Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,679
- 70,979
Michezo ya Kimataifa kama Olimpic na mingineyo huwa inabeba Utaifa na ni njia mojawapo ya kulitangaza taifa pia kulijengea heshima. Katika michezo iliyopita ya London, jirani zetu Kenya walifanikiwa kupata medali 11. Dhahabu 2,Fedha 5, na Shaba 4. Na sisi hapa kwetu kama kawaida tuliambulia patupu.
Katika hali isiyo ya Kawaida Rais wa Kenya amecharuka na kuamua kuunda tume ya kuchunguza kwa nini Kenya imepata medali hizo 11 pekee na si zaidi ya hapo? Hii inaonyesha ni jinsi gani Rais Kibaki anavyopenda heshima ya nchi yake iendelee kuwa juu zaidi ya hapo ilipofikia.
Kwetu sisi pamoja na aibu ya kutopata kitu, ni Business as usual. Habari hiyo ndio imetoka wala hakuna hata tamko lolote. Mheshimiwa Rais wetu wewe umeridhika? mbona kama kuna medali hata moja tuu ingepatikana ungeiitisha Ikulu kuipokea kwa mbwembwe? Tafadhali nawe chukua hatua katika hili sio kujisifia kuleta makocha tuu ambao wanaishia kulipwa vizuri na heshima yetu nje inazidi kupotea kwa kutokufanya vizuri.
Mkuu charuka na wewe.
Katika hali isiyo ya Kawaida Rais wa Kenya amecharuka na kuamua kuunda tume ya kuchunguza kwa nini Kenya imepata medali hizo 11 pekee na si zaidi ya hapo? Hii inaonyesha ni jinsi gani Rais Kibaki anavyopenda heshima ya nchi yake iendelee kuwa juu zaidi ya hapo ilipofikia.
Kwetu sisi pamoja na aibu ya kutopata kitu, ni Business as usual. Habari hiyo ndio imetoka wala hakuna hata tamko lolote. Mheshimiwa Rais wetu wewe umeridhika? mbona kama kuna medali hata moja tuu ingepatikana ungeiitisha Ikulu kuipokea kwa mbwembwe? Tafadhali nawe chukua hatua katika hili sio kujisifia kuleta makocha tuu ambao wanaishia kulipwa vizuri na heshima yetu nje inazidi kupotea kwa kutokufanya vizuri.
Mkuu charuka na wewe.