Maseto
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 944
- 546
Wana Jf.habari. Niko hapa Deluksi hotel,karibu na kwenye msiba wa kanumba.watu wamemzingira ajuza mmoja mnene,mfupi akiwa amevaa gauni anayedaiwa ameanguka eneo hili kutokana na ungo wake aliokuwa anasafiria kufeli.anadaiwa kutoa maelezo ya kujichanganya.kuna wanaosema anadai alikuwa anatokea mbagala akienda kwenye msiba wa kanumba,na wengine wanasema alikuwa anatokea sumbawanga kuelekea naigeria akiwa na wenzake wapatao watano kwenye kikao cha wachawi.vijana wameacha msiba na kumzingira bibi huyo,wengine wanamvuta bila utaratibu kama vile mbweha wanavyonyanganyana mzoga.ni balaa hapa.magari yanapita kwa tabu mno.watu wanaimba turudishie kanumba wetu,wengine mwanga!mwanga!