kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,301
- 12,600
Sisi wanachama wa CHADEMA tunataka kuona, kusikia na kufanya mambo yanayosaidia kujenga, kukuza na hatimaye CHADEMA kuingia ikulu.
Kwa mara nyingine CHADEMA imenasa kwenye mtego wa ulimbo wa CCM. CHADEMA Inahangaika na kuwaondoa wanawake wao bungeni kwenye uchaguzi ambao cHADEMA walikataa kuutambua matokeo yake mpaka Leo.
Kesi hii ya kutaka akina Mdee watoke bungeni ilipaswa kutanguliwa na CHADEMA kuyatambua matokeo ya uchaguzi wa 2020 kwanza. CHADEMA walipaswa kuishia kwenye kuwafukuza uanachama akina Mdee TU basi na sio kukaza shingo lazima watoke kwenye bunge ambalo wao hawalikubali.
Kesi Yao ingekuwa na mashiko kama chadema wangepinga wabunge wote wa bunge kuweko bungeni maana hawakuchaguliwa kihalali kwa kutumia tume wasioikubali kuwa sio huru.
Maadam hawakuyatambua matokeo ya uchaguzi basi bunge pia sio halali kwao. Kumlazimisha Mdee TU kuwa ndiye wakutoka bungeni badala ya bunge zima ni kukosa dira na mwelekeo.
Kwangu Mimi akina Mdee hawapaswi kuwa bungeni sawa na wabunge wengine wote kutokana na namna uchaguzi mzima ulivyoendeshwa. Njaa Kali, undugu na ukabila ndiyo sababu ya kuwashupalia akina Mdee.
Kwa mara nyingine CHADEMA imenasa kwenye mtego wa ulimbo wa CCM. CHADEMA Inahangaika na kuwaondoa wanawake wao bungeni kwenye uchaguzi ambao cHADEMA walikataa kuutambua matokeo yake mpaka Leo.
Kesi hii ya kutaka akina Mdee watoke bungeni ilipaswa kutanguliwa na CHADEMA kuyatambua matokeo ya uchaguzi wa 2020 kwanza. CHADEMA walipaswa kuishia kwenye kuwafukuza uanachama akina Mdee TU basi na sio kukaza shingo lazima watoke kwenye bunge ambalo wao hawalikubali.
Kesi Yao ingekuwa na mashiko kama chadema wangepinga wabunge wote wa bunge kuweko bungeni maana hawakuchaguliwa kihalali kwa kutumia tume wasioikubali kuwa sio huru.
Maadam hawakuyatambua matokeo ya uchaguzi basi bunge pia sio halali kwao. Kumlazimisha Mdee TU kuwa ndiye wakutoka bungeni badala ya bunge zima ni kukosa dira na mwelekeo.
Kwangu Mimi akina Mdee hawapaswi kuwa bungeni sawa na wabunge wengine wote kutokana na namna uchaguzi mzima ulivyoendeshwa. Njaa Kali, undugu na ukabila ndiyo sababu ya kuwashupalia akina Mdee.