Pakome
JF-Expert Member
- Dec 8, 2024
- 1,541
- 916
Nimeandika ujumbe huu ili baadaye Muumba asinilaumu kwa kushindwa kutoa neno linaloweza kuponya maelfu ya vijana wenzangu
Tumekuwa tukijadili mada nyingi hapa JF kwa muda mrefu sana hasa mada tata ambazo zinafundisha nidhamu, mada zilizopelekea mzozo mkali lakini baada ya wasomaji kutuliza hasira baadaye wakagundua nilikuwa sahihi
Mfano nilipokosoa Kanisa la Ufufuo na Uzima pale lilipotuhumu Jeshi la Polisi lakini baada ya Kanisa kusoma andiko langu wakajirekebisha na kurudi na malalamiko yaliyohusisha upotevu wa mali na fedha za Kanisa, malalamiko ambayo hayakudhalilisha tena Jeshi la Polisi
Kwahiyo pamoja na Ukaidi walionao watu bado wanaweza kupona
Tutazidi kukabana koo hivi hivi na kuchaniana mashati mpaka pale wasomaji watakapogundua kuwa makosa ni ya kuachana nayo
Jambo kubwa lililonigusa sana ni kuhusiana na mipango ya vijana juu ya maswala ya siasa
Mipango ambayo imekuwa ikilenga maandamano na mambo mengi ya kisiasa na hata yale yanayovunja utu
Vijana wenzangu, ukweli mchungu ni kuwa Raisi yeyote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huwa haondolewi madarakani kwa njia za kudhalilisha au kutweza utu wa binadamu
Sheria na Katiba ya Tanzania vimelaani matendo hayo tangu enzi za Mwl Nyerere
Matendo hayo yamebainishwa kama kufuru kwa nchi ya Tanzania
Wananchi wa Tanzania pamoja na Serikali yake waliwekeana kiapo hicho na kukubaliana Kikatiba tangu enzi za Mwl Nyerere
Kwahiyo, endapo utafanya makosa hayo utakuwa umevunja maagano pamoja na makubaliano ya Kikatiba na Kisheria Tanzania iliyowekeana na Wananchi wake tangu Mwezi wa tatu, tarehe 16 mwaka 1977
Ushauri wangu, sitakuchagulia, utajiongeza mwenyewe lakini lolote lile litakalokupata utalazimika kujilaumu mwenyewe kulingana na maamuzi yako
Matatizo ya Tanzania yanawezakutatuliwa kwa njia za kistaarabu na utulivu
Serikali inaweza kuwaponya Wananchi wake lakini na Wananchi wanaweza kuiponya Serikali yao kwa njia za busara
Matatizo ya Tanzania yanaumiza pande zote mbili Wananchi na Serikali yake
Wananchi wanapotaabika basi Serikali inatawaliwa na malalamiko yasiyoisha hata kupelekea kukosa amani
Vilevile Serikali inapotaabika basi Wananchi wanakosa huduma bora, taabu zinakuwa nyingi kwa Wananchi
Kwahiyo ni matatizo yanayogusa pande zote mbili ndiyo sababu watu wenye busara hawaoni lawama na visasi kama njia bora za kutatua matatizo ya nchi
Tumekuwa tukijadili mada nyingi hapa JF kwa muda mrefu sana hasa mada tata ambazo zinafundisha nidhamu, mada zilizopelekea mzozo mkali lakini baada ya wasomaji kutuliza hasira baadaye wakagundua nilikuwa sahihi
Mfano nilipokosoa Kanisa la Ufufuo na Uzima pale lilipotuhumu Jeshi la Polisi lakini baada ya Kanisa kusoma andiko langu wakajirekebisha na kurudi na malalamiko yaliyohusisha upotevu wa mali na fedha za Kanisa, malalamiko ambayo hayakudhalilisha tena Jeshi la Polisi
Kwahiyo pamoja na Ukaidi walionao watu bado wanaweza kupona
Tutazidi kukabana koo hivi hivi na kuchaniana mashati mpaka pale wasomaji watakapogundua kuwa makosa ni ya kuachana nayo
Jambo kubwa lililonigusa sana ni kuhusiana na mipango ya vijana juu ya maswala ya siasa
Mipango ambayo imekuwa ikilenga maandamano na mambo mengi ya kisiasa na hata yale yanayovunja utu
Vijana wenzangu, ukweli mchungu ni kuwa Raisi yeyote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huwa haondolewi madarakani kwa njia za kudhalilisha au kutweza utu wa binadamu
Sheria na Katiba ya Tanzania vimelaani matendo hayo tangu enzi za Mwl Nyerere
Matendo hayo yamebainishwa kama kufuru kwa nchi ya Tanzania
Wananchi wa Tanzania pamoja na Serikali yake waliwekeana kiapo hicho na kukubaliana Kikatiba tangu enzi za Mwl Nyerere
Kwahiyo, endapo utafanya makosa hayo utakuwa umevunja maagano pamoja na makubaliano ya Kikatiba na Kisheria Tanzania iliyowekeana na Wananchi wake tangu Mwezi wa tatu, tarehe 16 mwaka 1977
Ushauri wangu, sitakuchagulia, utajiongeza mwenyewe lakini lolote lile litakalokupata utalazimika kujilaumu mwenyewe kulingana na maamuzi yako
Matatizo ya Tanzania yanawezakutatuliwa kwa njia za kistaarabu na utulivu
Serikali inaweza kuwaponya Wananchi wake lakini na Wananchi wanaweza kuiponya Serikali yao kwa njia za busara
Matatizo ya Tanzania yanaumiza pande zote mbili Wananchi na Serikali yake
Wananchi wanapotaabika basi Serikali inatawaliwa na malalamiko yasiyoisha hata kupelekea kukosa amani
Vilevile Serikali inapotaabika basi Wananchi wanakosa huduma bora, taabu zinakuwa nyingi kwa Wananchi
Kwahiyo ni matatizo yanayogusa pande zote mbili ndiyo sababu watu wenye busara hawaoni lawama na visasi kama njia bora za kutatua matatizo ya nchi