Unajua wahubiri wengi huwa wanadai kuwa kifo kilikuwepo kutokana na adhabu juu ya kosa lililotendwa na Adamu na Hawa na bila kosa hilo kusingelikuwa na kifo kitu ambacho siyo sahihi kabisa;Ukweli ni kwamba kifo kilikuwepo hata kabla ya lile kosa isipokuwa Kifo chake kingelikuwa tofauti na hiki kinachotupata,Kifo ambacho tungekuwa nacho ni hiki; 1.Kifo kingelikuwa ni njia tu ya kumfikia Muumba wetu 2.Watu wasingelikuwa wanaogopa kufa,hivyo ingelikuwa ni tukio la furaha sana 3.Watu wangelikufa tu kwa Umri maalumu(yaani baada ya kuzeeka) tofauti na sasa. 4.Watu wangelikuwa tarehe na saa zao za kufa,tofauti na sasa ambapo watu hatujui siku wala saa. 5.Watu tungelikuwa tunauelewa juu ya kule tunakoelekea namna kulivyo.Kumbe ndugu zanguni mtagundua kuwa Dhambi ilifanya kifo kuwa kitu kibaya kinachoogofya sababu ni Uhasama tunaoujenga kati yetu na Mungu,Hivyo wengi tunajawa na hofu,mashaka,wasiwasi,woga,n.k. juu ya siku zetu za kufa kwa kuwa tunajijua kuwa tumekuwa tukimkosea Mungu.