HKigwangalla
JF-Expert Member
- Feb 6, 2008
- 717
- 971
Niliandika status kwenye FB wall yangu, kwenye twitter, wanabidii na mabadiliko forums, na nilikanusha hilo, maana halikuwepo...sijawahi kukamatwa bali ilikuwa kinyume chake na kwamba waliofanya hivyo walikuwa wana-plot kunichafua ili wasababishe nisiteuliwe na Chama kugombea nafasi ya NEC kupitia Nzega (na wamefanikiwa, hongera zao). Namshukuru Mungu ka-bajeti nilikokuwa nikatumie kwa ajili ya kampeni yangu kwenye NEC nimekatumia kwa mambo mengine, na nimewashinda kwenye uenyekiti, uNEC, Uenezi n.k. Kama nilikamatwa waulize hao wenye magazeti kwa nini hawakupiga picha matukio hayo - kwanza la kugawa vitumbua na mbili la kukamatwa na PCCB? waambie waweke hapa kama ni hadithi za ukweli. Mimi niliishaga acha kuyaamini magazeti 100% siku nyingi sana, huwa nawapa 60% tu!mh dr H Kigwangalla, nakupongeza kwa kunitomeza na kujibu baadhi ya hoja hapa jamvini. KEEP IT UP, natamani na vijana wenzio huko katika ccm ( mwigulu nchemba, january, bashe, lusinde 'kibajaji')wataiga huu mfano wako mzuri.
MH, kuna siku ililetwa habari hapa kuwa umekamatwa nzega ukigawa rushwa ya vitumbua na tsh 2000 kwa wajumbe, tulikusubiri sana hapa jf uje uthibitishe au kukanusha KIMYA!
na mpaka leo hatuujui ukweli ni upI mkuu,,
kwa kuwa leo upo hapa naomba ufafanuzi wako
nikimbie hoja gani sasa hizi blah blah zenu mnazofanya kuwa-please waliowanunulia gadgets? Hamna hoja za saizi yangu hapa nimepoteza muda kiasi cha kutosha tu
AND FINALLY... Kakimbia... Hawezi kugawa tena VITUMBUA !!!
kichwa cha hii habari hakijakaa vizuri...Hivi ndiyo alivyoandika kwenye ukurasa wake wa FaceBook:--
"Hamisi Kigwangalla
4 hours ago
"Uchaguzi Mkuu wa CCM Wilaya ya Nzega umemalizika salama na tumepata viongozi mahiri. Ni imani yangu tukiwapa ushirikiano wa kutosha CCM sasa itakuwa moja, imara na yenye kusonga mbele. Hongereni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Nzega kwa kung'oa kwa kiasi kikubwa vigogo na waasisi wa siasa za ufuasi na wenye kufanya siasa za kumridhisha mtu mmoja tu, pia kwa kuwakwamisha wengi wa wafuasi wa siasa hizo na kuingiza majembe ya ukweli! Mmedhihirisha pesa peke yake si kigezo cha kushinda uchaguzi, mmefanya kweli. Nawashukuruni nyote kwa kufuata na kutumia ushauri wangu kwamba tujenge CCM moja imara, kusiwe na watu wa Kigwangalla na wala wa Selelii, kuwe na wanaCCM wamoja...mlinipa faraja ya ushindi na pale mliponibeba juu juu niliogopa kwamba msije mkawa mmedhamiria kwenda kunitupa, ila nakushukuruni sana hamkufanya hivyo badala yake mlishukuru kwa ushauri wangu..."
"Mara baada ya fununu za matokeo ya uchaguzi kuwa wazi kuna watu wawili maarufu walizimia, na walipozinduka waliangua vilio na hawajaonekana Nzega tena...tunawapa pole na kuwatakia quick recovery huko waliko! Huo ndiyo ushindani...na sisi tunawaambia kuwa wasihofu kitu watatendewa haki siku zote katika chama hiki na katika uongozi huu. Malengo yetu ilikuwa ni kuondoa watu wa hovyo, wachumia tumbo na wanaofanya kazi kwa maelekezo ya mtu mmoja tu na sasa kuweka watu makini na mahiri watakaokisimamisha chama, hata kama itamaanisha kuniadhibu mimi pale itakapobidi...Chama Kwanza, Mtu baadaye! Hakuna mtu maarufu na wa maana ndani ya CCM kuliko CCM yenyewe. Nimesikia wanataka kuikimbia nchi, tunawasihi wasifanye hivyo, waendelee tu kuwa waadilifu na waaminifu kwa chama na kwa nchi na ipo siku mambo yao yatawanyookea tu!"
Inasikitisha sana kumuona mtu anayeitwa Mh Mbunge akijibizana kwa stahili hii. Mkuu, kuna stahili ya kujibu hoja, hoja hazijibiwi kimipasho mipasho hivi. Hapa sasa naanza kuamini kuwa tunaoimaliza CCM ni sisi wenyewe!
Kuna namna ya kujibu hoja, siyo kwa stahili hii. Mbaya zaidi anajibizana na watu asiowafahamu!!!Acha pumba na wewe .. angenyamaza hapa si mngeamini? Kwani dk na yeye si binadam kama wewe hapo . Dr mtu akiweka mguu wewe weka jiwe hivyo hivyo tuone kama wataendelea kukuzushia hapa.
Dr. Hamisi Kigwangalla said:
- Mara baada ya fununu za matokeo ya uchaguzi kuwa wazi kuna watu wawili maarufu walizimia, na walipozinduka waliangua vilio na hawajaonekana Nzega tena...!
- Nimesikia wanataka kuikimbia nchi, tunawasihi wasifanye hivyo, waendelee tu kuwa waadilifu na waaminifu kwa chama...!
- Malengo yetu ilikuwa ni kuondoa watu wa hovyo, wachumia tumbo na wanaofanya kazi kwa maelekezo ya mtu mmoja tu...!
Kigwangalla kaongea vizuri sijaona vijembe vyovyote.
Chama said:...ameongea kama msomi na mwenye dira ya kukitakia chama mema, wengi mnasema vibaya kwa sababu mnachotaka ni migongano ndani ya CCM kwa faida yenu, BIG UP DR.Kigwangalla
Halafu kuna watu wanasema tunataka viongozi wasomi vijana...kaazi kweli kweli!Halafu kuna watu wanasema tunataka viongozi vijana... kadizooo!!!
Naona mmjipanga vijana wa aliyewatuma hapa kwa kazi moja tu, kunichafua, kisa nini mmepewa Ipad za bure...bahati mbaya sana aliyewapeni hizo gadgets amekula hasara maana nyote mmejaa fallacy, hamna hoja na wala uwezo wa kujifunza chochote kwa kuwa na access na information kupitia vyombo hivyo... tatizo la JF ni hilo watu mnajificha nyuma ya alias
nikimbie hoja gani sasa hizi blah blah zenu mnazofanya kuwa-please waliowanunulia gadgets? Hamna hoja za saizi yangu hapa nimepoteza muda kiasi cha kutosha tu
Kuna namna ya kujibu hoja, siyo kwa stahili hii. Mbaya zaidi anajibizana na watu asiowafahamu!!!
Sent from my BlackBerry 9810 using JamiiForums
Nimefuatilia posts zako na naona lazima kuna kitu baina yenu wawili. Haiwezekani umshambulie HKigwangalla kiasi hiki bila sababu yoyote. Labda mkuu ungetuweka wazi ili na sisi tuwe kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuchangia kwenye bifu lenu.
Kaka tulia angalia NYUMA anza UPYA unakwenda MBIO sana KISIASA na hautakuwa hauna
maana mbeleni kama hautajirekebisha, ulianza kwa kasi NCHI yetu UFISADI una MIZIZI wewe
Mwenyewe hauwezi kuiondoa Unatakiwa UWE Na UNYENYEKEVU na sio kujilimbikizia
MADARAKA UBUNGE ULITOSHA sio na U NEC PIA TULIZANA ANZA UPYA sasa hivi kweli
Una Maadui Wengi zaidi ya Marafiki lakini kazi njema itakurudishia MARAFIKI na NEEMA...
THERE IS ALWAYS SILVER LINING IN THE SKY !!!
kwani kikwete baada ya 2015 bado atakua na nguvu?
Ha ha ha hahahahaah Saint Ivuga, naona hapo kwenye vitumbua umepakomalia sana.Rejao unachoongea ni sawa ila kuna muda inabidi tu afanane na hao anaowajibu kwa muda ili kuweza kuwajibu inavyotakiwa . mfano kaambiwa hapo kuwa "kakimbia jukwaa na hawezi kugawa tena vitumbua" so swali kama hilo ama kebehi kama hio angajibu nini? Ni kuipotezea ama kuivaa hivyo hivyo so jamaa hana kosa . Ila mwambie awe anagawa hata vitu vya ukweli kisela sio mavitumbua bhana.
Nimefuatilia posts zako na naona lazima kuna kitu baina yenu wawili. Haiwezekani umshambulie HKigwangalla kiasi hiki bila sababu yoyote. Labda mkuu ungetuweka wazi ili na sisi tuwe kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuchangia kwenye bifu lenu.
Inasikitisha sana kumuona mtu anayeitwa Mh Mbunge akijibizana kwa stahili hii. Mkuu, kuna stahili ya kujibu hoja, hoja hazijibiwi kimipasho mipasho hivi. Hapa sasa naanza kuamini kuwa tunaoimaliza CCM ni sisi wenyewe!
Mipasho ni mipasho tu, hata hadija kopa husema ukweli
if our leaders wanaongea mipasho na sisi kuwashabikia, then we are lost dogs...........
Uongozi unaendana na utashi, heshima, na maarifa.... haijawahi kutokea popote mipasho ikawa na maarifa, utashi au heshima achilia mbali hekima
POLENI SANA