Kalunguine
JF-Expert Member
- Jul 27, 2010
- 2,543
- 134
Habari kuwa Kikwete anakubaliana na wabunge katika mjadala wa kuwawajibisha mawaziri kwa wizi wa pesa za wizara na idara mbalimabli haziwezi kupita bila kuuliza maswali ya msingi. Kwanza inabidi tujiulize, Kikwete aliisoma taarifa ya CAG? Swali hili ni muhimu kwa kuwa tunafahamu kuwa Kikwete amewahi kupewa mfano wa hundi wenye tarakimu ambazo haziendani na maneno yeye akatwaa hundi hiyo yenye makosa. Kama hakusoma hundi yenye ukurasa mmoja iweje taarifa kubwa ya CAG?
Pia ni rahisi kuamini kuwa taarifa ya Richmond ilijadiliwa bungeni bila yeye kuisoma. Ndiyo maana baada ya kujadiliwa na kumwondoa Lowasa alisikitika mbele ya wazee wa Dar kuwa ilikuwa ni ajali ya kisiasa.
Alienda mbali kuwa Chadema wanatuhumu wao, wanapeleleza wao na kuhukumu wao. Kama angeisoma ile taarifa kabla angeweza kumwokoa rafiki yake Lowasa. Halafu tunakumbuka sheria ya uchaguzi aliyoisaini ikiwa na makosa na baadaye kurekebishwa baada ya kusainiwa.
Kama Kikwete hakuweza kusona makosa kwenye ukurasa mmoja wa hundi na pia pia sheria ya gharama ya uchaguzi na taarifa ya Richmond kwa nini tuamini kuwa alisoma lundo la taarifa za CAG? Ni rahisi kuamini kuwa Kilwete hakusoma taarifa ya CAG na kwa hiyo hakujua kilichomo. Kama angejua angweza kuwaokoa mawaziri wake.
Lakini ilimpasa tu kukubaliana na wabunge kwa kuwa wananchi wengi walikasirishwa na wizi mkubwa unaofanywa na mawaziri. Kwa kuwa ni rahisi kuamini kuwa Kikwete hakuisoma ile taarifa ya CAG inayohitaji mkaguzi mwingine wa kuisoma, habari kuwa alipendezwa na mjadala ya wabunge ni ya kutiliwa mashaka makubwa
Pia ni rahisi kuamini kuwa taarifa ya Richmond ilijadiliwa bungeni bila yeye kuisoma. Ndiyo maana baada ya kujadiliwa na kumwondoa Lowasa alisikitika mbele ya wazee wa Dar kuwa ilikuwa ni ajali ya kisiasa.
Alienda mbali kuwa Chadema wanatuhumu wao, wanapeleleza wao na kuhukumu wao. Kama angeisoma ile taarifa kabla angeweza kumwokoa rafiki yake Lowasa. Halafu tunakumbuka sheria ya uchaguzi aliyoisaini ikiwa na makosa na baadaye kurekebishwa baada ya kusainiwa.
Kama Kikwete hakuweza kusona makosa kwenye ukurasa mmoja wa hundi na pia pia sheria ya gharama ya uchaguzi na taarifa ya Richmond kwa nini tuamini kuwa alisoma lundo la taarifa za CAG? Ni rahisi kuamini kuwa Kilwete hakusoma taarifa ya CAG na kwa hiyo hakujua kilichomo. Kama angejua angweza kuwaokoa mawaziri wake.
Lakini ilimpasa tu kukubaliana na wabunge kwa kuwa wananchi wengi walikasirishwa na wizi mkubwa unaofanywa na mawaziri. Kwa kuwa ni rahisi kuamini kuwa Kikwete hakuisoma ile taarifa ya CAG inayohitaji mkaguzi mwingine wa kuisoma, habari kuwa alipendezwa na mjadala ya wabunge ni ya kutiliwa mashaka makubwa