Usedcountrynewpipo
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 3,636
- 2,734
Nimemsifu Mkulu kwa maamuzi magumu aliyoyachukua kuwakinga 'wanyonge' dhidi ya uonevu wa utashi wa kisiasa. Maamuzi ya Mkulu yamenikumbusha mtihani kama huo aliokabiliwa nao Pilato. Pilato alikuwa na mamlaka ya kumwacha huru Yesu Kristo na alikuwa na nafasi hiyo moja tu. Lakini kutokana na kelele za Wayahudi Pilato alilazimika kumwachia huru Baraba alikyekuwa mhalifu wa hali ya juu.
Pilato alitoa hukumu yake kwa kusikiliza kelele za watu. Kikwete ametoa haki kwa kuangalia hali halisi. Iwapo angesikiliza kelele za wabunge, wanasiasa na wanaharakati wengine leo hii kuna wanyonge wangeonewa kwa kuonekana kuwa wanyang'anyi. Iwapo kweli IPTL ilistahili kulipwa pesa zake, kwa nini isilipwe? Iwapo watu wako na sympath kwa wamachinga pale wanaponyang'anywa haki zao, ni vema pia kuwa na thympathy kwa watu wengine hata kama wametuzidi kipato na uwezo wa mali.
Mtu unapokuwa rais, inabidi kutoa maamuzi kulingana na haki, na sio kwa ushabiki wa kisiasa. Nampongeza JK kwa kufaulu mtihani huu mgumu uliomshinda Pilato...
Pilato alitoa hukumu yake kwa kusikiliza kelele za watu. Kikwete ametoa haki kwa kuangalia hali halisi. Iwapo angesikiliza kelele za wabunge, wanasiasa na wanaharakati wengine leo hii kuna wanyonge wangeonewa kwa kuonekana kuwa wanyang'anyi. Iwapo kweli IPTL ilistahili kulipwa pesa zake, kwa nini isilipwe? Iwapo watu wako na sympath kwa wamachinga pale wanaponyang'anywa haki zao, ni vema pia kuwa na thympathy kwa watu wengine hata kama wametuzidi kipato na uwezo wa mali.
Mtu unapokuwa rais, inabidi kutoa maamuzi kulingana na haki, na sio kwa ushabiki wa kisiasa. Nampongeza JK kwa kufaulu mtihani huu mgumu uliomshinda Pilato...