kati yao watu
wazima 250, watoto
31 na wafanyakazi
wa meli 9.
Amiri Jeshi Mkuu,
Mheshimiwa Jakaya
Mrisho Kikwete
aliagiza vyombo vya
ulinzi na usalama vya
Serikali ya Muungano
yaani JWTZ na Polisi
waanze kazi ya
uokoaji mara moja.
Kazi hiyo imefanywa
kwa kushirikiana na
vyombo vya usalama
vya Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar
na meli za
makampuni binafsi.
Mpaka giza lilipokuwa
limeingia na hivyo
kazi ya uokoaji
kusitishwa mpaka
kutakapokucha
tarehe 19 Julai, 2012,
watu 136 walikuwa
wameokolewa na
maiti 31 zilikuwa
zimepatikana. Aidha,
mali zilizokuwa
kwenye meli hiyo
hazikuweza
kuokolewa.
Kufuatia ajali hiyo,
Rais wa Jamhuri ya
Muungano
alizungumza na Dkt.
Ali Mohamed Shein,
Rais wa Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar
na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi.
Alimpa pole kwa ajali
iliyotokea hasa kwa
vifo na majeraha
waliyopata
Watanzania wenzetu
na watu wasiokuwa
raia wa Tanzania.
Alimuomba afikishe
salamu za
rambirambi kwa
ndugu zetu
waliopotelewa na
jamaa zao na
kuwapa pole
waliopata majeraha
na maumivu
maungoni mwao.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano alisema
kuwa huu ni msiba
wetu sote na
kwamba majonzi yao
ni majonzi yake na ya
Watanzania wote.
Kwa ndugu zetu
waliojeruhiwa
tunawaombea kwa
Mwenyezi Mungu
awape ahueni na
wapone haraka ili
waweze kuendelea
na shughuli zao za
kujiletea maendeleo
na kulijenga taifa
letu.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa
Tanzania
amempongeza Rais
wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi,
Dkt. Ali Mohamed
Shein na viongozi
wote wa ngazi
mbalimbali kwa
uongozi wao thabiti
tangu taarifa ya
kutokea kwa ajali
mpaka sasa.
Aidha,
amewapongeza
maafisa na askari wa
vyombo vya ulinzi na
usalama na
wafanyakazi wa meli
binafsi, kwa juhudi
kubwa walizozifanya
za uokoaji wa ndugu
zetu waliopatwa na
maafa haya
makubwa na ya aina
yake. Amewataka
waendeleze juhudi
hizo leo na siku
zijazo.
Rais amewataka
wananchi wawe na
moyo wa subira na
uvumilivu wakati kazi
ya uokoaji inaendelea.
Kama ilivyofanyika
katika ajali ya MV
Spice Islander miezi
10 iliyopita, uchunguzi
wa kina utafanyika
kubaini chanzo cha
ajali.
Kutokana na ajali hiyo
na msiba huu
mkubwa, Rais wa
Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania,
Mheshimiwa Rais
Jakaya Mrisho
Kikwete,
ametangaza
maombolezo ya taifa
ya siku tatu ambapo
bendera zitapepea
nusu mlingoti kuanzia
leo, tarehe 19 Julai,
2012.
Asanteni sana.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
19 Julai, 2012
MHESHIMIWA DKT.
JAKAYA MRISHO
KIKWETE, RAIS WA
JAMHURI YA
MUUNGANO WA
TANZANIA,
KUFUATIA AJALI YA
KUZAMA KWA MELI
YA MV SKAGIT
ILIYOTOKEA TAREHE
18 JULAI, 2012,
CHUMBE, ZANZIBAR
Jana tarehe 18 Julai,
2012, majira ya alasiri
kumetokea ajali ya
kuzama kwa meli ya
MV SKAGIT katika
eneo la Chumbe,
Zanzibar. Meli hiyo
iliyokuwa ikitokea Dar
es Salaam kueleka
Zanzibar ilikuwa
imebeba watu 290.
Kati yao watu
wazima 250, watoto
31 na wafanyakazi
wa meli 9.
Amiri Jeshi Mkuu,
Mheshimiwa Jakaya
Mrisho Kikwete
aliagiza vyombo vya
ulinzi na usalama vya
Serikali ya Muungano
yaani JWTZ na Polisi
waanze kazi ya
uokoaji mara moja.
Kazi hiyo imefanywa
kwa kushirikiana na
vyombo vya usalama
vya Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar
na meli za
makampuni binafsi.
Mpaka giza lilipokuwa
limeingia na hivyo
kazi ya uokoaji
kusitishwa mpaka
kutakapokucha
tarehe 19 Julai, 2012,
watu 136 walikuwa
wameokolewa na
maiti 31 zilikuwa
zimepatikana. Aidha,
mali zilizokuwa
kwenye meli hiyo
hazikuweza
kuokolewa.
Kufuatia ajali hiyo,
Rais wa Jamhuri ya
Muungano
alizungumza na Dkt.
Ali Mohamed Shein,
Rais wa Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar
na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi.
Alimpa pole kwa ajali
iliyotokea hasa kwa
vifo na majeraha
waliyopata
Watanzania wenzetu
na watu wasiokuwa
raia wa Tanzania.
Alimuomba afikishe
salamu za
rambirambi kwa
ndugu zetu
waliopotelewa na
jamaa zao na
kuwapa pole
waliopata majeraha
na maumivu
maungoni mwao.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano alisema
kuwa huu ni msiba
wetu sote na
kwamba majonzi yao
ni majonzi yake na ya
Watanzania wote.
Kwa ndugu zetu
waliojeruhiwa
tunawaombea kwa
Mwenyezi Mungu
awape ahueni na
wapone haraka ili
waweze kuendelea
na shughuli zao za
kujiletea maendeleo
na kulijenga taifa
letu.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa
Tanzania
amempongeza Rais
wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi,
Dkt. Ali Mohamed
Shein na viongozi
wote wa ngazi
mbalimbali kwa
uongozi wao thabiti
tangu taarifa ya
kutokea kwa ajali
mpaka sasa.
Aidha,
amewapongeza
maafisa na askari wa
vyombo vya ulinzi na
usalama na
wafanyakazi wa meli
binafsi, kwa juhudi
kubwa walizozifanya
za uokoaji wa ndugu
zetu waliopatwa na
maafa haya
makubwa na ya aina
yake. Amewataka
waendeleze juhudi
hizo leo na siku
zijazo.
Rais amewataka
wananchi wawe na
moyo wa subira na
uvumilivu wakati kazi
ya uokoaji inaendelea.
Kama ilivyofanyika
katika ajali ya MV
Spice Islander miezi
10 iliyopita, uchunguzi
wa kina utafanyika
kubaini chanzo cha
ajali.
Kutokana na ajali hiyo
na msiba huu
mkubwa, Rais wa
Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania,
Mheshimiwa Rais
Jakaya Mrisho
Kikwete,
ametangaza
maombolezo ya taifa
ya siku tatu ambapo
bendera zitapepea
nusu mlingoti kuanzia
leo, tarehe 19 Julai,
2012.
Asanteni sana.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
19 Julai, 2012