Kielelezo kingine cha udikteta aliouacha Hayati Magufuli ni kuua media kabisa

Kabla ya kuingia kwenye mchakato wa katiba lazima kuwe na majadiliano na makubaliano ya awali(preminary discussions and agreement/ consensus on basic principles of ought to) kuhusu misingi ya kitaifa ambayo haiwezi kubadilishwa na katiba mpya maana yake unaua taifa la Tanzania i.e muundo wa muungano. Haya mambo bila kupata makubaliano ya awali kitaifa hapo hapatakuwa na a way forward kwenye jambo hili. Tanzania ni tofauti na Kenya, Uganda, S.A na nchi nyingi za Afrika kimuundo, desturi, maslahi, na utamaduni wake, kwa namna yoyote lazima kuingia kwenye duru hii inahitaji umahiri na siyo porojo za wanasiasa wenye mlengo wa kusambaratisha taifa kiaina.

Hayo yanaweza kubakia kama yana maana kwa hivyo, lakini katiba mpya ni lazima. Na hakuna mjadala wowote wa maana utafanyika kwenye hilo, maana hakuna uwanja wa mijadala ya hivyo kwenye nchi hii, zaidi ya vikao vya vyama vya siasa. Ni hivi mjadala wa katiba mpya ni wawana siasa, hizi porojo za wananchi wote, sijui mjadala ya kitaifa ni porojo tu.
 
Kesho ni katiba day na katiba hakuna mtu yeyote ambaye hana maslahi nayo.

Waandishi wa habari kama Mwangosi na Azuory Gwanda waliuwawa kwa sababu ya katiba mbovu na mpaka leo hatujawai kuona wanasiasa waliosababisha wakiwajibishwa.

Watu kama wakina Ngurumo wamekimbia nchi mpaka leo kwa sababu ya habari zao za kiuchunguzi kutotakiwa na tawala za ccm.

Awamu ya Magufuli waandishi mpaka walipigwa viboko na kuwekwa ndani

Utawala wa Magufuli vyombo vya habari vilifungwa na kupewa faini kubwa kubwa kwa sababu ya katiba na sheria mbovu.

Lakini leo watu wanaanzisha katiba movement Ila cha kushangaza hakuna hata media moja inayosaport movement hiyo!!.

Cha kushangaza siku Samia akitangaza kukubali katiba media zitaandika kumpongeza bila kuwapongeza walio anzisha movement hii

Bongo hatuna media kabisa!!

Inasikitisha Sana.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tungekuwa na katiba nzuri inayotambua na kulinda haki za raia, hata wewe huenda ungepata elimu nzuri ambayo ingepunguza au kufuta uwendawazimu wako ambao unao sasa hivi.
Nakushauri hiyo mimba toa
 
Subiri uone kama kuna huo ujinga wa katiba

Haikwepeki hata mfanyeje, labda kama hoja hiyo isingekuwa imeshikiwa bango na cdm. Hapo ndio utajua kuwa kuna chama cha watu, na chama cha vyombo vya dola.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Bongo hatuna media kabisa!!
Hivi unategemea akina Bakile, Meena, Ruyungu, n.k walivyo na njaa kali Wana ubavu wa kuandika kinacho muudhi mama?? Wanajikomba kwa mama ili wapate kupewa japo uDAS, ama uDED.

Uteuzi wa waandishi wa habari ndiyo umeuwa akili zao kabisa. Kila mtu anajipendekeza.

Balile alitumia dakika 4:56 kuomba safari za nje, stimulus package, matangazo ya serikali, na malipo ya madeni. Bure kabisa!!!
 
Kesho ni katiba day na katiba hakuna mtu yeyote ambaye hana maslahi nayo.

Waandishi wa habari kama Mwangosi na Azuory Gwanda waliuwawa kwa sababu ya katiba mbovu na mpaka leo hatujawai kuona wanasiasa waliosababisha wakiwajibishwa.

Watu kama wakina Ngurumo wamekimbia nchi mpaka leo kwa sababu ya habari zao za kiuchunguzi kutotakiwa na tawala za ccm.

Awamu ya Magufuli waandishi mpaka walipigwa viboko na kuwekwa ndani

Utawala wa Magufuli vyombo vya habari vilifungwa na kupewa faini kubwa kubwa kwa sababu ya katiba na sheria mbovu.

Lakini leo watu wanaanzisha katiba movement Ila cha kushangaza hakuna hata media moja inayosaport movement hiyo!!.

Cha kushangaza siku Samia akitangaza kukubali katiba media zitaandika kumpongeza bila kuwapongeza walio anzisha movement hii

Bongo hatuna media kabisa!!
Katiba ndo nchi.
 
Ila magu alijisahau Sana.... Kumbe mtu a natumia moyo wa luku afu akawa kama hatakufa...
 
Haikwepeki hata mfanyeje, labda kama hoja hiyo isingekuwa imeshikiwa bango na cdm. Hapo ndio utajua kuwa kuna chama cha watu, na chama cha vyombo vya dola.
Kwa vile imeshikiwa bango na chadema ndio itaandikwa upya?

Niambie movement gani mliwahi kushikia bango mkafanikiwa?

Mkuu unakuwa kama mmawia na wewe?

Hizi kelele zenu za katiba kwani zimeanza mwaka huu?
 
Hivi unategemea akina Bakile, Meena, Ruyungu, n.k walivyo na njaa kali Wana ubavu wa kuandika kinacho muudhi mama?? Wanajikomba kwa mama ili wapate kupewa japo uDAS, ama uDED.

Uteuzi wa waandishi wa habari ndiyo umeuwa akili zao kabisa. Kila mtu anajipendekeza.

Balile alitumia dakika 4:56 kuomba safari za nje, stimulus package, matangazo ya serikali, na malipo ya madeni. Bure kabisa!!!
Si mlikuwa mnashangilia kuteuliwa kwao mkisema anawakomesha mataga?

Tukiwambia ccm kuna vichwa mnabisha! Kila move wanayofanya huwa wana calculate mile zaidi ya milioni mbele
 
Hakuna mtu muovu kama Dk. Hassan Abbas. Yan yule inatakiwa amfuate jamaa haraka sana
 
Je, mtakubali maoni ya upande mwingine? Kilichoshindikana katika michakato iliyopita ni pande mbili kutokukubaliana, sidhani kama kitakuwa tofauti hivi sasa.
Rasimu ya katiba ipo tayari, ni kupigiwa kura tu ya ndio au hapana ili itumike au isitumike
 
Kwa vile imeshikiwa bango na chadema ndio itaandikwa upya?

Niambie movement gani mliwahi kushikia bango mkafanikiwa?

Mkuu unakuwa kama mmawia na wewe?

Hizi kelele zenu za katiba kwani zimeanza mwaka huu?

Kwa taarifa yako kuna katiba pendekezwa hadi tunavyoongea, na haikuanzishwa na ccm. Na sasa ni lazima muelekee kibla taka msitake.
 
Kwa taarifa yako kuna katiba pendekezwa hadi tunavyoongea, na haikuanzishwa na ccm. Na sasa ni lazima muelekee kibla taka msitake.
Ilianzishwa na chadema?

Ok, ikawa sasa ikabaki kuwa pendekezwa tu?

Vipi nipe picha za huko tabata mkuu!
 
Ilianzishwa na chadema?

Ok, ikawa sasa ikabaki kuwa pendekezwa tu?

Vipi nipe picha za huko tabata mkuu!
Ni lini ccm iliwahi kuwa na agenda ya katiba mpya? Kilichopelekea kuandika katiba mpya ndio hicho hicho kitasukuma hilo kwa sasa.

Ya huko tabata bado sijayajua maana siko Dar wiki hii, niko navuma maharage tu huku porini.
 
Kesho ni Katiba day na katiba hakuna mtu yeyote ambaye hana maslahi nayo.

Waandishi wa habari kama Mwangosi na Azory Gwanda waliuawa kwa sababu ya katiba mbovu na mpaka leo hatujawai kuona wanasiasa waliosababisha wakiwajibishwa.

Watu kama wakina Ngurumo wamekimbia nchi mpaka leo kwa sababu ya habari zao za kiuchunguzi kutotakiwa na tawala za ccm.

Awamu ya Magufuli waandishi mpaka walipigwa viboko na kuwekwa ndani

Utawala wa Magufuli vyombo vya habari vilifungwa na kupewa faini kubwa kubwa kwa sababu ya katiba na sheria mbovu.

Lakini leo watu wanaanzisha katiba movement Ila cha kushangaza hakuna hata media moja inayosaport movement hiyo!!.

Cha kushangaza siku Samia akitangaza kukubali katiba media zitaandika kumpongeza bila kuwapongeza walio anzisha movement hii

Bongo hatuna media kabisa.
Vyombo vyote ni vya makada wa CCM
 
Ni lini ccm iliwahi kuwa na agenda ya katiba mpya? Kilichopelekea kuandika katiba mpya ndio hicho hicho kitasukuma hilo kwa sasa.

Ya huko tabata bado sijayajua maana siko Dar wiki hii, niko navuma maharage tu huku porini.
Safi sana!
.
Kumbe wewe uko porini una vuna maharage una akili sana kuliko hawa bavicha wanaosubiri siku Lisu awe rais awape maisha mazuri
 
Safi sana!
.
Kumbe wewe uko porini una vuna maharage una akili sana kuliko hawa bavicha wanaosubiri siku Lisu awe rais awape maisha mazuri

Bora ningebaki huko huko Dar, huku natoa somo la katiba mpya kama sina akili nzuri. Cha ajabu kabisa nimekuta huku wananchi wana uelewa wa mambo kwa kiwango cha kutosha. Yaani wananieleza ule uhuni wa uchaguzi mkuu uliopita A-Z. Nimefarijika kuona wale ccm inaotambia kuwa ni mtaji, wako mbele kuliko ccm inavyodhania. Kwa sasa vyombo vya dola ndio silaha pekee ya ccm kukaa madarakani.
 
Back
Top Bottom