jerrytz
JF-Expert Member
- Oct 10, 2012
- 5,990
- 4,356
Wanajukwaa,
Leo nimeona nishirikiane nanyi katika hoja hii tata. Licha ya wanadamu kuonekana kuzoea kifo bado kifo kimekuwa fumbo kubwa tangu nyakati za zamani, wanafalsafa na wataalaamu wa kada za maisha wameeleza kifo kwa namna tofauti lakini wengi hawakufikia hitimisho.
Nimekuwa nikitafakari kuhusu kifo na nimejenga hoja katika maswali matatu.
1. Je mwanadamu anastahili kufa kwa sababu ya ubinanamu wake?
Nimekuwa nikisikia watu wakisema, baadhi yao kwa kunukuu vitabu vya kidini kwamba kila nafsi lazima ionje umauti. Nini msingi wa kauli hii? Je mwanadamu anakufa kwa sababu ya ubinamu wake au kifo ni sehemu ya kuwa mwanadamu?
2. Kifo kama daraja kuelekea kwenye maisha bora
Hapa ipo dhana/ nadharia ya maisha baada ya kifo, bila kuathiri unaamini nini kuhusu hili, unadhani kuna maisha bora zaidi baada ya kifo? Baadhi ya wakristo wanaamini kuwa tupo duniani ili kuishi maisha yenye haki ya kumpendeza muumbaji ili awapatie zawadi ya uzima wa milele yaani maisha yasiyo na mwisho baada ya kufa. Niseme hili hapa, ni kawaida ya mwanadamu kutamani kuendelea kuishi, hii ipo kwenye akili zetu, maisha yasiyo na mwisho. Kwa waislamu wao wanaamini uwepo wa pepo ambapo wale waliompendeza Mungu wataishi.
3. Kifo kama adhabu kwa mwanadamu
Wapo wanaoamini kutokana na imani zao kuwa mwanadamu anakufa kutimiza adhabu ya kosa lillilofanywa na Adam na Hawa (tamko la Mungu kwa Adam na Hawa katika kitabu cha mwanzo sura ya tatu).Hapa mambo mengi huibuka kama kwanini mfululizo wa adhabu hii uendelee kwa vizazi vyote?! Je ni haki kwa mwanandamu mwingine kufa kwa kosa la Adam na Hawa? ! Hakuna aliyechagua kuwa mwanadamu kwanini tuchaguliwe kufa? ! Hii imefanya wengi kuamini kuwa tunaishi ili tufe.
Hitimisho: Japo kifo kinabaki siri naamini kinaweza kujadilika na kupanua ufahamu wetu kuhusiana nacho.
Leo nimeona nishirikiane nanyi katika hoja hii tata. Licha ya wanadamu kuonekana kuzoea kifo bado kifo kimekuwa fumbo kubwa tangu nyakati za zamani, wanafalsafa na wataalaamu wa kada za maisha wameeleza kifo kwa namna tofauti lakini wengi hawakufikia hitimisho.
Nimekuwa nikitafakari kuhusu kifo na nimejenga hoja katika maswali matatu.
1. Je mwanadamu anastahili kufa kwa sababu ya ubinanamu wake?
Nimekuwa nikisikia watu wakisema, baadhi yao kwa kunukuu vitabu vya kidini kwamba kila nafsi lazima ionje umauti. Nini msingi wa kauli hii? Je mwanadamu anakufa kwa sababu ya ubinamu wake au kifo ni sehemu ya kuwa mwanadamu?
2. Kifo kama daraja kuelekea kwenye maisha bora
Hapa ipo dhana/ nadharia ya maisha baada ya kifo, bila kuathiri unaamini nini kuhusu hili, unadhani kuna maisha bora zaidi baada ya kifo? Baadhi ya wakristo wanaamini kuwa tupo duniani ili kuishi maisha yenye haki ya kumpendeza muumbaji ili awapatie zawadi ya uzima wa milele yaani maisha yasiyo na mwisho baada ya kufa. Niseme hili hapa, ni kawaida ya mwanadamu kutamani kuendelea kuishi, hii ipo kwenye akili zetu, maisha yasiyo na mwisho. Kwa waislamu wao wanaamini uwepo wa pepo ambapo wale waliompendeza Mungu wataishi.
3. Kifo kama adhabu kwa mwanadamu
Wapo wanaoamini kutokana na imani zao kuwa mwanadamu anakufa kutimiza adhabu ya kosa lillilofanywa na Adam na Hawa (tamko la Mungu kwa Adam na Hawa katika kitabu cha mwanzo sura ya tatu).Hapa mambo mengi huibuka kama kwanini mfululizo wa adhabu hii uendelee kwa vizazi vyote?! Je ni haki kwa mwanandamu mwingine kufa kwa kosa la Adam na Hawa? ! Hakuna aliyechagua kuwa mwanadamu kwanini tuchaguliwe kufa? ! Hii imefanya wengi kuamini kuwa tunaishi ili tufe.
Hitimisho: Japo kifo kinabaki siri naamini kinaweza kujadilika na kupanua ufahamu wetu kuhusiana nacho.