Kha..! Nyie BAKWATA kulikoni..?

Status
Not open for further replies.
Dini gani mnategemea mwandamo wa mwezi.....mwezi usipoandama mtaendelea kufunga?...........allah!
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Ulivyoanza maelezo yako nilifaham mwisho lazima ujichanganye!<br />
Mwezi una hisabu zake nawe wafunga kwa kufuata hizo siku. Sio lazima wakiswali makkah au indonesia watu wote waswali idi.<br />
Hapo ndipo hujua uelewa wa wachangiaji unapoanzia...<br />
Tazama katika uislam ibada muhim na ngumu kuliko zote ni swalat lakin ibada hii inaswaliwa kutokana na masaa ya eneo husika mbona hamjasema kuna swalat ngapi????<br />
Umuhim ni hizo siku ulivyoanza kufunga na utavyomaliza kufungua.<br />
Wala halina maelezo na hujja nyingi kama wengi wanavyohiaji kulizungumzia. Hapo hakuna utata...ndio maana wasomi wakubwa hawawezi jadili hilo...linabaki kwenu wachache wa ilm hiyo!<br />
Ndio muingie madrasani mjifunze vizuri.<br />
Tena kwenye majamvi ndio penyewe!
<br />
<br />
kumbe hii kitu ni RAMLI
 
Walikuwa wanapata maamuzi kutoka Serikalini wakati wa Nyerere, kwa sasa wanapata kutoka kanisani!

Kama Siku Hizi Msikiti na Waislam mnatii Maagizo ya Kanisa ina Maana Ufalme wa Allah Umefitinika na sasa Hauwezi kusimama kamwe
 
Hapo ndio utajuwa kwanini Waislaam tunataka kadhi na mahakama ya kadhi virudishwe, vilikuwepo vikaondolewa na nyerere kwa udini wake.

Kinachokataliwa sio mahakama ya kadhi na kadhi mwenyewe. Kinachokataliwa ni mfumo unaotaka kutumika. Kuitaka serikali uhusike as if mahakama ya kadhi ni chombo cha serikali! Mnaweza kuanzisha kama Katoliki walivyo na mahakama yao. Hawakuhitaji serikali kurekebisha katiba ili waanzishe mahakama yao. Lakini lazima kiwe ni nje ya mfumo wa serikali. Kwamba atayetaka kufuata utaratibu wa dini ya kiislamu ataufuata huko ambaye hataki atatumia mahakama zetu za kawaida. Lakini pili kwanini uanzishe kitu ambacho kinamfanya hata yule asiye amini katika hilo abebe mzigo wa kukiendesha maana kitatakiwa kihudumiwe na pesa ya walipa kodi ambao ni mjumuiko wa wale wanao amini na wale wasio amini. Kwanini msianzishe nje ya mfumo wa serikali na kikaendeshwa na kuhudumiwa na pesa ya waamini tu, kama wanavyofanya Roman wala hawakuhitaji serikali kutengeneza vifungu vya kuwalinda na wala hawahitaji kuwa sponsored na serikali. Tukitaka serikali isiyona dini ijingize kwenye kuendesha shughuli za dini tena kwa katiba hatutafika mbali! Itakuwaje kila makundi ya dini mbali mbali yakitaka serikali itambue mambo yao na kuyaweka kwenye katiba lakini pia yahudumiwe kwa pesa inayopatikana toka kwa makundi yote? Maana mnataka kadhi mkuu alipwe na serikali kama wanavyolipwa na mahakimu wa mahakama zetu. Vinginevyo tuendelee kutumia mahakama zetu zinazoendeshwa na serikali maana haziegamii upande wowote.
Ni suala la kujipanga mkaja na mkakati wa kuanzisha kadhi na mahakama ya kadhi pasipo kuitaka serikali iikubali katika katiba ili iweze kuihudumia. Kama vile katiba ambavyo mekaa kimya katika makundi mengine, lakini huku ikijua kuwa yapo yanafanya kazi na mtu ambaye anahisi hajatendewa haki anarudi kwenye mahakama za kawaida na mambo yanasuluhishwa.
 
Mods huu mchanganyika mara nyingine haufai wengi wano changia humu wanafata mtiririko wa yale waliyo kuwa wakiyazungumza..
Ni ubora ile thread yangu mngeipeleka kwenye jukwaa la dini ii iwe msaada kwa waisilamu wengine walio kwenye mkanganyiko.
kwani hapa ni wachache tu watapata nafasi ya kusoma ile makala.

nawakilisha tafadhali
 
Ndio maana wanafanya njama kuhakikisha waislam wanfarakana katika kila jambo hata katika ibada zao.<br /> Zote ni athari za mfumo kristo ila mwisho wake unakuja karibuni.
<br /> <br / ukristo unaingiaje hapa wkat rais muislam makamu wk muislam bakwata waislam vipi uuingize ukristo
 
Mods huu mchanganyika mara nyingine haufai wengi wano changia humu wanafata mtiririko wa yale waliyo kuwa wakiyazungumza..
Ni ubora ile thread yangu mngeipeleka kwenye jukwaa la dini ii iwe msaada kwa waisilamu wengine walio kwenye mkanganyiko.
kwani hapa ni wachache tu watapata nafasi ya kusoma ile makala.

nawakilisha tafadhali
Na wewe ni wa wapi? yaani zile copy & paste kutoka kwenye internet wewe unaita makala? makala andika kwa kutumia mawazo yako na sio kucopy na kuja kupaste hapa.
 
Hapo nimekubali hujja yako japo si muislam.
Tatizo wanatumia chuki iliopo Bakwata kuwatusi wengine si sahihi...bakwata hawaongozi ibada...kama taasisi imeamua kutangaza na wengine wanasema wanafuata au wanaungana na waislam wengine ulimwenguni ni sawa kwao. Maana hakuna tatizo maana siku za mwezi hazizidi 31 na leo ni 30 tatizo lipo wapi?
Kwa madai yao wanasema idi zipo ngapi hawa nawaona hata ilm ya dini na mas'ala mazito kama haya hawafaham 100%.
Ibada kubwa na ngumu ni swala mbona tunaswali tafauti kila siku ...hilo nalo mbona hawasemi swalat ziko ngapi duniani? Umuhim ni kusubir muda .
Wasiwababaishe watu wengine!
Ilm za dini ni kujenga hujja kiilm...hakuna vya technology...ndio iwe lazima kufuatwa...kua itatoa mizozo ...si kweli.
Inshaallah idi kesho j5!

mmhh....shekhe usilete maswala ya zamani wakati tupo advanced bana.....zamani hakukuwa na mawasilianao na ndo maana ilikua tabu kupata taarifa za miandamo ya miezi lakini sio sasa......hebu niambie kiukweli kabisa mfano afrika kusini wakiona mwezi wewe hutakula idd? na kwa nini? kuna mtu hapo juu aliuliza swali na mimi narudia kuuliza ...(mwenye enzi mungu atusamehe kwa hili..) kama mtume (s.a.w) angekuwepo na kwa kuwa yeye yupo makka na yeye angetangaza kuonekana kwa mwezi huko makka je ungekula iddi?? mana ndo ingekuwa imetangazwa na kiongozi wa waislam ambaye ndo tunafuata sunna na mafundisho yake hadi leo.......ungesubiri BAKWATA wakuambie ule idd wakati kiongozi wa umma amekwishasema??.......swali la mfano kwako...
 
mmhh....shekhe usilete maswala ya zamani wakati tupo advanced bana.....zamani hakukuwa na mawasilianao na ndo maana ilikua tabu kupata taarifa za miandamo ya miezi lakini sio sasa......hebu niambie kiukweli kabisa mfano afrika kusini wakiona mwezi wewe hutakula idd? na kwa nini? kuna mtu hapo juu aliuliza swali na mimi narudia kuuliza ...(mwenye enzi mungu atusamehe kwa hili..) kama mtume (s.a.w) angekuwepo na kwa kuwa yeye yupo makka na yeye angetangaza kuonekana kwa mwezi huko makka je ungekula iddi?? mana ndo ingekuwa imetangazwa na kiongozi wa waislam ambaye ndo tunafuata sunna na mafundisho yake hadi leo.......ungesubiri BAKWATA wakuambie ule idd wakati kiongozi wa umma amekwishasema??.......swali la mfano kwako...

nakushauri na wewe mkuu usome ile post "makala" ya jamaa "Iliyo wekwa "hapo nyuma utaelewa hili swala kwa undani zaidi
 
Ndio maana wanafanya njama kuhakikisha waislam wanfarakana katika kila jambo hata katika ibada zao.<br />
Zote ni athari za mfumo kristo ila mwisho wake unakuja karibuni.
<br />
<br />
wewe ni muislamu au Kaafir? kwani allah si amesema! angetaka mngekuwa kundi moja lakini hitlafu miongoni mwenu ni lazima ziwepo. Umebakia kidole juu kapua umebana mfumo kristo mfumo kristo! na kijuba, makwabazi, ndevu kama beberu, kanzu viraka tupu, unachonga mtaani mfumo kristo huku unabip, daah! hivi allah hana uwezo au yuko likizo mpaka mfumo kristo uingie kwenu? wee chonga tu, kesho wajanja wakukamue ngama!
 
wewe ff si muumini ni kaafir fulani tu! Hivi ni kweli wewe kama muumini umuombe kaafir (serkali) kuwapangia mfumo wa ibada zenu(mahakama ya qadi) halafu qadi alipwe na kodi ya wauza nguruwe? hee! kweli uislamu uishie. imebakia kung'oa nyota na mwezi miskitini na kuweka misalaba. au! manake mmeshindwa kujiongoza! mtaomba tena serkali ndio itangaze muandamo wa mwezi mfunge kisha mwandamo tena mfungulie! mnauza uislamu tena kwa risiti.
 
Kila taasisi ina taratibu zake. kabla ya kulaumu ni lazima ujue taratibu za kila taasisi. Kwa Tanzania Bara Shekh wa mkoa wa DSM na anamamblaka ya kutangaza mwezi na Shekh Suranga wa Tanzania visiwani anamamlaka yakutangaza mwezi kwa visiwani.

Quran inasema fungeni kwa kuuona mwezi na fungueni kwa kuuona mwezi. sasa mwezi kwa nchi ambazo majira/muda hatuendani ndpo umetoka lakini kwetu haujatoka. Kwamfano, huku kwetu ikiwa saa 12 jioni china ni saa 6 usiku yaani siku nyingine. Maleysia na Australia ndo balaa kabisa. leo kwetu ni tarehe 30 kwa wenzetu mwezi uliko toka ni tarehe 31, sasa itakuaje wewe ule Idd wakati muda hauendani?

hebu jiulize, leo ukiwa Dar unafuturu wenzetu wa Mwanza bado wamefunga mpaka saa moja kasoro usiku, hali kadhalika kwa Kigoma. Nikikuambia kua kuna nchi sasa hivi wameshindwa kufunga Ramadhani kwasababu mchana ni masaa 14 utakubali? hivyo, kula IDd leo kwasisisi sio sahihi through dini ni imani na imani yako nimuhimu kwa Allah
 
hv ndo mnajiita great thinkers? Nimepitia post nyingi sana... Nlicho kiona ni kwamba wengi wenu huwa mnapenda sana kuongea kwa hisia...yaani mnaendeshwa kwa hisia..matokeo ni kwamba mtu hachangii fact rather anachangia vile ambavyo yeye angependa iwe....great thinking need kudadavua mada jamani....acheni upupu.
 
Hata wenye akili <b>kali </b>si ndo wanaofaulu madaraja ya juu! Magamba tu kampeni yao ya kufarakanisha watu.<br />
Mwenyezi Mungu katika surat Yunus aya ya 5 anabainisha kuwa mwezi hupita katika vituo vyake ili kutokana na hilo watu wajue hisabu za nyakati( idadi ya siku na miezi na miaka). then ifahamike kuwa idadi ya vituo hivyo ni 28, yaani 14 kila upande hivyo baada ya siku ya 29 ni siku ambayo mwezi utakuwa less visible na siku inayofuata utaanza kituo chake kipya. Ndipo mtume akasema funga ni siku 29, la kama hamkuuona (kutokana na sababu mbalimbali, na ukumbuke katika kipindi hicho kupata habari ni suala la barua inayopelekwa kwa masiku kadhaa) tofauti na siku hizi. Pia ifahamike kuwa kuuona (shahida)kulikokusudiwa hapa ni kushuhudia/shahidi bimaana ikiwa tu baadhi ndio waliouona na wameshuhudia hata wale ambao hawakuuona wanalazimika kufuata mwandamo huu. La ikiwa kuuona huku si kwa kushuhudia vipi ya wale ambao wana ulemavu wa macho. Kumbuka kwamba hii hesabu ya kukamilisha 30 inategemea na environment/geographical features and weather conditions. Kwani ni possible kutokana na mazingira ya kijiografia na hali ya hewa inawezekana eneo fulani wanaweza kuuona mwezi na jingine wasiweze kuuona, hivyo ni wajibu kwa waliouuona wawambie wale wasiouona ili nao wafuate. Sasa hili kama nilivyosema mwanzo, kwa miaka ya nyuma ilikuwa ni vigumu kupashana habari ndani ya saa 24 lakini kwa sasa ni suala la seconds. So why Bakwata mnataka kuipotosha dini hii na kuyumbisha watu. Mwisho Kifo cha Bakwata kitakuwa kama kifo cha ccm, watu hawatakubali kila siku kuwayumbisha.
<br />
<br />
Hapo umenipa mashala na maelezo yako. Wapi ndani ya quran imeeleza kua mwezi unazunguuka masiku 28?
Nina ufaham na hayo mambo ya mwezi lakin kwenye dini ya islam hayo hakuna. Unataka kutuelimisha GMT nayo imeanzia wapi?
Maswala haya hakuna haja ya kuwalalamikia Bakwata. Bakwata wanayo matatizo yao basi isiwe kila kiti ni bakwata. Kwanza tuelimishane wenyewe mambo yetu ya dini. Kitendo cha kutaja ubaya wa mwenzio kabla hujataja ubaya wako si kizuri. Pale bakwata wapo masahykh wazuri hawawezi? Kwani makkah inatawaliwa na ukoo wa aali sood nayo ndivyo mtume alifundisha?
Marhum mufti ibn baaz na mamabo makubwa alioyafanya hakua wakimjali kama sherehe zao za serikali ilhali ni mji mtukufu.
Acheni ushabiki kwanza!
 
jamani mwezi ulionekana wapi?? msipende kuwalaumu bakwata bakwata,waislamu tumeamrishwa funga kwa kuona mwezi na fungua kwa kuona mwezi msifate mkumbo kwenye mambo ya kiimani kabisa EID ni kesho na ninawatakia wote EID MUBARAAK.
 
Dini ni imani na kila mtu anaimani yake. Hebu kila mtu afate imani yake na tusikwaruzane kwaajili ya imani ya mtu na wala si vizuri kuitana makafiri. Kumbukeni hadithi ya Mtume Mohamed (s.a.w) pale aliposema jirani yako ndo ndugu yake, hapa mtume hakutaja dini.

kwenye nukuu yangu ya mwanza nimesema, Mwezi ukiandama sehemu ambayo majira ni sawa basi ni halali kula Idd kama ilivyo andikwa kwenye Quran na si vinginevyo. kwa yule aliyetoa mfano wa southafrica, hatujaachana sana kimajira ya muda kwani tumepishana masaa mawili tu.
 
mmhh....shekhe usilete maswala ya zamani wakati tupo advanced bana.....zamani hakukuwa na mawasilianao na ndo maana ilikua tabu kupata taarifa za miandamo ya miezi lakini sio sasa......hebu niambie kiukweli kabisa mfano afrika kusini wakiona mwezi wewe hutakula idd? na kwa nini? kuna mtu hapo juu aliuliza swali na mimi narudia kuuliza ...(mwenye enzi mungu atusamehe kwa hili..) kama mtume (s.a.w) angekuwepo na kwa kuwa yeye yupo makka na yeye angetangaza kuonekana kwa mwezi huko makka je ungekula iddi?? mana ndo ingekuwa imetangazwa na kiongozi wa waislam ambaye ndo tunafuata sunna na mafundisho yake hadi leo.......ungesubiri BAKWATA wakuambie ule idd wakati kiongozi wa umma amekwishasema??.......swali la mfano kwako...
<br />
<br />
Huu mfano wako ni dhaifu sana katika uislam. Mtume alishaambiwa dini imekamilika. Ukisema angekua mtume yupo hai unamaanisha dini bado ina mapungufu!
Ukumbuke katika uislam ibada iliyokua nzito na ngumu ni swalat...je unajua duniani tunaswali tafauti tafauti kila siku? Achilia hii ya kufunga na kufungua na ile ya arafat kule kwa mahujaji.
Haya mambo yanaenda kiilm zaidi na si vile mtu anavyofikiria mwenyewe.
Kama nawe umekula leo haya mungu akuongoze uujue usawa ukiwa hapo ulipo ufuate vipi ibada zako.
 
Wakuu officialy according to BAKWATA kesho Waislamu nchini wanakamilisha siku 30 za mwezi mtukufu na eid itakuwa jtano. Hekima ya mwezi mtukufu ni kuwa watu wafunge kwa pamoja na wafungue pamoja katika eneo husika na kuna chombo maalum cha kutangaza mwezi sio kila mtu tu wengine waweza danganya watu ili wafuate matakwa yao.
KWA WAISLAMU:ni muhimu kuheshimu mamlaka inayowaongoza ukizingatia wengi wao hawana ufahamu mkubwa kuhusu masuala ya dini hiyo.
ukifuatilia wengi wanaolalamika si wala waislamu. Na kama waisilamu hawakuwa wala katika mfungo. Tuheshimu mamlaka zilizo madarakani. Sheikh Mkuu asije akatangaza mwezi kwa staili ya report ya DJ mara kasimamishwa mara karudi mara kasimamishwa tena.
 
kwanza hiyo nguzo ya funga imeshajifia yenyewe! sasa ukiwa mwezini unalima utaangalia mwezi gani? kama ni nguzo jengo lishaanza kubomoka. poleni!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom