Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,989
Tukio kubwa limeripotiwa kutokea mkoani Kigoma, Wilaya ya Uvinza ambapo Askari wanne wameuawa kwa sababu walitaka kuwanyanganya ng’ombe wafugaji wa jamii ya kisukuma kwenye msitu wa Kagera, Nkanda.
Askari hao wanadaiwa kumpiga risasi mchungaji baada ya kuwagomea wasichukue ng'ombe na wafugaji hao waliposikia kuuliwa kwa mchungaji walienda na zana za jadi wakaua askari watatu na Afisa Misitu mmoja.
Mpaka sasa wananchi zaidi ya 40 wamekamatwa na wengine wanaendelea kusakwa huku vyombo vingi vya habari vikizuiliwa kuripoti suala hilo.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa jamii hiyo ya wafugaji imeamua kujichukulia sheria mkononi baada ya kuchoshwa na matendo haya ya uonevu ambayo yamekuwa endelevu kwa muda mrefu.
UPDATE
Waliofariki ni Afisa msitu mmoja na Mgambo 2.
Inadaiwa kuwa mgambo hao walienda kutekeleza jukumu lao la kukagua eneo hilo la pori ambalo shughuli za kibinadamu zimezuiliwa, ndipo kundi kubwa la watu liliwavamia na kuwashambulia.
Kitendo hiki kilitokea baada ya Mgambo kuanza kuwaondoa mifugo waliowakuta, ambao kwa mujibu wa taratibu hawaruhusiwi kuwepo kwenye eneo hilo.
Watu 46 walikamatwa, na 28 kati yao waliotambuliwa kujihusisha na uvunjifu huo wa amani wamepelekwa mahakamani.
Askari hao wanadaiwa kumpiga risasi mchungaji baada ya kuwagomea wasichukue ng'ombe na wafugaji hao waliposikia kuuliwa kwa mchungaji walienda na zana za jadi wakaua askari watatu na Afisa Misitu mmoja.
Mpaka sasa wananchi zaidi ya 40 wamekamatwa na wengine wanaendelea kusakwa huku vyombo vingi vya habari vikizuiliwa kuripoti suala hilo.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa jamii hiyo ya wafugaji imeamua kujichukulia sheria mkononi baada ya kuchoshwa na matendo haya ya uonevu ambayo yamekuwa endelevu kwa muda mrefu.
UPDATE
Waliofariki ni Afisa msitu mmoja na Mgambo 2.
Inadaiwa kuwa mgambo hao walienda kutekeleza jukumu lao la kukagua eneo hilo la pori ambalo shughuli za kibinadamu zimezuiliwa, ndipo kundi kubwa la watu liliwavamia na kuwashambulia.
Kitendo hiki kilitokea baada ya Mgambo kuanza kuwaondoa mifugo waliowakuta, ambao kwa mujibu wa taratibu hawaruhusiwi kuwepo kwenye eneo hilo.
Watu 46 walikamatwa, na 28 kati yao waliotambuliwa kujihusisha na uvunjifu huo wa amani wamepelekwa mahakamani.