Kikwete apokelewa na wanachama CUF badala ya CCM airport Tanga

Mkuu mzeelapa usiende mbali chunguza kinacho endelea Kenya wenzetu kwenye EAC, JUZI WAMEFUKUZA KAZI mAJAJI WA MAHAKAMA YA RUFAA WANNE, Sio kuwastafisha ni kuwafukuza kazi!!!! Bado huoni faida ya kuwa na mabadilko tuu, umelidhika na wizi unaoendelea chini hapa tuu?????

 

KOMBAJR kuna watu hapa wanataka kupotosha wana Great Thinkers kua hizi picha ni PHOTOSHOP! Nasema washindwe na walegee! hii ilikua live hata kwenye TV yao ya TBC1. Na sasa ukitaka kujua CCM ni watu wa ajabu angalieni taarifa ya habari kwenye station yao ya TBC1 leo saa 2 usiku hawatazionyesha hizi picha japokua ndoa yao na CUF inamgogoro.
 

Tumia akili angalau za kuzaliwa! Vyama vya upinzani havikusanyi kodi hivyo havina uwezo wa kuwaendeleza wananchi kiuchumi!

Kazi wanayoweza wapinzani hivi sasa ni kuwahamasisha wananchi kisiasa ili wananchi wajitambue; wajue wajibu wao wa kujikomboa kutoka kwa mabeberu mamboleo wanaohujumu rasilimali za taifa kwa faida yao binafsi!
 
Inawezekana fuso ziligoma kubeba wana magamba kutoka mashambani, au walipata tetesi kuwa hakutakuwepo ubwabwa katika mapokezi hayo.
 
Jakaya ni mwanachama wa CUF. Bagamoyo, Tanga, Zanzibar, Pemba, Mtwara na Lindi ni ngome za CUF. Jakaya ni mwanachama hai wa CUF. Angalia jinsi anavyoiua CCM. Na pia haikuwa shida kwake kuwashawishi CUF kujiunga na CCM kwa lengo la kupata serikali ya mseto. Akimaliza kipindi chake cha uraisi atatangaza rasmi kujiunga CUF.
 
Mzee Mtumishi wetu katika wazo lako #101. Nakubaliana na wewe na nimekuwa nikifuatilia habari za Kenya. Pamoja na tukio ulilotaja pia ajira zao na hata mchakato wa kumpata mwanasheria wao mkuu ulifanyika kwa uwazi tena live. Hiyo tuseme ni hatua mojawapo, lakini kwa muda hao wapinzani waliokuwepo madarakani kwa miaka karibu kumi ni mafanikio yaliyopatikana yanalingana na ahadi zao? Mabadiliko ya katiba nakubali, nadhani hilo ndio la msingi, maendeleo je? Labda wenzetu mlioko Kenya mtujuze..
 
Mkuu Ileje kwenye #103. (bahati mbaya mtandao hauniwezeshi kupata quotation niki-click Reply with Quote haiuninganishi). Kwanza punguza jazba...hapa hatugombani. Maendeleo hayaletwi na fedha peke yake, nilichokuwa nashauri maeneo yale ambayo vyama vya upinzani wameyashika waendelee kuhamasisha na kuwaelekeza wananchi wajiletee maendeleo ili tuone tofauti, sio kwa kutegemea kodi peke yake, isitoshe hata iweje uchumi na makusanyo ya kodi hayawezi kutufikisha tunakotaka kwa harakaharaka kama upinzani unavyotaka tuamini. Para yako ya pili uko sahihi lakini hujajibu hayo uliyoyawekea rangi nyekundu. Tuliowachagua tunataka watusaidie kuleta maendeleo tutawapimaje mwaka 2015? Kwa kuvunja rekodi ya kufanya maandamano? Wabunge wanaacha majimbo yao wanakwenda kufanya maandamano, kwani hayo maandamano Slaa peke yake hatoshi mpaka msururu wa wabunge wote wa CDM wawepo? Fikiria mbunge atoke Mbeya kwenda kuandamana Arusha...!hapo pia kuna matumizi mabaya ya rasilimali kidogo zinazopatikana ktk chama..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…