Kijana mpambanaji, hatma yako ipo mkononi mwako

Kijana mpambanaji, hatma yako ipo mkononi mwako

Rungwe88

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2013
Posts
307
Reaction score
610
Nitaandika kwa kifupi sana hii mada.
Kuna vijana wanajitafuta kutoka kiuchumi ili kukizi mahitaji muhimu kama chakula, malazi(nyumba), na mavazi kwake binafsi, familia, ndugu n k.

Sasa yameongezeka mahitaji muhimu mengine kama gari, simu za gharama n.k

Sasa kijana mpambanaji hakuna kazi, Biashara, mradi n.k kinachoweza kukufanya kumudu maisha au kua tajiri zaidi ya kile unachopenda kufanya.

Kuna watu wanasema Kuna Biashara ile, kazi hii, mradi fulani n.k ukifanya ndio utafanikiwa kimaisha.
Ukweli ni kwamba Kuna asilimia kubwa kufanikiwa kimaisha, kipesa n.k ukifanya kitu unachopenda kwa ufanisi na ubora wa Hali ya juu kuliko watu wengine mnaofanya kitu Cha aina moja.

Mfano kama wewe ni daktari basi kuwa daktari Bora kuliko wengine, vivo hivyo kwa mkulima, mwanamichezo, msanii, mhandisi, mfanyabiashara, betting n.k jifunze kitu unachopenda kila siku kwa adabu, akili, nguvu, nidhamu, ujasiri n.k
Mafanikio yako, yapo mikononi mwako.
Asante
 
Wakati mwingine maisha yanatubagaza na kutubananga Hadi mtu unashindwa kuelewa unapenda kufanya Nini.
Watu wengi Tunafanya kilichopo mbele yetu ilimradi Cha halali ili mkono uende kinywani.
Nimemaliza nachoka mimi kaka yenu
 
Wakati mwingine maisha yanatubagaza na kutubananga Hadi mtu unashindwa kuelewa unapenda kufanya Nini.
Watu wengi Tunafanya kilichopo mbele yetu ilimradi Cha halali ili mkono uende kinywani.
Nimemaliza nachoka mimi kaka yenu
Ukishafika hatua ya kubanangwa na maisha basi ujue upo hatua chache kufikia mafanikio.

Hiyo tafsiri yake ni kwamba una kiu ya juu ya mafanikio ila haufanyi kitu, kazi, Biashara n.k kwa usahihi
 
Wengi tunapenda kufanya kitu ambacho kinatuletea return kubwa bila kujali tunakipenda au laah
Ni sahihi kufanya hivyo, ila kwa upande mwingine hilo ni tatizo sababu ni rahisi sana kukata tamaa kufanya kitu kwa mtazamo huo.

Ni sawa na mwanamke kuolewa sababu ya tamaa ya mali, mali ikiisha na ndoa inavunjika
 
Tuna idea
Hatuna hela
Aisee
Ni mwanzo mzuri, sababu kila kitu kilianza kwenye idea ndio ikaja pesa.
Kama mtu Hana hata idea hilo ni tatizo kubwa zaidi.

Naweza kutaja njia chache za kupata ela au mtaji.
1. Kuajiriwa kwa mda fulani
2. Kukopa kwa ndugu, rafiki, taasisi za fedha n.k
3. Kuuza kitu chako fulani
4. Kupata msaada kama hisani kwa watu wanaokuamini n.k
5. Hata kuiba pia ni chanzo Cha mtaji ( at your own risks).
Angalia wewe una fursa ipi mkononi mwako kati ya hizo chache nne nilizotaja
 
Back
Top Bottom