Kijana aliyekaribia kumkamata aliyerusha Bomu Jumamosi alipigwa risasi.!

Wadau,
Nimekaa, nikatafakari juu ya taarifa inayohusu mlipuko huko Arusha na kujiuliza maswali haya bila jibu:
  1. Ni kwa nini Polisi waende kwenye mkutano wa hadhara (kama huo wa huko Arusha) huku wakiwa na silaha za moto?
  2. Je? Sheria za ulinzi na usalama hasa zile zinazowasimamia Polisi zinasemaje kuhusu ubebaji na utumiaji wao wa silaha za moto?
  3. Hata kama ni kwa kujihami na fujo za raia, yale maji ya kuwasha, risasi za plastic, virungu, n.k viko wapi mpaka watangulize silaha za moto?
  4. Hao viongozi wetu (Pinda, Kikwete, Lukuvi, n.k) ambao mara kwa mara wamekuwa wakiwakingia kifua hawa Polisi wanaoua raia mara kwa mara nao hawajui hizo sheria? Au wao ndio wanaowatuma? Mbona watu kama Pinda na Kikwete hawafananii kuwa na roho kama hizo? (Labda Lukuvi).
  5. .........? :shock:

Naomba mnisaidie kupata majibu ili roho yangu itulie kwenye msimamo mmoja! Ahsanteni.
 
Please take note: huyu majeruhi aliongea mbele ya waziri wa serikali ya Tanzania. Kwa kuwa nahisi upo karibu na serikali. Nakuomba ukafanye verification kwa huyo waziri. Yaani wewe furaha yako ilikuwa haya yaliyosemwa yafichwe, tusiyajue?. Shameless guy


Ni elfu saba mkuu inaongea, siyo yeye.
 
Hizi ni siasa za majitaka tu, nani hawajui mwananchi uandishi wao wa kichochezi na kupidhisha mambo

Sasa kama mwandishi alimhoji majerui hospitali na akasema aliyoyasema, ulitaka mwandishi aandike nini? Wewe unasema Mwananchi ni gazeti linaloandika habari za uongo na majitaka, upande mwingine gazeti hilo ndo linakuwa No. 1 Tanzania kwa uandishi bora na habari zilizohakikiwa, tukisema mtu kama wewe hujitambui, mnaleta maneni ya ki "nchemba nchemba"

Kalaga bhaho...
 
Please take note: huyu majeruhi aliongea mbele ya waziri wa serikali ya Tanzania. Kwa kuwa nahisi upo karibu na serikali. Nakuomba ukafanye verification kwa huyo waziri. Yaani wewe furaha yako ilikuwa haya yaliyosemwa yafichwe, tusiyajue?. Shameless guy
Acha kumpa promo bure huyo,yuko karibu na serikali ipi huyo? Hawa ni wale wachumia tumbo wa 7 thou group hana alijualo zaidi ya paymaster wake Nape na labda cashier wa pale Lumumba. Tulio karibu na serikali tunajua statement ya yule kijana imeleta athari gani. Mkuu Donyongijape hata ndani ya serikali hali sio shwari kabisa, bado kuna kundi kubwa la viongozi (hasa wenye taaluma zao) hawaungi mkono mikakati hii ya kina Mwigulu maana inapoteza maisha ya watu na kuwa tia ulemavu na hakuna ajuaye ni lini ndugu yake atauawa au kujeruhiwa hivyo ni mashaka tuu.
 
Last edited by a moderator:
Nasikia landlords wa kiarusha wameapa kuwafanyia polisi ktk nyumba zao hata ikibidi kuziwasha moto...kwa vile ccm watakuja zijenga kwa sifa.

Nikifikirie ile migomba nahofia polisi.
 
chadema chama cha watanganyika bila kuchagua dini. ndicho chama chenye kukubalika na watanganyika wote kwa kuwa kinatetea maslahi ya wanyonge
 
Back
Top Bottom