Kikao cha wanaume

Kikao cha wanaume

Daudi1

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2013
Posts
14,563
Reaction score
22,838
Habari ya muda wanajamii naomba tujadiliane hili katika jamii yetu tukiwa kama wanaume karibuni

Najua hapa kijijini kwetu kuna uhuru wa kuongea bila kuvunja sheria za kijiji nami natumia uhuru huo huo,Langu moja tu ni kuhusu hizi fake ID. Wote tunatumia fake ID na zinasaidia mambo mengi,zinafanya mtu unatoa lolote la moyoni bila kujali lakini kuna watu wanazo Id mbili mbili sio shida kwakuwa sheria za kijiji zinaruhusu

Sasa hili la mwanaume kutumia ID ya kike linamaanisha nini? Humu ndani kama jina la kijiji linavyojieleza watu wanajenga mahusiano,wanatengeneza urafiki,sasa kama mwanaume unapotumia ID ya kike unataka kutuambia nini? kwamba unafurahi wanaume wanavyokutongoza? au unafurahia unavyotoa maada kama mwanamke na watu wanavyotoa maoni yao,furaha inakuwa wapi haswa? sijui kama kua wanawake wanatumia ID ya kiume pia ila nauliza tu kwa wanaume wenzangu hili mnalichukuliaje?

Uhuru unapopitiliza madhara yake ndiyo haya sijui mpaka mtu unatumia ID ya kike unakuwa umefikiria nini? kama kuna wanaume wanapumuliwa visogoni basi waandike zile ID zao Ant fulani ili mtu anapoomba urafiki ajue ni rafiki wa aina gani aliye naye.

Ni hilo tu ndugu zangu sijui na wewe kwa mtazamo wako unalionaje hilo,ni vizuri ukachangia maada iliyowekwa maana wengine mtaanza kusema ooh umekutana nayo hapana ndugu sijakutana nayo ila nimeona niulize tu kwenu mnalionaje,na kama halijakaa sawa basi tuungane tulipinge hilo kwa sauti moja hata hao watunga sheria wanaweza kubadilisha kama mtaona ni vema
********************
Karibuni​
Cc: kwa wanaume wote na wanawake karibu mtuambie mnajisikiaje mwanaume akitumia ID ya kike?
 
Mkuu mimi naungana na wewe ujue hata kama unazo zaidi ya moja kama mwanaume endelea na jinsia yako na kama mwanamke halikadhalika pia

Sababu unawabania riziki wenye shida za ukweli, mfano mtu akilini mwako unajua huyu mrembo unamtokea kumbe njemba inajifanya mrembo kwa kweli hapo ni kuzibiana fursa
 
Mimi hata dhana ya ID mbili siielewi, anyways ngoja nikale makande kwanza!!!
Labda wengine wanajiadhari na Ban lakini vipi kuhusu hawa wanatumia za kike?
 
mrembo mashalaah.,
Unaitwa huku uje ujitetee maana watu wa tabia yako wanazidi humu. Mwanaume unafikiaje hiyo hatua aisee? Wanaume wa kizazi hiki tumemuangusha Mungu kwa sehem kubwa sana, Mungu tusamehe tu ni baadhi yetu wanachafua heshma kubwa uliotupatia.
 
Last edited by a moderator:
ndo mana unatakiwa kuwa greatthinker lasivyo unaingilia bongo za watu,JIONGEZE ndo mana ya uhuru you are so young to judge the undefined
 
Uthibitisho wa kuridhisha, kuhitimisha, na usiopingika kuwa kuna mwanaume anatumia ID ya kike uko wapi?
Hizi siyo tuhuma kwamba zinahitaj ushahidi ni hoja ya mwanaume kutumia ID ya kike inamaanisha nini?
 
Unajua, in my mind men are the stronger sex. We admire them for their manhood, their conduct of affairs etc etc. Ukiwa kama mwanamke ukatamani kuwa mwanamme hamna atakaekushangaa because they will take it as appreciation of the opposite sex.

But ukiwa mwanaume ukawa unaongea kike kike, ukawa unaleta issue za kike hell there will be a price to pay because people won't take it lightly.

What man wishes to be a woman? It is considered weak. And gay.
 
Unajua, in my mind men are the stronger sex. We admire them for their manhood, their conduct of affairs etc etc. Ukiwa kama mwanamke ukatamani kuwa mwanamme hamna atakaekushangaa because they will take it as appreciation of the opposite sex.

But ukiwa mwanaume ukawa unaongea kike kike, ukawa unaleta issue za kike hell there will be a price to pay because people won't take it lightly.

What man wishes to be a woman? It is considered weak. And gay.
Well said mkuu ndo maana hata mimi nikauliza nikiwa na mtazamo kama wako,sasa sijui inakuaje,ngoja tuwasikilize wanasemaje
 
ndo mana unatakiwa kuwa greatthinker lasivyo unaingilia bongo za watu,JIONGEZE ndo mana ya uhuru you are so young to judge the undefined
Hakuna aliyehukumu,na kwa kutumia ID fake haiondoi uhalisia wa mwanamke au mwanaume,uhuru upo na kwa mtazamo wako kama mwanaume uhuru huu unatakiwa kuwa hivi? karibu
 
Anayejua ni yeye tu.

Kama yupo au wapo basi waulize wao.
Wewe kwa mtazamo wako unalionaje,inakuaje utakapojkuta unawasiliana na mtu PM ukidhani wa kike kumbe wa kiume,utafikiria nini kuhusu huyo mwanaume?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom