ng'adi lawi
JF-Expert Member
- Sep 27, 2014
- 2,956
- 1,116
Ukawa mgekuwa na lengo la kusogea mbele mgefanikiwa lkn target ya kuchukua dola kwa 2015 itawapoteza bado mu wachanga sana wingi wa watu siyo sababu ya kuwa ndio uwezo wenu kwani mambo mengi mmekuwa mnafanya ki shabiki tuu na kelele nyingi huku mkitegemea nguvu ya umma huo cyo ukomavu wa kisiasa hamfai bado.
CCM hamlali kwa hofu ya UKAWA? Kushika dola hakuna cha uchanga. Kura za rais na wabunge zikitosha dola tayari. Baada ya uchaguzi kinachobadilika ni rais na baraza la mawaziri tu vyombo vingine vinabaki kama vilivyo. Wananchi wanachotaka ni mabadiliko ktk itendaji na siyo 'business as usual' kama ccm walivyozoea. CCM acheni hofu na kuchonganisha Ukawa hila zenu ziko hadharani na hamwezi kutugawa safari hii.