Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,422
- 24,432
- Thread starter
- #61
Kuna ukweli, sometimes lugha na hata matendo yaliyokuwa yakifanywa na mheshimiwa yule yalikuwa yana tia hofu na hata kuwa kero kubwa kwa jamii.Huyo kiongozi alianza kujitupia takataka mwenyewe tangu alivyokuwa hai.
Kawapa urahisi hawa wa sasa kumtumia yeye kama chaka lao tu.
Yani kiongozi aongee maneno mbovumbovu waziwazi na kujichafua mwenyewe mchana kweupe tunamuona halafu mnategemea akifa asitupiwe takataka kweli?
Ujinga gani huo?
Wasiojulikana
Kodi hewa
Kughushiwa mashtaka kubambikwa
Kunyang'anywa mali kwa nguvu
Kuna "waliopotea"
Ukabila(Sukuma Gang)-watu tunaanza kusahau
Lakini vile vile kuna aliyofanya vema
Vituo vya afya
Barabara
Ndege(ingawaje zipo mbovu)
SGR-hata kama haijakamilika
Bwawa la umeme JNHEPP-Stiglaz
Jukumu letu ni kupembua jema na baya lake.
Lakini kula na kunywa(ufisadi) na kutupia takataka kaburini?