Kikokotoo cha kustaafu kisilete ubishi

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,313
12,613
Hakuna ambae hatastaafu kazi, kesho kama sio wewe utakaestaafu basi atastaafu baba yako, shangazi, babu, mama mkubwa, dada, kaka, mama, baba mdogo, jirani nk. Hivyo, haki lazima itendeke hata kwa anaeachishwa au kuacha Kazi mwenyewe apewe chake.

Kitu cha msingi ni elimu ya kustaafu kazi itolewe kwenye mitaala yetu ya sekondari ili kila MTU bila kujali anafanya Kazi gani afahamu namna ya kushughulikia kustaafu kwake Kazi.

Kila mfanyakazi na kila kijana wa Leo lazima afahamu kuwa iko siku siku atazeeka na kushindwa kufanya hiki anachokifanya Leo kupata chakula, malazi, mavazi, matibabu na starehe, hivyo aanze kuanzia sasa kuwaza na kuchukua hatua juu ya namna atavyopata chakula, malazi, mavazi na matibabu yake siku akiacha Kazi kwa uzee au ugonjwa, au kuachishwa Kazi.

Kikokotoo kisiwe na mizengwe ndani yake, kikokotoo lazima kijikumbushe kuwa hata hii misharahara wanayopewa watumishi Leo ni midogo sana kuliko uhalisia, wanapunjwa sana sana sana. Hii sio mishahara bali ni posho tu wanapewa. Hivyo kikokotoo kilenge pia kurekebisha athari za mishahara mishahara midogo wanayolipwa watumishi.

Hivyo hakuna mtumishi awe waziri, mbunge, mkuu wa majeshi au mwalimu asiyetaka kikokotoo kinachompa ahueni pale atakapostaafu.
 
Watumishi hasa awamu ya tano wameumuzwa sana jamani?/miaka mitano hakuna nyongeza ni hatari sana mafao yao yatapunjwa !?? Sana wameishi kwa kudhalilika sana !!! Tunaomba mamlaka husika ziwafute machozi hawa watu!!
 
Watumishi hasa awamu ya tano wameumuzwa sana jamani?/miaka mitano hakuna nyongeza ni hatari sana mafao yao yatapunjwa !?? Sana wameishi kwa kudhalilika sana !!! Tunaomba mamlaka husika ziwafute machozi hawa watu!!
Sasa kama kikokotoo hakitazingatia kuwa kwa miaka 6 watumishi hawakupandishwa madaraja wala kupatiwa nyonheza ya mishahara hicho kikokotoo kitakuwa cha kijambazi kuibia watumishi mchana kweupe.
 
Sasa kama kikokotoo hakitazingatia kuwa kwa miaka 6 watumishi hawakupandishwa madaraja wala kupatiwa nyonheza ya mishahara hicho kikokotoo kitakuwa cha kijambazi kuibia watumishi mchana kweupe.
Kiukweli mwendazake amemuachia mama zigo zito mno mno mno yan Samia unakazi Mama!?? Mifumo ilivurugwa mnono sijui angekaa miaka kumi na hiyo ambayo Ndugai na kundi lake walitaka aongezewe nchi ingekuaje
 
Fao la kujitoa vipi,, nimechoka na ajira ya muhindi nataka niingie kitaa lakini mtaji wenyewe ni huto tusenti tulitopo huko NSSF
Msaada kwa anayejua
 
  • Thanks
Reactions: rr3
Kiukweli mwendazake amemuachia mama zigo zito mno mno mno yan Samia unakazi Mama!?? Mifumo ilivurugwa mnono sijui angekaa miaka kumi na hiyo ambayo Ndugai na kundi lake walitaka aongezewe nchi ingekuaje
Msala aliouacha kwa mama Samia no pamoja na ahadi za papo kwa papo bila kuangalia mapato, kusema machinga wasiguswe ni Bomu linaloweza kumlipukia MTU yeyote SAA yoyote popote, kuahidi ajira kwa JKT wanaotumiwa kwenye Kazi za ujenzi miradi ya serikali na kutoaji, kutopandisha madaraja na mishahara kwa watumishi kwa muda mrefu, kufukuza wafanyabiashara na kupiga marufuku vyama vya siasa visifanye Kazi zao
 
Fao la kujitoa vipi,, nimechoka na ajira ya muhindi nataka niingie kitaa lakini mtaji wenyewe ni huto tusenti tulitopo huko NSSF
Msaada kwa anayejua
Kumnyima MTU FAO LA kujitoa nikulazimisha MTU aajiriwe kwa lazima hata kama hapendi, Kwani 85% ya watu wetu wetu hawajaariwa na hawana FAO LA uzeeni wala LA kujitoa kulima, kufuga na kuvua. Mpeni tu hela yake akaungane na wenzake wakulima, wafugani na wavuvi wasiokuwa na FAO lolote.
 
Hakuna ambae hatastaafu kazi, kesho kama sio wewe utakaestaafu basi atastaafu baba yako, shangazi, babu, mama mkubwa, dada, kaka, mama, baba mdogo, jirani nk. Hivyo, haki lazima itendeke hata kwa anaeachishwa au kuacha Kazi mwenyewe apewe chake.

Kitu cha msingi ni elimu ya kustaafu kazi itolewe kwenye mitaala yetu ya sekondari ili kila MTU bila kujali anafanya Kazi gani afahamu namna ya kushughulikia kustaafu kwake Kazi.

Kila mfanyakazi na kila kijana wa Leo lazima afahamu kuwa iko siku siku atazeeka na kushindwa kufanya hiki anachokifanya Leo kupata chakula, malazi, mavazi, matibabu na starehe, hivyo aanze kuanzia sasa kuwaza na kuchukua hatua juu ya namna atavyopata chakula, malazi, mavazi na matibabu yake siku akiacha Kazi kwa uzee au ugonjwa, au kuachishwa Kazi.

Kikokotoo kisiwe na mizengwe ndani yake, kikokotoo lazima kijikumbushe kuwa hata hii misharahara wanayopewa watumishi Leo ni midogo sana kuliko uhalisia, wanapunjwa sana sana sana. Hii sio mishahara bali ni posho tu wanapewa. Hivyo kikokotoo kilenge pia kurekebisha athari za mishahara mishahara midogo wanayolipwa watumishi.

Hivyo hakuna mtumishi awe waziri, mbunge, mkuu wa majeshi au mwalimu asiyetaka kikokotoo kinachompa ahueni pale atakapostaafu.
Usisahau wabunge wakimaliza 200 mls kabla ya kufunga bunge la mwsho inakuwa kwenye acc zao.
Hawawezi kukumbuka wewe
 
Kiukweli mwendazake amemuachia mama zigo zito mno mno mno yan Samia unakazi Mama!?? Mifumo ilivurugwa mnono sijui angekaa miaka kumi na hiyo ambayo Ndugai na kundi lake walitaka aongezewe nchi ingekuaje

Bwana Yule angeharibu Sana nchi thanks God 17/03/2021.
 
Watumishi hasa awamu ya tano wameumuzwa sana jamani?/miaka mitano hakuna nyongeza ni hatari sana mafao yao yatapunjwa !?? Sana wameishi kwa kudhalilika sana !!! Tunaomba mamlaka husika ziwafute machozi hawa watu!!
Kama mishahara Yao haikupanda kwa miaka 5, hii inamaana kuwa hata malipo Yao ya uzeeni yataathiriwa na jambo hili kwakuwa makato Yao yamepungua pia.
 
Kama mishahara Yao haikupanda kwa miaka 5, hii inamaana kuwa hata malipo Yao ya uzeeni yataathiriwa na jambo hili kwakuwa makato Yao yamepungua pia.

Ndivyo ilivyo.bwana Yule alikuwa katili Sana.wengine aliuwa mojakwa moja wengine anawauwa taratibu.
 
Ndivyo ilivyo.bwana Yule alikuwa katili Sana.wengine aliuwa mojakwa moja wengine anawauwa taratibu.
Kama taifa tusifanye mchezo na Katiba mpya safi inayoweza kuchuja na kudhibiti wagombea wasiofaa. Katiba ambayo inaagiza mgombea achunguzwe sio TU uraia, elimu na uzoefu wake bali hata afya yake ya mwili, akili na kijamii,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom