Kifahamu chumba kiitwacho Room 39 kipo Korea Kaskazini. Majasusi wote hatari hutoka humo Inasadikiwa kinaendeshwa na Kim Yo-jong dada yake Kim Jong-un

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
Nilipokuwa nikisoma kuhusu dada yake kiongozi wa Korea Kaskazini aitwae Kim Yo-jong nikapata kidogo ufahamu wa chumba kiitwacho Room 39 ambacho inasadikiwa kuwa mume wake dada huyo aitwae Choe Song ambae ni mtoto wa mtumishi wa serikali Chong Ryong-hae nae anafanya kazi ndani ya chumba hicho.

Chumba hiki kina majina mengi kadhaa kama vile Bureau au Kitengo, Division au sehemu au pia Office 39.

Chumba hiki kipo ndani ya jengo la chama cha wafanyakazi wa Korea kaskazini jengo ambalo halipo mbali na makazi rasmi ya kiongozi wa Korea Kaskazini bwana Kim Jong-un.

Lakini kiukweli hiki ni kitengo maalum cha kijasusi ambacho kinafanya kazi zake ndani ya chama cha wafanyakazi wa Korea Kaskazni ambacho kina jukumu moja tu, kuhakikisha viongozi wa Korea Kaskazini wana fedha za kigeni za matumizi wakiwa nje ya nchi hiyo.

Room 39 kipo chini ya usimamizi wa kamati kuu ya chama hicho lakini upande wa kamati ya kijeshi ambayo ina majukumu ya kupitisha matumizi ya fedha kwa jeshi kwenye ununuzi wa silaha na usimamzi wa maliasili za nchi hiyo madini yakiwemo.

Inakisiwa kuwa kitengo hicho kinaingiza kati ya dola milioni 500 hadi bilioni 1 au zaidi kwa mwaka, na fedha hizo ni kutokana na biashara za aina zote tunazozifahamu duniani zikiwemo halali na haramu.

Ukiangalia kazi za kitengo hiki waweza kukifananisha kwa mbali na jeshi maalum la Iran la IRGC ambalo pia linajitegemea na linahisiwa kuingiza kiasi cha dola hadi bilioni 12 kwa mwaka zinatotokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Tofauti iliyopo kidogo ni kwamba Chumba 39 au Room 39 kimejikita zaidi kwenye ujasusi wa nje ya Korea Kaskazini na kinaratibu ofisi na makampuni mbalimbali ndani na nje ya Korea Kaskazini huku wakibadilisha majina mara kwa mara.

Mfano wa makampuni mbalimbali yanayoendesha shughuli zake nje ya Korea Kaskazini ni migahawa iitwayo Pyongyang ambayo ipo sehemu mbalimbali duniani.

Kampuni ingine ni ile ya KNIC ambayo inashughulika na masuala ya bima na ina ofisi katika miji ya Hamburg nchini Ujerumani na London nchini Uingereza. Mwaka 2015 umoja wa Ulaya uliwahi kuifungia kampuni hii kutokana na kujishughulisha na biashara haramu na bima bandia na kujipatia fedha kutokana na kudai bima hewa.

Chumba 39 kilianzishwa kwenye miaka ya 70 na Kim II Sung ambae ni babu yake Kim Jong-un na kukabidhiwa majukumu ya kuhakikisha utawala wa Korea kaskazini huishiwi fedha za kujiendesha pamoja na usimamizi wa uchumi wa nchi hiyo.

Mahali kilipoanzia shughuli zake ni chumba kilichoitwa Office 39 na baadae kubatiza chumba hichi jina la Room 39 kikiwa nyuma ya chumba kingine kiitwacho room 36 ambacho kazi yake kubwa ni kusimamia fedha za utawala wa Korea Kakazini.

Chumba hiki kina shughuli nyingi na kimesheheni majasusi wenye taaluma zote muhimu wakiwemo wakemia ambao hudaiwa kutengeneza madawa mbalimbali na kuyauza nchini China, Japan na sehemu zingine barani Asia.

Pia majasusi wakemia wa chumba 39 wanasadikiwa kutengeneza dawa za kuongeza nguvu za kiume maarufu kama Viagra zenye vimelea mbalimbali kwenye viwanda vyake vilivyoko sehemu iitwayo Chonglin na kuuza kwenye nchi za Hong Kong, China na Mashariki ya kati.

Kitengo hiki pia kina wataalam wa masuala ya fedha na watengenezaji noti bandia ziitwazo "Supernotes" ambazo huonekana kama fedha halali kwa matumizi na huwa na thamani ya hadi dola milioni 100.

Kitengo hiki cha kipekee pia hutengeneza bidhaa ambazo baadae huwekwa nembo ya bidhaa za China na kupitishwa na kufanikiwa kufika kwenye masoko ya kimataifa kwenye nchi kama za Ufaransa, Italia na Korea Kusini.

Bidhaa hizo ni pamoja na Eyelashes (kalamu ya urembo wa kope za macho), vifaa vya muziki na sigara ambavyo kwa pamoja vinasadikiwa kuiingizia nchi hiyo dola milioni 120 kwa mwaka.

Kwa upande wa mauzo ya silaha nchi hiyo iliwekewa vikwazo kwenye uuzajiw a silaha zake lakini chumba namba 39 kikafanikwia na mwaka 2014 silaha za Korea kaskazini ziliuzwa kwa kutumia makampuni yake yenye majna halali kwa nchi za Syria, Myanmar, Eritrea, Tanzania, Ethiopia, Somalia na Iran.

Kitengo hiki pia mwaka 2016 kwa kutumia majasusi wake wataalam wa teknolojia walifanikiwa kudukua hazina ya New York iitwayo Federal Reserve na kuchukua kiasi cha dola bilioni 1.

Majasusi wa Marekani walipokuwa wakifuatilia wizi huo walikuja kugundua kasoro ya maandishi kwenye makaratasi ya kuombea kufanya mialama na ndipo walipogundua kasoro kwenye neno Foundation lililoandikwa "fandation" ndipo walipobaini kuwa wakorea kaskazini ndio walofanya uharibifu.

Itakumbukwa kuwa mwaka huohuo wa 2016 ndio mwaka ambao kulitokea kirusi cha kompyuta cha "Wannacry" ambacho kilivamia mifumo mbalimbali ya kompyuta duniani.

Pia majasusi hao wa Room 39 waliweza kuingiza kwenye mifumo ya ulinzi wa anga ya Korea Kusini na kufanikiwa kuiba ndege za kivita na kisha kuzirusha na kuzitua salama nchini Korea Kaskazini na zisipatikane hadi leo.

Nchi nyingi zilizoendelea kwa sasa zimeamua kuwekeza kwenye utaalam wa masuala ya mitandao uitwao Cyber Security kwani inasadikiwa kuwa chumba namba 39 kina majasusi wengi walopikwa tayari kushambulia nchi yoyote ile duniani.

Ama hakika chumba hiki kiitwacho Room 39 ni chumba hatari kuwahi kutokea duniani na hivi karibuni na kuendelea tuzidi kusikiliza kauli zinazotoka kwa utawala wa PyongYang khasa dada yake Kim Jong-un aitwae Kim Yo-jong ambae kiufundi anaonekana ndie kamanda wa Room 39.

Hii inaweza kumfanya aonekane kuwa ni mwanamke hatari zaidi kuwahi kutokea duniani.

NB: Ombi kwa MOds msiuunganishe uzi huu.

Karibu.
 
Habari za kusadikika from N.k wewe unazijua i wonder

Mara nyingi "defectors" ndo watoaji wa hizi habari ila inahitaji muda kuwasikiliza ingawa hutoa madini muhimu sana kuhusu Korea Kaskazini.

Ila sasa hivi hawa defectors wanatolewa vitisho vya mara kwa mara kwa kuuza taarifa za Korea Kaskazini kwa maadui hususan Korea Kusini.

Kama juzi tu huyu mwanamke ametoa onyo kali kwa defectors.
 
NIlipokuwa nikisoma kuhusu dada yake kiongozi wa Korea Kaskazini aitwae Kim Yo-jong nikapata kidogo ufahamu wa chumba kiitwacho Room 39 ambacho inasadikiwa kuwa mume wake dada huyo aitwae Chong Ryong-hae anafanya kazi ndani ya chumba hicho.

Chumba hiki kina majina mengi kadhaa kama vile Bureau au Kitengo, Division au sehemu au pia Office 39.

Chumba hiki kipo ndani ya jengo la chama cha wafanyakazi wa Korea kaskazini jengo ambalo halipo mbali na makazi rasmi ya kiongozi wa Korea Kaskazini bwana Kim Jong-un.

Lakini kiukweli hiki ni kitengo maalum cha kijasusi ambacho kinafanya kazi zake ndani ya chama cha wafanyakazi wa Korea Kaskazni ambacho kina jukumu moja tu, kuhakikisha viongozi wa Korea Kaskazini wana fedha za kigeni za matumizi wakiwa nje ya nchi hiyo.

Room 39 kipo chini ya usimamizi wa kamati kuu ya chama hicho lakini upande wa kamati ya kijeshi ambayo ina majukumu ya kupitisha matumizi ya fedha kwa jeshi kwenye ununuzi wa silaha na usimamzi wa maliasili za nchi hiyo madini yakiwemo.

Inakisiwa kuwa kitengo hicho kinaingiza kati ya dola milioni 500 hadi bilioni 1 au zaidi kwa mwaka, na fedha hizo ni kutokana na biashara za aina zote tunazozifahamu duniani zikiwemo halali na haramu.

Ukiangalia kazi za kitengo hiki waweza kukifananisha kwa mbali na jeshi maalum la Iran la IRGC ambalo pia linajitegemea na linahisiwa kuingiza kiasi cha dola hadi bilioni 12 kwa mwaka zinatotokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Tofauti iliyopo kidogo ni kwamba Chumba 39 au Room 39 kimejikita zaidi kwenye ujasusi wa nje ya Korea Kaskazini na kinaratibu ofisi na makampuni mbalimbali ndani na nje ya Korea Kaskazini huku wakibadilisha majina mara kwa mara.

Mfano wa makampuni mbalimbali yanayoendesha shughuli zake nje ya Korea Kaskazini ni migahawa iitwayo Pyongyang ambayo ipo sehemu mbalimbali duniani.

Kampuni ingine ni ile ya KNIC ambayo inashughulika na masuala ya bima na ina ofisi katika miji ya Hamburg nchini Ujerumani na London nchini Uingereza. Mwaka 2015 umoja wa Ulaya uliwahi kuifungia kampuni hii kutokana na kujishughulisha na biashara haramu na bima bandia na kujipatia fedha kutokana na kudai bima hewa.

Chumba 39 kilianzishwa kwenye miaka ya 70 na Kim II Sung ambae ni babu yake Kim Jong-un na kukabidhiwa majukumu ya kuhakikisha utawala wa Korea kaskazini huishiwi fedha za kujiendesha pamoja na usimamizi wa uchumi wa nchi hiyo.

Mahali kilipoanzia shughuli zake ni chumba kilichoitwa Office 39 na baadae kubatiza chumba hichi jina la Room 39 kikiwa nyuma ya chumba kingine kiitwacho room 36 ambacho kazi yake kubwa ni kusimamia fedha za utawala wa Korea Kakazini.

Chumba hiki kina shughuli nyingi na kimesheheni majasusi wenye taaluma zote muhimu wakiwemo wakemia ambao hudaiwa kutengeneza madawa mbalimbali na kuyauza nchini China, Japan na sehemu zingine barani Asia.

Pia majasusi wakemia wa chumba 39 wanasadikiwa kutengeneza dawa za kuongeza nguvu za kiume maarufu kama Viagra zenye vimelea mbalimbali kwenye viwanda vyake vilivyoko sehemu iitwayo Chonglin na kuuza kwenye nchi za Hong Kong, China na Mashariki ya kati.

Kitengo hiki pia kina wataalam wa masuala ya fedha na watengenezaji noti bandia ziitwazo "Supernotes" ambazo huonekana kama fedha halali kwa matumizi na huwa na thamani ya hadi dola milioni 100.

Kitengo hiki cha kipekee pia hutengeneza bidhaa ambazo baadae huwekwa nembo ya bidhaa za China na kupitishwa na kufanikiwa kufika kwenye masoko ya kimataifa kwenye nchi kama za Ufaransa, Italia na Korea Kusini.

Bidhaa hizo ni pamoja na Eyelashes (kalamu ya urembo wa kope za macho), vifaa vya muziki na sigara ambavyo kwa pamoja vinasadikiwa kuiingizia nchi hiyo dola milioni 120 kwa mwaka.

Kwa upande wa mauzo ya silaha nchi hiyo iliwekewa vikwazo kwenye uuzajiw a silaha zake lakini chumba namba 39 kikafanikwia na mwaka 2014 silaha za Korea kaskazini ziliuzwa kwa kutumia makampuni yake yenye majna halali kwa nchi za Syria, Myanmar, Eritrea, Tanzania, Ethiopia, Somalia na Iran.

Kitengo hiki pia mwaka 2016 kwa kutumia majasusi wake wataalam wa teknolojia walifanikiwa kudukua hazina ya New York iitwayo Federal Reserve na kuchukua kiasi cha dola bilioni 1.

Majasusi wa Marekani walipokuwa wakifuatilia wizi huo walikuja kugundua kasoro ya maandishi kwenye makaratasi ya kuombea kufanya mialama na ndipo walipogundua kasoro kwenye neno Foundation lililoandikwa "fandation" ndipo walipobaini kuwa wakorea kaskazini ndio walofanya uharibifu.

Itakumbukwa kuwa mwaka huohuo wa 2016 ndio mwaka ambao kulitokea kirusi cha kompyuta cha "Wannacry" ambacho kilivamia mifumo mbalimbali ya kompyuta duniani.

Pia majasusi hao wa Room 39 waliweza kuingiza kwenye mifumo ya ulinzi wa anga ya Korea Kusini na kufanikiwa kuiba ndege za kivita na kisha kuzirusha na kuzitua salama nchini Korea Kaskazini na zisipatikane hadi leo.

Nchi nyingi zilizoendelea kwa sasa zimeamua kuwekeza kwenye utaalam wa masuala ya mitandao uitwao Cyber Security kwani inasadikiwa kuwa chumba namba 39 kina majasusi wengi walopikwa tayari kushambulia nchi yoyote ile duniani.

Ama hakika chumba hiki kiitwacho Room 39 ni chumba hatari kuwahi kutokea duniani na hivi karibuni na kuendelea tuzidi kusikiliza kauli zinazotoka kwa utawala wa PyongYang khasa dada yake Kim Jong-un aitwae Kim Yo-jong ambae kiufundi anaonekana ndie kamanda wa Room 39.

Hii inaweza kumfanya aonekane kuwa ni mwanamke hatari zaidi kuwahi kutokea duniani.

NB: Ombi kwa MOds msiuunganishe uzi huu.

Karibu.
SAWASAWA
 
Wabongo hamna kitu hamjui ila kwa Magu mmegonga mwamba mnahanya tu
We can't breath
Eai5CelWAAISpUV.jpg
 
NIlipokuwa nikisoma kuhusu dada yake kiongozi wa Korea Kaskazini aitwae Kim Yo-jong nikapata kidogo ufahamu wa chumba kiitwacho Room 39 ambacho inasadikiwa kuwa mume wake dada huyo aitwae Chong Ryong-hae anafanya kazi ndani ya chumba hicho.

Chumba hiki kina majina mengi kadhaa kama vile Bureau au Kitengo, Division au sehemu au pia Office 39.

Chumba hiki kipo ndani ya jengo la chama cha wafanyakazi wa Korea kaskazini jengo ambalo halipo mbali na makazi rasmi ya kiongozi wa Korea Kaskazini bwana Kim Jong-un.

Lakini kiukweli hiki ni kitengo maalum cha kijasusi ambacho kinafanya kazi zake ndani ya chama cha wafanyakazi wa Korea Kaskazni ambacho kina jukumu moja tu, kuhakikisha viongozi wa Korea Kaskazini wana fedha za kigeni za matumizi wakiwa nje ya nchi hiyo.

Room 39 kipo chini ya usimamizi wa kamati kuu ya chama hicho lakini upande wa kamati ya kijeshi ambayo ina majukumu ya kupitisha matumizi ya fedha kwa jeshi kwenye ununuzi wa silaha na usimamzi wa maliasili za nchi hiyo madini yakiwemo.

Inakisiwa kuwa kitengo hicho kinaingiza kati ya dola milioni 500 hadi bilioni 1 au zaidi kwa mwaka, na fedha hizo ni kutokana na biashara za aina zote tunazozifahamu duniani zikiwemo halali na haramu.

Ukiangalia kazi za kitengo hiki waweza kukifananisha kwa mbali na jeshi maalum la Iran la IRGC ambalo pia linajitegemea na linahisiwa kuingiza kiasi cha dola hadi bilioni 12 kwa mwaka zinatotokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Tofauti iliyopo kidogo ni kwamba Chumba 39 au Room 39 kimejikita zaidi kwenye ujasusi wa nje ya Korea Kaskazini na kinaratibu ofisi na makampuni mbalimbali ndani na nje ya Korea Kaskazini huku wakibadilisha majina mara kwa mara.

Mfano wa makampuni mbalimbali yanayoendesha shughuli zake nje ya Korea Kaskazini ni migahawa iitwayo Pyongyang ambayo ipo sehemu mbalimbali duniani.

Kampuni ingine ni ile ya KNIC ambayo inashughulika na masuala ya bima na ina ofisi katika miji ya Hamburg nchini Ujerumani na London nchini Uingereza. Mwaka 2015 umoja wa Ulaya uliwahi kuifungia kampuni hii kutokana na kujishughulisha na biashara haramu na bima bandia na kujipatia fedha kutokana na kudai bima hewa.

Chumba 39 kilianzishwa kwenye miaka ya 70 na Kim II Sung ambae ni babu yake Kim Jong-un na kukabidhiwa majukumu ya kuhakikisha utawala wa Korea kaskazini huishiwi fedha za kujiendesha pamoja na usimamizi wa uchumi wa nchi hiyo.

Mahali kilipoanzia shughuli zake ni chumba kilichoitwa Office 39 na baadae kubatiza chumba hichi jina la Room 39 kikiwa nyuma ya chumba kingine kiitwacho room 36 ambacho kazi yake kubwa ni kusimamia fedha za utawala wa Korea Kakazini.

Chumba hiki kina shughuli nyingi na kimesheheni majasusi wenye taaluma zote muhimu wakiwemo wakemia ambao hudaiwa kutengeneza madawa mbalimbali na kuyauza nchini China, Japan na sehemu zingine barani Asia.

Pia majasusi wakemia wa chumba 39 wanasadikiwa kutengeneza dawa za kuongeza nguvu za kiume maarufu kama Viagra zenye vimelea mbalimbali kwenye viwanda vyake vilivyoko sehemu iitwayo Chonglin na kuuza kwenye nchi za Hong Kong, China na Mashariki ya kati.

Kitengo hiki pia kina wataalam wa masuala ya fedha na watengenezaji noti bandia ziitwazo "Supernotes" ambazo huonekana kama fedha halali kwa matumizi na huwa na thamani ya hadi dola milioni 100.

Kitengo hiki cha kipekee pia hutengeneza bidhaa ambazo baadae huwekwa nembo ya bidhaa za China na kupitishwa na kufanikiwa kufika kwenye masoko ya kimataifa kwenye nchi kama za Ufaransa, Italia na Korea Kusini.

Bidhaa hizo ni pamoja na Eyelashes (kalamu ya urembo wa kope za macho), vifaa vya muziki na sigara ambavyo kwa pamoja vinasadikiwa kuiingizia nchi hiyo dola milioni 120 kwa mwaka.

Kwa upande wa mauzo ya silaha nchi hiyo iliwekewa vikwazo kwenye uuzajiw a silaha zake lakini chumba namba 39 kikafanikwia na mwaka 2014 silaha za Korea kaskazini ziliuzwa kwa kutumia makampuni yake yenye majna halali kwa nchi za Syria, Myanmar, Eritrea, Tanzania, Ethiopia, Somalia na Iran.

Kitengo hiki pia mwaka 2016 kwa kutumia majasusi wake wataalam wa teknolojia walifanikiwa kudukua hazina ya New York iitwayo Federal Reserve na kuchukua kiasi cha dola bilioni 1.

Majasusi wa Marekani walipokuwa wakifuatilia wizi huo walikuja kugundua kasoro ya maandishi kwenye makaratasi ya kuombea kufanya mialama na ndipo walipogundua kasoro kwenye neno Foundation lililoandikwa "fandation" ndipo walipobaini kuwa wakorea kaskazini ndio walofanya uharibifu.

Itakumbukwa kuwa mwaka huohuo wa 2016 ndio mwaka ambao kulitokea kirusi cha kompyuta cha "Wannacry" ambacho kilivamia mifumo mbalimbali ya kompyuta duniani.

Pia majasusi hao wa Room 39 waliweza kuingiza kwenye mifumo ya ulinzi wa anga ya Korea Kusini na kufanikiwa kuiba ndege za kivita na kisha kuzirusha na kuzitua salama nchini Korea Kaskazini na zisipatikane hadi leo.

Nchi nyingi zilizoendelea kwa sasa zimeamua kuwekeza kwenye utaalam wa masuala ya mitandao uitwao Cyber Security kwani inasadikiwa kuwa chumba namba 39 kina majasusi wengi walopikwa tayari kushambulia nchi yoyote ile duniani.

Ama hakika chumba hiki kiitwacho Room 39 ni chumba hatari kuwahi kutokea duniani na hivi karibuni na kuendelea tuzidi kusikiliza kauli zinazotoka kwa utawala wa PyongYang khasa dada yake Kim Jong-un aitwae Kim Yo-jong ambae kiufundi anaonekana ndie kamanda wa Room 39.

Hii inaweza kumfanya aonekane kuwa ni mwanamke hatari zaidi kuwahi kutokea duniani.

NB: Ombi kwa MOds msiuunganishe uzi huu.

Karibu.
Hicho sio chumba sasa.ni godown kabisa
 
Back
Top Bottom