Riwa
Platinum Member
- Oct 11, 2007
- 2,607
- 3,068
Dk. Bana ambaye ni Mwenyekiti Mwenza wa Taasisi ya Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (Redet), alisema kuwa jambo analoweza kulifanya Rais kwa sasa katika kupambana na vita hiyo ni kutoa motisha kwa wale watakaowafichua watuhumiwa.
Alibainisha kuwa serikali inaweza kujipanga ikatoa motisha ya kati ya sh milioni tatu hadi tano kwa kila atakayetoa taarifa za wauza dawa za kulevya na wala rushwa ambazo zitathibitika kuwa za kweli.
"Kwenye jamii hawa watu wanaoitwa whistleblower's (wapiga vilimbi) wapo, hivyo wakipewa motisha watawataja wauza dawa hizo na wala rushwa ilimradi tuhuma hizo zithibitike ni za kweli," alisema
Dr Bana siku hizi naona uwezo wake wa kufikiri critically na kuja na solution zenye tija umepungua sana...yaani siku hizi kila akiombwa comment on sensitive issues anaongea bla bla blaaah hata msela wa Manzese stand tu pale ana pointi bora zaidi!