Hivi Mh Rais wetu Kikwete anakua anapoteza kumbukumbu haraka au ni mimi ndio sio simuelewi vema Mh Rais??
Sí majuzi kati tu yeye mwenyewe amesema anaridhishwa na jinsi mchakato unavyoendelea na akatoa baraka kwa Bunge la katiba kuendelea na mchakato ??
Jamani labda mi nazeeka kushindwa kuelewa mambo vema, Hivi si huyu huyu alisema tujiandae kisaikolojia kuwa serikali tatu badae akaja akasema serikali tatu zitasababisha jeshi kuchukua nchi???
Mh Rais labda anazungumzia vitu tofauti tofauti ambavyo mimi navichanganya??? Jamani nisaidie ndugu yenu nimwelewe rais wangu JK (Sio JK Nyerere yeye namwelewa vema tu)