Kila kona ya Tanzania naona watu wengi sana wamefurahia Dkt. Kigwangalla kuachwa katika Baraza la Mawaziri. Walioko kwenye sekta ya utalii wamefurahi sana. Cha ajabu hata ambao hawako kwenye sekta ya utalii wamefurahi pia.
Ndugu yangu Khamisi una suala la kujiuliza ni kwanini watu wengi wamefurahia wewe kuachwa na JPM.
Ofcoz kuna vitu vilikuwa vinaniboa hata mimi kama zile tabia zako za kutweet tweet! Hivi Waziri wa Wizara kubwa kama ya Utalii unatoa wapi muda kwa kubishana mitandaoni?
Pole sana ila bado kijana mdogo unao muda wa kujifunza.
Ukishangaa ya Kingwangala utaona maajabu kwa Trump si alikuwa ana tweet mpaka Amri au maelekezo na zinafanyiwa kazi? Sasa Rais Trump na Kingwa wetu ni mlima na Kichuguu.
Hata hivyo uwaziri ni bonus tu, ubunge mbona unatosha sana , si anawawakilisha tu waliomchagua, halafu sio masikini Hamisi ni mpambanaji haswa hata hao walioteuliwa wengi tu hawatamaliza mitano
Washabiki wa simba,ambao wapo upande wa dewji.
Hata hivyo uwaziri ni bonus tu,ubunge mbona unatosha sana ,si anawawakilisha tu waliomchagua,halafu sio masikini hamisi.no mpambanaji haswa.hata hao walioteuliwa wengi tu hawatamaliza mitano.