Mkuu kama kwenye avatar yako umependa na umefanikiwa kuweka picha ya mtoto wa mzungu usiyemjua hata unashindwaje kuwapenda watoto wa mpenzi wako?
Anyway, Shukuru hata unapendwa kiasi kwamba mdada kasema ua iwe akakutambulisha wanawe kwani wengi wamefichwa wakajua miaka mitano ama zaidi baada ya ndoa.
Wabichi unaowanadi ni kweli wanapendeza machoni ila kumbuka watakuzalia watoto wa wanaume wengine ndani ya ndoa na utalea mpaka unakufa hujui si wa kwako na hii ndiyo dharau kubwa kuliko zote.
Ushauri wangu ni umepata anayekupenda na unajua hilo hivyo tulia. Najua kuna kasumba ya single mothers Tanzania na Africa kama si dunia nzima ila nina mifano mizuri ambayo ingekupa imani nao.
Wewe angalia, kuwa naye karibu ujue kuwa hana yale zaidi ambayo hayarekebishiki mjadiliane. Ukiamua kumuoa mpende na watoto wake ukiamua la muache kwa heshima na mbaki na siri zenu msianikane atapata wa kumpenda.
Sent using
Jamii Forums mobile app