Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

ccm ni udini ni bomu litawaripukia sasa hapa ndipo walipo malizikiwa na propagander zao sasa wanahangaika hakuna njia ya kupita
 
Chama cha zamani hakina mvuto wala sera za kulikomboa taifa dhidi ya ujinga, maradhi na umasikini.Chama kimekuwa chini ya matajiri wanaotumia fedha kuongoza badala ya miiko ya uongozi.Kwaheri chama cha zamani,karibu chama cha demokrasia na maendeleo ili tujenge nchi.
 
CCM ya Kikwete imewafikisha watu waamini kwamba amani na usalama ni kukaa kimya kama kondoo wenye hofu. CCM inatumia hofu hii iliyopandikizwa kuendeleza dhuluma, kukalia haki za watu na kutumia polisi kuaminisha kwamba Tanzania leo kuna magaidi. CCM walianza kupandikiza hofu ya "magaidi' katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga mwaka juzi, wakati aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM, Wilson Mukama alipotangaza kapata habari kwamba CHADEMA wameingiza Mungiki wa Kenya. Polisi hawakuwa na habari na hawakumhoji Mukama.

Mwaka jana, Katibu wa Uchumi wa CCM, Mwigulu Nchemba alizunguka nchi nzima akidai ana mkanda unaoonyesha ugaidi wa CHADEMA. Polisi walijiweka kando na madai hayo. Na pale walipoona wimbi la watu kuhama analojia na kuingia digitali (CHADEMA) linazidi kuongezeka ndipo ‘CCM' wakamkamata Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA, Wilfred Lwakatare kwa madai ni gaidi.
Mwaka jana Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alizunguka nchi nzima akitangaza kwamba Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa ana kadi ya CCM.

Siku Juliana Shonza alipotimuliwa uanachama wa CHADEMA, alikusanya waandishi wa habari na kutapika mambo mengi, mojawapo ni kwamba kuna matumizi mabaya ya fedha za chama. Baada ya kusomea propaganda ndani ya CCM na wakahitimu, wiki iliyopita Shonza na Mtela Mwampamba waliibuka na kudai Dk. Slaa ana mpango wa kumuua Naibu wake, Zitto Kabwe. Makada wawili hao wakaeleza hata mpango huo ulivyo.

Pamoja na kwamba tuhuma hizo nzito zinahitaji Jeshi la Polisi kufanyia kazi, Shonza na Mwampamba wameachwa huru hata kukemewa tu. Hapo ndipo ujue Shonza na Mwampamba, kama ilivyokuwa kwa Nape, Mwigulu na Mukama wametumwa na CCM kutia hofu kama rais mwenyewe aliyedai amesomewa itikafu na misikiti mitatu, lakini amekaa kimya. Kweli rais wa nchi anaombewa afe lakini hachukui hatua? Hii ndiyo CCM!
Nini maana yake CCM? Mtambo huu wa analojia CCM unapaswa kuzimwa 2015 ili kupitia digitali wananchi wapate usikivu mzuri wa habari na waone picha nzuri ya uhuru wao, demokrasia, uchumi, elimu, afya, ustawi wa jamii, mazao yao, barabara zao, uhusiano wao, heshima yao, utu wao na viongozi wasioshinda misibani.

h.sep3.gif
 
thubutu. muulize zitto alivyokoswakoswa kwa sumu. haendi mtu huko.
 
Sisi tunawaelewa wote CDM ni chama makini ngoja 2015 ifike uone
 
2015 sio mbali. Ccm wameigawa nchi yetu kidini, kwa madai kwamba chama cha CUF ni waislam na CHADEMA ni wakristo, japo hawajawah kusema CCM ni dini gani. Ccm wanategemea kutugawa huku kupunguze kasi ya mabadiliko. Lakin kwa uelewa ulivyokua leo, ccm lazima izime
 
Mwenye macho anaona, mwenye masikio anasikia. Hazipiti siku mbili au tatu nchi bila kuwa na vurugu, ghasia, mauaji, malalamiko na kadhalika vinavyotokana na usimamizi mbovu, sera mbovu za utawala, kukosekana haki na utawala bora na tamaa za utajiri kwa wachache ndani ya ngazi karibu zote za utawala.

Wananchi, kwa kuwa wengi tunataka mabadiliko mwaka 2015 inabidi tufanye maamuzi mazito kuwatokomeza hawa magambaz wanatuletea majonzi kila kukicha.
 
Watu hawana ajira,unategemea nini?EL aliwaambia wakampuuza sasa ndiyo matokeo yake!JK tangaza ofisi zote,mabenki,usafiri zifanye kazi masaa 24,kuwe na shift 3,watu wapate ajira na nchi ipate maendeleo haraka haraka.
 
Kama ndio kutimiza lengo lenu la 'kuifanya nchi isitawalike' basi mmefeli!
 
Naona mmeamua kujifariji na kujiliwaza.
 
Mwenye macho anaona, mwenye masikio anasikia. Hazipiti siku mbili au tatu nchi bila kuwa na vurugu, ghasia, mauaji, malalamiko na kadhalika vinavyotokana na usimamizi mbovu, sera mbovu za utawala, kukosekana haki na utawala bora na tamaa za utajiri kwa wachache ndani ya ngazi karibu zote za utawala.

Wananchi, kwa kuwa wengi tunataka mabadiliko mwaka 2015 inabidi tufanye maamuzi mazito kuwatokomeza hawa magambaz wanatuletea majonzi kila kukicha.

Sio lazima iwe 2015,kwani ni nani anayejua mpango wa Mungu?THE HAGUE NI LAZIMA ITIE TEAM TZ SOON VITENDO DHALIMU VYA DOLA HII KANDAMIZI.JE UNAKUMBUKA KAULI YA LT MWALIMU J.K NYERERE?IPO SIKU CCM KITAKUMBATIA MATAJIRI NA WANANCHI MASKINI WATANUNULIWA KUKIINGIZA IKULU?JE HAJATIMIA.LET US WAIT,ITS A MATTER OF TIME,THEREFORE time will tell.
 
Ni ndoto za mchana/ slaa alijidai oh kikwete hata fika 2015. Sasa kuna kila dalili yeye ndiye hatafika 2015. Chadema kinakufa, hii propaganda ya kuchukua nchi ni kelele za kujifariji ya moyoni chadema wanayo. Hakuna mkao wa kuchukua nchi. Ukiangalia safu ya viongozi unatamani ujifiche uvunguni. Linganisha hiyo safu na kina mwakyembe muhongo, magufuli kagasheki tibaijuka hahahahaha poleni msaidieni raila kulia
 
Polisi wetu wamekalia kupiga waendesha bodaboda Kawe. Wanamwacha Mwampamba ambaye amekiri wazi kuujua mpango uliopelekea kuuawa kwa muuza magazeti wa Morogoro!
 
Wenye upeo wa kuona karibu watapingana na wazo hili lakini huo ndiyo ukweli, kuelekea uchaguzi wa 2015 CCM itakuwa hoi kabisa.

Zipo sababu nyingi baadhi ya sababu zitakazosababisha chama hicho kufa ni hizi hapa:-

1. Katika historia ya CCM ni kipindi cha miaka ya hivi karibuni kimekuwa kikitumia nguvu nyingi mno kupita kiasi na mara nyingine wametumia vyombo vya usalama kukinusuru

2. Chama cha Mapinduzi kupitia serikali yake kimeshindwa kutekeleza ahadi zake zilizotolewa mwaka 2010 wakati wa kampeni angalau kwa asilimia 40, ikumbukwe uchaguzi ni mwaka kesho kutwa

3. Kauli ya maisha bora kwa kila mtanzania kwa kipindi hiki imegeuka kuwa kero kwa Watanzani kila wanapoisikia
4.Najua kuelekea uchaguzi 2015, wasaliti na wanafiki wa CCJ Mwakyembe, Sitta na Nape akipita Mbabe wao Edward Lowassa ambaye walisema ni fisadi na sasa wamegeuka wanasema ni msafi, wataikimbia ccm na kurudi ccj
5. Watanzania waliowengi kwa sasa hawaoni mtu yoyote bkutoka chama hicho kama anaweza kupewa dhamana ya kuongoza Nchi hii, labda pekee walio katika usingizi yaani hawahelewi nchi ilikotoka tangu enzi za Mwalimu muasis wa Taifa hili, ilipo na itakapokuwa kwa miaka ijayo endapo ccm wataendelea kuipa dhamana ya kuongoza nchi hii
6. Mpasuko wa umoja wa kitaifa , leo hii tunasikia sakata la nani achinje nyama, sumu hiyo ya udini imeasisiwa na ccm, na hapo hakuna cha kujitetea . Hilo jambo linawakera wengi na ni miongoni mwa sababu zitakazosababisha ccm kufa kuelekea 2015
7. Siasa zinazoendeshwa na ccm kwa sasa sio za kistaarabu ni za kihuni , fitina , hujuma na chuki zidi ya vyama pinzania, watanzania wamechoka hawataki tena siasa za namna hiyo, wanataka hoja na si vinginevyo
8. Ufisadi uliokithiri kwa baadhi ya watanzania wenzetu tuliowaamini tukawapa dhamana na sasa wanatugeuka na kama si kutugeuka basi wanatutafuna, pengo kati ya wenye nacho na wasiokuwa nacho ni kubwa mno
9. Serikali iliyopo kwa sasa ya ccm inaonekana kuwa legelege mno haimanishi kuwatumikia watanzania kwa moyo wa dhati, watanzania wamegundua hilo na wamehamua kukipumzisha ccm na kujaribu vyama vingine vya upinzani


Nawasilisha
 
Mkuu, hoja zoka ni za msingi;hata hivyo,nimejikuta nacheka kwani umewapiga madongo mazito na ya ukweli mtupu!
 
Back
Top Bottom