General Mangi
JF-Expert Member
- Dec 21, 2013
- 15,301
- 23,025
Heri ya Mwaka Mpya waungwana.
Leo napenda kushare na ninyi wana MMU hasa wanaume ambao wana ndoto ya kufika mbali.
Imekuwa kawaida sana kwa mwanaume kutoa pesa au kuhonga (nazungumzia kwa wale mabachela). Vijana wengi tumekuaa wepesi sana kutoa pesa kwa mwanamke ambae huna malengo nae au hata kama una malengo naye lakini matumizi yamekuwa makubwa sana kwake.
Kwa kijana ambae umezaliwa kwenye familia duni, ni wazi kwamba kama inataka kuwa na mapesa mengi kuna vitu lazima uviweke kushoto.
1. Kuhonga
2. Starehe
3. Michango isiyo na umuhimu.
Mwaka 2017 niliamua kufanya maamuzi ya magumu ambayo yalinifanya nionekane tofauti lakini ni mwaka ambao nilipata mafanikio.
Kwanza nilipunguza idadi ya wanawake, nikabakia na mmoja ambaye hata hivyo tulishindwana kutokana na kupenda kutumia pesa pasipo kuitafuta.
Ilikuwa ngumu sana kuamua hivi kwani hakuna kiti kigumu kama kumweleza mpenzi wako kuwa huna pesa, lakini mwishowe nikazoea.
Nilimu kupunguza marafiki wasio na umuhimu. Marafiki wengi ni mzigo, mara leo nirushie elfu 5, mara vocha. Unaweza dharau vipesa hivyo lakini nikwambie ndugu, HAKUNA PESA NDOGO. Wengi waliniona naringa, mchoyo, najitenga lakini ndiyo njia ambayo kwa hali yangu nimeamini itanifikisha mbali, na nimepata matokeo mazuri.
Niliamua kutoshiriki kwenye michango isiyo na umuhimu mfano harusi. Mimi naamini harusi ni jambo binafsi, kama unafanya harusi unapaswa kugharamia kila kitu.
Kutumia pesa za watu kufanya anasa ni ujinga. Mimi kama nitafanya harusi sitomchangisha mtu, hivyo nami sitachangia harusi ya mtu.
Niliamua kupunguza matumizi yasio na lazima, mfano kwenda club, kupiga vyombo, vyakula vya gharama, kupenda vitu vya kisasa n.k
Nilimua kuacha usharobaro, kujifanya classic, msomi, hii ilileta ugomvi hata na mpenzi wangu niliye kuwa naye.
Anyway, nchotaka kuwambia vijana wenzangu, heshimu sana pesa. Pesa ina hitaji nidhamu sana.
Usiendeshwe na hisia za kimwili vinginevyo hutaki kuwa na mapesa mengi au kuja kuishi maisha mazuri.
Ukifikia ujasiri wa kufanya hayo hapo juu, stori za vyuma kukaza utasikia kwa wenzio.
2018 lazima tufanye kweli.
Mangi.
Leo napenda kushare na ninyi wana MMU hasa wanaume ambao wana ndoto ya kufika mbali.
Imekuwa kawaida sana kwa mwanaume kutoa pesa au kuhonga (nazungumzia kwa wale mabachela). Vijana wengi tumekuaa wepesi sana kutoa pesa kwa mwanamke ambae huna malengo nae au hata kama una malengo naye lakini matumizi yamekuwa makubwa sana kwake.
Kwa kijana ambae umezaliwa kwenye familia duni, ni wazi kwamba kama inataka kuwa na mapesa mengi kuna vitu lazima uviweke kushoto.
1. Kuhonga
2. Starehe
3. Michango isiyo na umuhimu.
Mwaka 2017 niliamua kufanya maamuzi ya magumu ambayo yalinifanya nionekane tofauti lakini ni mwaka ambao nilipata mafanikio.
Kwanza nilipunguza idadi ya wanawake, nikabakia na mmoja ambaye hata hivyo tulishindwana kutokana na kupenda kutumia pesa pasipo kuitafuta.
Ilikuwa ngumu sana kuamua hivi kwani hakuna kiti kigumu kama kumweleza mpenzi wako kuwa huna pesa, lakini mwishowe nikazoea.
Nilimu kupunguza marafiki wasio na umuhimu. Marafiki wengi ni mzigo, mara leo nirushie elfu 5, mara vocha. Unaweza dharau vipesa hivyo lakini nikwambie ndugu, HAKUNA PESA NDOGO. Wengi waliniona naringa, mchoyo, najitenga lakini ndiyo njia ambayo kwa hali yangu nimeamini itanifikisha mbali, na nimepata matokeo mazuri.
Niliamua kutoshiriki kwenye michango isiyo na umuhimu mfano harusi. Mimi naamini harusi ni jambo binafsi, kama unafanya harusi unapaswa kugharamia kila kitu.
Kutumia pesa za watu kufanya anasa ni ujinga. Mimi kama nitafanya harusi sitomchangisha mtu, hivyo nami sitachangia harusi ya mtu.
Niliamua kupunguza matumizi yasio na lazima, mfano kwenda club, kupiga vyombo, vyakula vya gharama, kupenda vitu vya kisasa n.k
Nilimua kuacha usharobaro, kujifanya classic, msomi, hii ilileta ugomvi hata na mpenzi wangu niliye kuwa naye.
Anyway, nchotaka kuwambia vijana wenzangu, heshimu sana pesa. Pesa ina hitaji nidhamu sana.
Usiendeshwe na hisia za kimwili vinginevyo hutaki kuwa na mapesa mengi au kuja kuishi maisha mazuri.
Ukifikia ujasiri wa kufanya hayo hapo juu, stori za vyuma kukaza utasikia kwa wenzio.
2018 lazima tufanye kweli.
Mangi.