Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,172
Afya mgogoro. Unajuaje, labda kadondoka tena na amefichiwa siri?
Kama kuna impropriety zimefanyika, improprieties hizi haziwezi ku stick katika ubadhirifu wa madaraka au matumizi ya madaraka kwa rushwa kwa mujibu wa sheria mpya ya gharama za uchaguzi.
Tatizo nchi yenyewe changa na vitu havijawa defined katika njia iliyo watertight kutoruhusu loopholes. Na kwa sababu kuna loopholes na vitu vilivyo ill defined kibao, CCM watashinda tu.
Kwa mfano, sote tunajua rais wa Tanzania akiwa anatekeleza kazi zake za urais hawezi kushitakika mpaka kuwe na impeachment, na rais huyu huyu wa Tanzania ndiye Mwenyekiti wa CCM na mgombea wa urais wa CCM anayetuhumiwa, swali linakuja, Kikwete ametoa nyongeza za mishahara kama mgombea wa CCM au kama rais wa Tanzania? Sheria mpya ya gharama za uchaguzi inaongelea vipi mipaka ya utendaji wa rais kuhusiana na mchakato wa uchaguzi hususan katika kuhakikisha hakuna rushwa inayoachwa kuwezekana ?
Kikwete anaweza kusema aliahidi nyongeza za mishahara kama rais, a sitting president, and it is unfair kumletea Kikwete mgombea charges zinazomhusu Kikwete rais. Kumletea charges hizi Kikwete katika capacity yake iliyohusika (rais) itabidi kwanza process ya impeachment ifanyike, process ya impeachment haiwezi kufanyika bungeni kwa sababu bunge lishavunjwa, labda lipelekwe mahakamani kama katiba yetu inaruhusu, rais awe impeached, aonekane ana cha kujibu.
Rais anapo execute kazi zake za kirais ana immunity ambayo inataka impeachment kwanza kabla ya kumshtaki. Kikwete alitoa ahadi katika capacity yake ya kiraisi akitekeleza kazi za serikali, kuunganisha kazi za serikali na ugombea urais wa chama itakuwa kitu kigumu sana hapo.
Hata kama swala la impeachment litaletwa mbele ya majaji, majaji wanaweza ku reason kwamba kumu impeach rais kutaleta precedent mbaya ambapo kuanzia sasa rais atakuwa ana wakati mgumu kufanya chochote kwa uhuru kwa kuhofia ku violate sheria za uchaguzi. Rais anaweza hata kuogopa kupeleka/ kuzindua miradi ya maji vijijini kwa kuhofia ku violate sheria ya gharama za uchaguzi.
It's not like Kikwete kakamatwa kwenye kikao cha siri cha kampeni yake akiwapa mlungula kina Mgaya na viongozi wengine wa vyama vya wafanyakazi.
kama kweli Tanzania ingekuwa na legal Institutions zinzofanya kazi zake kwa weledi kama Tume ya uchaguzi na ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa basi ni ukweli ulio wazi JK angeondolewa kugombea katika uchaguzi huu, lakini pia unaweza kuona ni kwa kiasi gani CCM wameshtuka na Pingamizi hilo, hivi unahisi nini kitatokea Tendwa akiomba JK aondolewe?
...Kwamba alidanganywa na wasaidizi wake?Aliisoma na kuielewa kabla hajasaini? usikute yale yaleeeeeeeeeeee ya kila siku
Mazee nilitaka kuuliza the very same question hapa.
Nahisi zitatolewa sheria hata za kikoloni za 1901 zilizotoholewa kutoka British India kumpiga coup Tendwa na kuonyesha kwamba uamuzi wake ni null and void, CCM watapiga rufaa mahakamani na mchezo utaendelea mahakamani with a view to reinstate Kikwete.
Halafu Tendwa better have a plane ticket out of the country and some mask at the ready.
But it won't have to come to that.Tendwa ni mtu wao.