Khadija Kopa: Najutia sana kitendo cha kufanya abortion

Frumence M Kyauke

JF-Expert Member
Aug 30, 2021
630
1,245
Khadija Omar Abdallah Kopa (amezaliwa Zanzibar, 1963) ni mwimbaji wa muziki wa Taarab na mtunzi wa nyimbo kutoka nchini Tanzania. Mbali ya muziki, Kopa ni mama wa nyumbani, mfanyabiashara na pia mwanaharakati wa kisiasa nchini Tanzania.

Khadija Kopa
Jina la kuzaliwa: Khadija Omar Abdallah Kopa

Amezaliwa:1963
Kazi yake:Mwimbaji, mtunzi wa nyimbo, Mtayarishaji wa rekodi, mwanamuziki

Ala:Sauti
Miaka ya kazi:1990–hadi sasa
Ameshirikiana na Diamond Platnumz, Abdul Misambano, Ali Star, Mzee Yusuph, TOT

Anafahamika zaidi kwa ushirikiano wake mkubwa na bendi ya TOT. Ameanza kuimba Taarab tangu mwaka 1990 na bendi ya kwanza kujiunga nayo ilikuwa Culture Musical Club.

Mtoto wake wa kike Zuhura Othman Soud, afahamikaye kwa jina la kisanii kama Zuchu ni mwimbaji pia. Alijiunga na Wasafi Classics na kutoa nyimbo maarufu kama vile: Nisamehe, Sukari, Yalaa, Cheche, Wana.

Hivi karibuni mwanamuziki huyu amejutia sana kitendo cha kufanya abortion na kutoa kauli kwa lengo la kuwaasa wanawake wenye tabia hiyo, Khadija Kopa anasema

Kutoa mimba ni ujinga sana, maana saizi ningekuwa na watoto wangu kama saba. Najuta kweli kweli, lakini unajua wakati ule ndio jina limesimama kweli kweli, sasa wakati huo nilee mimba wapi na wapi. Ila najuta pengine ukute mwanangu angekuwa Rais sasa. Namuomba Mungu anisamehe, najuta sana na vijana msifanye hilo. Mungu naomba anisamehe sitaki kulisikia tena jambo hilo"- Khadija Kopa

images (6).jpeg
 
Huyu mama pamoja na mambo mengine ni mkweli na anajua maana halisibya Toba tofauti na wengine wanaogugumia maumivu ya dhambi ndani

1. Kitendo alichokifanya kutubu hadharani dhambi kubwa kama hii ya mauaji ndicho hicho wakatoliki wanalalamikiwa na madhehebu na dini nyingine kuungama kwa binaadam mwenzake( Padre)

2. Huwezi kutubu moja kwa moja kwa Mungu usiyemuona ukasema dhambi imetoka. Kutubu lazima usikie aibu ya kile ulichokitenda, umweleze binadamu ambaye Mungu amemuumba kwa mfano wake na ukishatoa mzigo huo kifuani urudi Kwa Mungu na kuomba msamaha wa kutokurudia tena na Mungu atakusamehe

3. Kuna watu wana madhambi Makubwa , wanamfanya Mungu kama mjomba wao, wanamwomba kimawenge chumbani kesho wanarudia tena
 
Kuna watu watajitia Ujaji ili wamuhukumu huyu Mama lakini ukweli ni kuwa wanawake wengi mno waliopo kwenye umri wa kubeba mimba wanafanya abortions.

Wanawake waliopo kwenye ndoa wanaongoza kutoa mimba, mke anachepuka anabeba ujauzito wa mashaka, kwa kuepuka aibu ya kuzaa mtoto asiyefanana na Baba ama watoto wengine anaona bora atoe mimba.

Kuna wengine wanazitoa sababu ya ugumu wa malezi. Unaweza kuishi na mwanamke chumba kimoja miaka nenda rudi lakini usihisi wala kujua mienendo yake. Tumbo la uzazi linaambatana na siri nyingi mno.

Paternity fraud na abortions naviona sawa tu, aliyetoa mimba siyo mdhambi kuliko anayebambikia watoto.
 
Huyu mama pamoja na mambo mengine ni mkweli na anajua maana halisibya Toba tofauti na wengine wanaogugumia maumivu ya dhambi ndani

1. Kitendo alichokifanya kutubu hadharani dhambi kubwa kama hii ya mauaji ndicho hicho wakatoliki wanalalamikiwa na madhehebu na dini nyingine kuungama kwa binaadam mwenzake( Padre)

2. Huwezi kutubu moja kwa moja kwa Mungu usiyemuona ukasema dhambi imetoka. Kutubu lazima usikie aibu ya kile ulichokitenda, umweleze binadamu ambaye Mungu amemuumba kwa mfano wake na ukishatoa mzigo huo kifuani urudi Kwa Mungu na kuomba msamaha wa kutokurudia tena na Mungu atakusamehe

3. Kuna watu wana madhambi Makubwa , wanamfanya Mungu kama mjomba wao, wanamwomba kimawenge chumbani kesho wanarudia tena
Huyo mama kwa mujibu wa imani yake bado hajajua maana ya toba.
Katika uislam mtu muovu mno ni yule anaefanya madhambi gizani(kwa kujificha) halafu akitoka hapo anaenda kuwasimulia watu.
Kwa mujibu wa uislam toba ni baina ya mja na mola wake.
Hii tabia ya kutubu kwa kuutangazia ulimwengu sio katika mila ya uislam.
 
Khadija Omar Abdallah Kopa (amezaliwa Zanzibar, 1963) ni mwimbaji wa muziki wa Taarab na mtunzi wa nyimbo kutoka nchini Tanzania. Mbali ya muziki, Kopa ni mama wa nyumbani, mfanyabiashara na pia mwanaharakati wa kisiasa nchini Tanzania.

Khadija Kopa
Jina la kuzaliwa: Khadija Omar Abdallah Kopa

Amezaliwa:1963
Kazi yake:Mwimbaji, mtunzi wa nyimbo, Mtayarishaji wa rekodi, mwanamuziki

Ala:Sauti
Miaka ya kazi:1990–hadi sasa
Ameshirikiana na Diamond Platnumz, Abdul Misambano, Ali Star, Mzee Yusuph, TOT

Anafahamika zaidi kwa ushirikiano wake mkubwa na bendi ya TOT. Ameanza kuimba Taarab tangu mwaka 1990 na bendi ya kwanza kujiunga nayo ilikuwa Culture Musical Club.

Mtoto wake wa kike Zuhura Othman Soud, afahamikaye kwa jina la kisanii kama Zuchu ni mwimbaji pia. Alijiunga na Wasafi Classics na kutoa nyimbo maarufu kama vile: Nisamehe, Sukari, Yalaa, Cheche, Wana.

Hivi karibuni mwanamuziki huyu amejutia sana kitendo cha kufanya abortion na kutoa kauli kwa lengo la kuwaasa wanawake wenye tabia hiyo, Khadija Kopa anasema

Kutoa mimba ni ujinga sana, maana saizi ningekuwa na watoto wangu kama saba. Najuta kweli kweli, lakini unajua wakati ule ndio jina limesimama kweli kweli, sasa wakati huo nilee mimba wapi na wapi. Ila najuta pengine ukute mwanangu angekuwa Rais sasa. Namuomba Mungu anisamehe, najuta sana na vijana msifanye hilo. Mungu naomba anisamehe sitaki kulisikia tena jambo hilo"- Khadija Kopa

View attachment 2065729
Hongera kwa hatua hii ambayo pia inakusaidia kuponya majuto ya nafsi yako. Hii inaweza kuwa tiba pia kwa matatizo ya urahibu niliona katika movie moja ya rubani cha pombe.
 
Huyu mama pamoja na mambo mengine ni mkweli na anajua maana halisibya Toba tofauti na wengine wanaogugumia maumivu ya dhambi ndani

1. Kitendo alichokifanya kutubu hadharani dhambi kubwa kama hii ya mauaji ndicho hicho wakatoliki wanalalamikiwa na madhehebu na dini nyingine kuungama kwa binaadam mwenzake( Padre)

2. Huwezi kutubu moja kwa moja kwa Mungu usiyemuona ukasema dhambi imetoka. Kutubu lazima usikie aibu ya kile ulichokitenda, umweleze binadamu ambaye Mungu amemuumba kwa mfano wake na ukishatoa mzigo huo kifuani urudi Kwa Mungu na kuomba msamaha wa kutokurudia tena na Mungu atakusamehe

3. Kuna watu wana madhambi Makubwa , wanamfanya Mungu kama mjomba wao, wanamwomba kimawenge chumbani kesho wanarudia tena

Kutubu Ni kujuta, kughairi Na kugeuka; haya yakikamilika moyoni mwako Toba imekamilika.
 
Kutubu Ni kujuta, kughairi Na kugeuka; haya yakikamilika moyoni mwako Toba imekamilika.
Ni rahisi kusema, kama hautoweka ushahidi kwa binadamu anayekuona , ukasema moyoni kwamba umekiri kwa Mungu , bado ni rahisi kurudia, kumbuka Yesu alivyowaponya ukoma ambao kwa wakati huo ulikuwa unasadikika ni matokeo ya kufanya dhambi kubwa sana , aliwaambia " NENDENI MKAJIONYESHE KWA MAKUHANI"
 
Ni rahisi kusema, kama hautoweka ushahidi kwa binadamu anayekuona , ukasema moyoni kwamba umekiri kwa Mungu , bado ni rahisi kurudia, kumbuka Yesu alivyowaponya ukoma ambao kwa wakati huo ulikuwa unasadikika ni matokeo ya kufanya dhambi kubwa sana , aliwaambia " NENDENI MKAJIONYESHE KWA MAKUHANI"

Padre mwenyewe anayetubisha katia mimba sister, Toba Ni moyo! Hali ya moyo; wewe mwenyewe umetubu Mara ngapi Na unarudia; ukijua utatubu tena!

Ila ukiwa Na sababu mwenyewe Za kutubu Na kuacha inakuwa Na nguvu zaidi!
 
Padre mwenyewe anayetubisha katia mimba sister, Toba Ni moyo! Hali ya moyo; wewe mwenyewe umetubu Mara ngapi Na unarudia; ukijua utatubu tena!

Ila ukiwa Na sababu mwenyewe Za kutubu Na kuacha inakuwa Na nguvu zaidi!
Sista yupi ? Hiyo ndiyo ilim mnayofundishwa kwa viboko madrasa ya kashfa na matusi? Huwezi kujibu hoja bila kashfa na maneno yadiyofaa?
 
Mimi Mkristo Kaka! Pope na ushoga kakubali almost, uchafu wa ki Catholic nimeuona Rome in 2013 wakati nasoma! Hujui mambo mengi Sana!
Kuna siku utaupata huo ukristu, endelea kuutamani kwa kufanya matendo ya huruma kwa maskini, heshimu kila binaadamu aliyeumbwa na Mungu epuka kinywa chako kutamka au mkono wako kuandika mambo machafu na mabaya dhidi ya mwenzako, hakika utamwona Yesu na utakuwa na nafasi yako mbinguni. Lakini mdomo wako ukitumika kuwasengenya wenzako na kuongea maneno mabaya hakika Mungu atakugeuzia kama sii wewe kizazi chako
 
Kuna siku utaupata huo ukristu, endelea kuutamani kwa kufanya matendo ya huruma kwa maskini, heshimu kila binaadamu aliyeumbwa na Mungu epuka kinywa chako kutamka au mkono wako kuandika mambo machafu na mabaya dhidi ya mwenzako, hakika utamwona Yesu na utakuwa na nafasi yako mbinguni. Lakini mdomo wako ukitumika kuwasengenya wenzako na kuongea maneno mabaya hakika Mungu atakugeuzia kama sii wewe kizazi chako

Nafuata neno la Mungu sio kingine! Na neno linataka badiliko la moyo sio kuungama Kwa wadhambi wenzangu!
 
Back
Top Bottom