Salim A. Msangi
JF-Expert Member
- Apr 26, 2011
- 566
- 511
- Thread starter
- #61
Kiongozi ninacho fanya ni utafiti binafsi, ndiyo maana kwenye kazi zangu nyingi utaoana naweka vyanzo vya taarifa ambacho ndicho kitu muhimu kwenye kazi yoyote ya kitafiti, na vyanzo ninavyo weka nahakikisha ni vya uhakika,wewe sasa msomaji kama inakuap mushkeli inabidi uje na hoja zako pia useme hichi si kweli kwa sababu kadha, kadha, hichi ndicho kwa sababu hii na hii, vinginevyo itakuwa ni maoni binfsi tu.Huko sasa ndio kushiriki kwenyewe. Sasa lipo tukio ambalo ameshawahi kuamrisha watu wake wafanye ?
Inaonekana haya mambo hayaeleweki na yamejengeka katika misingi ya uongo. Sasa je ushawahi kulipima hili jambo kwa mizani ya Uislamu ukajua uislamu unasemaje kuhusu kusambaza au kuelezea habari ambazo huwezi kuthibitisha juu ya ukweli wake ?
Ushawahi kuzihakiki hizo taarifa ukajua ni kweli zinatolewa na kiongozi ?
Unaonaje kama ungetumia muda wa kuhakiki ukweli wa jambo hili na kuweza kulithibitisha kisha ukatuwekea na ukazipima habari zako kwa mizani ya Uislamu,ingekuwa bora kwako.