Zack Abdul
JF-Expert Member
- Mar 9, 2026
- 509
- 489
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Kenani Kihongosi amesema msingi wa uhai na uimara wa chama ni kuheshimu vikao na maamuzi yake.
Akizungumza Tarime, Kihongosi amesisitiza kuwa viongozi na wanachama walioiva kiitikadi hutambua kuwa maamuzi ya mwisho ya vikao ndiyo maamuzi rasmi ya chama, kwani huko ndiko mipango hujadiliwa, hukubaliwa na kupewa mwelekeo wa pamoja.
Ameeleza kuwa CCM itaendelea kujengwa na wanachama watiifu, wazalendo na wanaoweka maslahi ya chama mbele kuliko makundi au maslahi binafsi.
Soma Pia: Kihongosi: CCM haijawahi kukosea, Hakuna aliye Mkubwa kuliko Chama
“Chama kwanza, watu baadaye. Tukipenda chama chetu, tukalinda umoja, mshikamano na nidhamu ya vikao, tutajenga CCM imara na yenye kuendelea kuaminiwa na wananchi,” amesema Kihongosi.
Aidha, amewataka viongozi kuachana na migawanyiko na kuhakikisha Tarime inabaki kuwa mfano wa umoja, upendo na mshikamano ndani ya Chama Cha Mapinduzi.
Akizungumza Tarime, Kihongosi amesisitiza kuwa viongozi na wanachama walioiva kiitikadi hutambua kuwa maamuzi ya mwisho ya vikao ndiyo maamuzi rasmi ya chama, kwani huko ndiko mipango hujadiliwa, hukubaliwa na kupewa mwelekeo wa pamoja.
Ameeleza kuwa CCM itaendelea kujengwa na wanachama watiifu, wazalendo na wanaoweka maslahi ya chama mbele kuliko makundi au maslahi binafsi.
Soma Pia: Kihongosi: CCM haijawahi kukosea, Hakuna aliye Mkubwa kuliko Chama
“Chama kwanza, watu baadaye. Tukipenda chama chetu, tukalinda umoja, mshikamano na nidhamu ya vikao, tutajenga CCM imara na yenye kuendelea kuaminiwa na wananchi,” amesema Kihongosi.
Aidha, amewataka viongozi kuachana na migawanyiko na kuhakikisha Tarime inabaki kuwa mfano wa umoja, upendo na mshikamano ndani ya Chama Cha Mapinduzi.