TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Kikao cha Kamati Kuu ya halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi kilichokuwa kikutane leo saa tano asubuhi, kimeahirishwa kutokana na kikao cha Maadili chini ya Mwenyekiti wake Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete kilichokaa mapema asubuhi kuchukua muda mrefu kuliko ilivyotegemewa kwenye ratiba.
Hivyo Kikao cha Kamati Kuu kinatarajia kufanyika majira ya saa kumi jioni ya leo, na kwamba wajumbe ambao walishafika eneo la ukumbi wa mikutano wa ofisi za Makao Makuu ya CCM maarufu kama whitehouse wametakiwa kuondoka na kurejea tena baadae saa kumi alasiri.
Kwa taarifa sahihi za mijadala na maazimio ya kikao hicho cha Kamati Kuu, fuatilia akaunti rasmi ya twitter ya Chama Cha Mapinduzi kwa anuani hii;
wajumbe wa Kamati Kuu wakijiandaa na Kikao kinachotegemea kuanza muda mfupi ujao.
Hivyo Kikao cha Kamati Kuu kinatarajia kufanyika majira ya saa kumi jioni ya leo, na kwamba wajumbe ambao walishafika eneo la ukumbi wa mikutano wa ofisi za Makao Makuu ya CCM maarufu kama whitehouse wametakiwa kuondoka na kurejea tena baadae saa kumi alasiri.
Kwa taarifa sahihi za mijadala na maazimio ya kikao hicho cha Kamati Kuu, fuatilia akaunti rasmi ya twitter ya Chama Cha Mapinduzi kwa anuani hii;
wajumbe wa Kamati Kuu wakijiandaa na Kikao kinachotegemea kuanza muda mfupi ujao.