nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,860
- 5,803
MKUU wa Wilaya ya Ilemela Jijini Mwanza, Serenge Mrenge, amefariki nchini India alikokuwa akitibiwa maradhi yaliyokuwa yakimsumbua.
Kifo cha mkuu huyo wa wilaya ya Ilemela kimetokea juzi nchini India ambapo alikuwa akitibiwa ugonjwa wa tumbo uliokuwa ukimtatiza kwa kipindi kirefu sasa.
Akithibitisha jana kifo hicho, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro, aliiambia Tanzania Daima: DC Mrenge amefariki jana (juzi), nchini India, alikokuwa akipatiwa huduma za kitabibu za ugonjwa wa tumbo uliokuwa ukimsumbua.
RC Kandoro alisema mkuu huyo wa wilaya ya Ilemela alipelekwa nje ya nchi zaidi ya wiki tatu zilizopita, baada ya Hospitali ya Rufaa ya Bugando ya jijini Mwanza, kushindwa kumtibu na kutoa kibali cha kupelekwa nchini India kwa matibabu ya tumbo ambapo mauti yamemkua huko.
Kifo cha mkuu huyo wa wilaya kimekuja miezi michache baada ya mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, Creophat Rugarabamu, kufariki nchini India alikopelekwa kwa matibabu ya shinikizo la damu.
Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Mwanza, mwili wa marehemu Mrenge atasafirishwa kutoka nchini India na kufika katika uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Dar es Salaam siku ya kesho Jumapili na baadaye kusafirishwa hadi nyumbani kwao jijini Tanga kwa ajili ya mazishi.
Mwili wa marehemu Mrenge utafika Dar es Salaam Jumapili wiki hii ukitokea India...na baada ya hapo shughuli za kiserikali za kumsafirisha hadi Tanga nyumbani kwao zitafanyika. Mungu alitwaa na Mungu ametoa...Amina, alisema Kandoro akionekana kugubikwa na majonzi.
Awali ilielezwa kwamba Mrenge alipelekwa nchini India akisumbuliwa na ugonjwa wa figo, huku taarifa nyingine zikidai anasumbuliwa na shinikizo la damu.
Mungu ailaze mahala pema roho ya marehemu Serenge Mrenge, Amina.
Kifo cha mkuu huyo wa wilaya ya Ilemela kimetokea juzi nchini India ambapo alikuwa akitibiwa ugonjwa wa tumbo uliokuwa ukimtatiza kwa kipindi kirefu sasa.
Akithibitisha jana kifo hicho, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro, aliiambia Tanzania Daima: DC Mrenge amefariki jana (juzi), nchini India, alikokuwa akipatiwa huduma za kitabibu za ugonjwa wa tumbo uliokuwa ukimsumbua.
RC Kandoro alisema mkuu huyo wa wilaya ya Ilemela alipelekwa nje ya nchi zaidi ya wiki tatu zilizopita, baada ya Hospitali ya Rufaa ya Bugando ya jijini Mwanza, kushindwa kumtibu na kutoa kibali cha kupelekwa nchini India kwa matibabu ya tumbo ambapo mauti yamemkua huko.
Kifo cha mkuu huyo wa wilaya kimekuja miezi michache baada ya mkuu wa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, Creophat Rugarabamu, kufariki nchini India alikopelekwa kwa matibabu ya shinikizo la damu.
Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Mwanza, mwili wa marehemu Mrenge atasafirishwa kutoka nchini India na kufika katika uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Dar es Salaam siku ya kesho Jumapili na baadaye kusafirishwa hadi nyumbani kwao jijini Tanga kwa ajili ya mazishi.
Mwili wa marehemu Mrenge utafika Dar es Salaam Jumapili wiki hii ukitokea India...na baada ya hapo shughuli za kiserikali za kumsafirisha hadi Tanga nyumbani kwao zitafanyika. Mungu alitwaa na Mungu ametoa...Amina, alisema Kandoro akionekana kugubikwa na majonzi.
Awali ilielezwa kwamba Mrenge alipelekwa nchini India akisumbuliwa na ugonjwa wa figo, huku taarifa nyingine zikidai anasumbuliwa na shinikizo la damu.
Mungu ailaze mahala pema roho ya marehemu Serenge Mrenge, Amina.