Kikwete aendelea kumshambulia Magufuli

Papa D

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
753
182
Wakti wa uzinduzi ujenzi wa Barabara ya New Bagamoyo JK aliendelea kuishutumu Wizara ya Ujenzi kwa kusema hadharani kwamba:- Wananchi kujenga kwenye Hifadhi ya Barabara ni Uzembe wa Wizara na Tanroads.

Jamani kuna Mantiki hapo kuishutumu Wizara na Tanroads?

Vipi habari ya kuchakachua noti mpya mbona hatujaskia kauli kali kama hiyo kwa wizara husika?

Jamani tubadilishane mawazo!!!
 
Akikaa kimya mnadai kuna vacuum ya uongozi, akikemea eti anawaumbua mawaziri wake!
Acheni uchokozi!

Tatizo sio kukemea au kukaa kimya bali kinachoshutumiwa hapa ni ukosefu wa busara katika kufanya hivyo.
 
sera za CCM zimeanza kutekelezwa kwa kasi zaidi.....UPANUZI WA BARABARA TOKA MWENGE UNAENEDELEA...HONGERENI CCM KWA KUBUNI NJIA YA KUPUNGUZA FOLNI NA KUKUZA UCHUMI
 
Mr presidentttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttt huyo anakata mbuga, mimi naona anatuyeyusha tu eti leo kaongea kwa ukali duh nikasema kikombeeeee kikombeeee kikombeeeee anabadilika
 
Mbona alipokuwepo Waziri Kawambwa hajawahi kukemea Tanroad na Wizara na madudu yalikuwepo

Umwona tena leo kwa kawambwa wizara ya elimu.
Hawa wote JK, Kawambwa ni sanaa tu na sanaa yenyewe hawaijui.
Wanajichekeshachekesha tu kwenye tivii hali wanachokiongea hakichekeshi na wasikilizaji wako sirias
 
Kutumia neno amemshambulia tena Magufuli kwa mtu ambaye hajasikia kwenye vyombo vya habari anaweza kukuelewa vibaya. Jk hakumshambulia Magufulu alikuwa anaeleza mapungufu ya wajanja wanaoweza kutumia ujanja na kuuibia serikali kwenye mradi wa kupanua barabara ya Mwenge - TEGETA na kuimbia wizara hiyo ikae mkao wa tahadhari na wajanja hao ambao amesema wamemchosha na haina budi wakashughulikiwa haraka. Lakini pia akaeleza kutorishwa kwake na hatua ya kuwaacha wananchi kuvamia maeneo ya wazi na hifadhi ya barabara na hili aliliekeza pia kwa Tanroads na kuwaagiza kwa kuanzia hataki kuona mtu aliyejenga ukuta pale jangwani anaendela na ujenzi huo na kazi hiyo amewaagiza tanroads kubomoa wenyewe kwani ndio wameacha kitendo hicho kikafanyika na akasisitiza mtu huyo akiishitaki serikali basi waliotoa kibali kwa mtu huyo watalipa fedha hizo kutoka mifukoni kwao.

katika hatua hiyo, Magufuli akasema wafanyabiashara wa soko la Tegeta waondoke mara moja kupisha upanuzi huo na kwamba akikawakuta hapo hakuna wa kulaumiwa na akamuomba Rais kuwa kwa agizo hilo anatumaini wataondoka kabla hajawaondoa kwa nguvu na kumuomba Rais JK kwamba wakikimbilia kwake asiwasikilize.
 
Akikaa kimya mnadai kuna vacuum ya uongozi, akikemea eti anawaumbua mawaziri wake!
Acheni uchokozi!

Kwahili naungana na wewe!me sipendi jk nor sipendi ccm ila ttz watz waga haturidhiki,mtu akikaa tu wanasema akifanya kitu wanasema!jmn mnataka nn?yan kwa mtindo huu hta akiingia slaa mtaona hafanyi kitu jamani
 
Wana-JF napendekeza kupigie debe kujengwa kwa Tanzania Executive Trauma Centre (kituo cha tiba cha akili zilizovurugika na kuathirika) kule maka makuu ya CCM Chimwaga Dodoma na matawi yake yawekwe pale State House Magogoni, makao makuu ya wilaya ya Monduli pamoja na kule Kigoma ili kusaidia kuokoa athari zake kwenye mwenendo na kauli za baadhi ya wana-CCM ambao hivi sasa mtu huhitaji kuambiwa kwamba siku nyingi wanaishi nje kabisa ya nafsi zao zilizozoeleka.

Laa sivyo basi jamii ya Tanzania ijiandae kabisa kuishi na gharama yake kubwa tutakayoishudia si kipindi kirefu sana hapo mbeleni. Daktari bingwa wa magonjwa akili na kuathirika mtu ki-saikoloji, Prof Kilonzo wa Muhimbili, chonde jiandae kupokea wagonjwa wengi sana wanaohitaji ushauri wa kitaam zaidi.

Wakati ambapo tunashuhudia dalili zote za 'JOTO INAPANDA JOTO INASHUKA' ulimi kudondoka watu, hivi sasa vijana ndio tunakuja ki-Tahrir Square zaidi ili tukatetee haki yetu ya kutunga katiba sisi wenyewe bidha bughudha za watawala.

Giya hiyo itakapowekwe Mzee Kilonzo kazi yako itakua kubwa zaidi nchini.
 
sasa kuhusu uzembe huo ulitaka wizara gani ilaumiwe? na kwa jambo kama hilo linaloonekana wazi ulitaka ulitaka aliseme chemba? mi nadhani rais ameonesha kutopendezwa na masuala hayo na ametekeleza jukumu lake ipasavyo
 
Mzee kaulize zaidi na zaidi hilo swali mpaka uje upate jibu mwenyewe. Usiombe kuibia umma ya watu masikini kama sisi hata sahani ya mwisho iliyotengenezwa kwa almasi na ukaanza kuponda nayo raha na maswahiba na bado utegemee kutokua na damu ya kunguru au kuandamwa ka bundi porini!!!

Masikini haporwi haki yake akaisamehe hata siku moja. Jiulizeni na zaidi kwamba ni kitu gani kimekwenda kombo?? Ila mwenzetu JK anaifahamu sana na akipenda huenda akawamegea jibu kiulaini tu!!!

Kwahili naungana na wewe!me sipendi jk nor sipendi ccm ila ttz watz waga haturidhiki,mtu akikaa tu wanasema akifanya kitu wanasema!jmn mnataka nn?yan kwa mtindo huu hta akiingia slaa mtaona hafanyi kitu jamani
 
Naona sasa kikwete ameanza kujenga mazoea mabaya ya kujifanya amekasirika kwa kutoridhika na utendaji wa baadhi ya wizara. Ninachoshangaa kwa nini amemwandama mhe. Magufuli wakati wizara nyingine kama madini ni uozo mtupu. Au ndiyo mbinu za kumalizana kuelekea 2015i





!!!!
 
Ukiwa na akili fupi utadhani anamkemea Waziri Magufuli! Lakini anakemea wizara yenye wataalamu ambayo ni full time and permanent employeed! sasa asisemee hilo kwa kuwa leo magufuli ni waziri? tuache cheap politics. Wizara ni taasisi hai ambayo haikomi au kuanza pale Magufuli akiwa waziri au asipokuwa waziri wa wizara hiyo.
 
Mr presidentttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttttt huyo anakata mbuga, mimi naona anatuyeyusha tu eti leo kaongea kwa ukali duh nikasema kikombeeeee kikombeeee kikombeeeee anabadilika
Wewe ndiwe pumba kabisa, yaelekea huna jambo la kufanya. Pole sana.
 
Back
Top Bottom