Haya yote ni serikali kushindwa kutawala chini ya CCM, na kukimbilia kikombe ili kutuliza vuguvugu la mabadiliko, hakika tujiandae kuona rangi ambazo hata hatujawahi kuziona.
Serikali yoyote iliyopoteza mwelekeo siku zote huwa inakumbatia hoja nyepesi nyepesi, kama ilivyotokea kwa Mobutu ambaye alishia kuwashinikiza wana muziki wa kizaire wamwimbie kwenye nyimbo zake, mwishowe akazikwa na watu wachache katika maziko yasiyo kuwa na heshima.
Kama CCM na viongozi wake wanasoma alama za nyakati vizuri wajiandae kuelekea huko, pona yao ni kujichuna ngozi na kutoa nyama ibaki mifupa walioikataa ya azimio la arusha.
Nje ya hapo ni kuporomoshwa kwa kishindo kikuu na chama kusambaratika mpaka baada ya miaka hamsini mingine.
iman yetu ndiyo itakayotuokoa....hakika tupo safarini....tutaona mengi na ya kustaaajabisha..... so tusiogope juu ya haya.... tuangalie mambo muhimu ya nchi,tunawezaje kukidhi haja za watanzania...miundombinu hali ngumu ya maisha... endapo mambo haya tungeyapa promotion na kuwa vinywani mwa watu kila siku hakika tanzania hii ingekuwa si kama tuionavyo... lakin kwa mambo ya msimu tupo attention sana... mungu bariki africa mungu bariki TANZANIA!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.