Lubebenamawe
JF-Expert Member
- Oct 27, 2014
- 1,952
- 2,194
Yaani wakimpata mtu dhaifu na loyal kwao kama Fred wa Tigo wanajipatia taarifa za siri za mteja kwa urahisi sana!Hii sheria ina udhaifu mkubwa sana, haipaswi kuwa ni police officer au law enforcement officer bali inapaswa kuwa ni mahakama.
Hivi hakuna watendaji wa hivyo vyombo ulivyotaja wanaotumia vibaya madaraka yao?Samahani mkuu niulize.
Hivi vyombo vya usalama vya nchi, TRA na Taasisi zingine kutaka kujua kuwa kuna uwezekano wa hujuma kuwepo na kutaka taarifa kwa ajili uchunguzi ni MATUMIZI MABAYA? Au kukosa weledi wa watendaji wa Taasisi ndio VIBAYA?
Pia maoni yangu tunahamisha goli, sasa tunajadili privacy ya Mbowe jambo ambalo ni Sawa lkn tunaacha kuziba kuwa kufanya miamala sio Kosa ana Haki ya kumtumia au kupokea pesa halali.
As if tuna cover kuwa kuna uhalifu kwa kutumia miamala.
Sir,Hii ni wakeup call, kuwa usitumie mitandao ya simu kama siyo lazima sana. Labda utumie zaidi data ili mawasiliano yawe kwa whatsap, skype au telegram, huduma ambazo savers hazipo nchini, lakini siyo sms wala calls, au kutuma hela
Sir,
Even these are susceptible to hacking !
Server kuwa mbali hakuzuii wadukuzi kufuatilia kila kitu
Hivi hakuna watendaji wa hivyo vyombo ulivyotaja wanaotumia vibaya madaraka yao?
Utawatambua kwa kuwaona??
Kama wapo au hawapo ni nani atasimama katikati kama refa kulinda maslahi na haki za kila upande??
Je, ni nani atafanya maamuzi kuwa muamala fulani ni batili mwingine ni halali??
Trust no one!
Kwa hiyo polisi waombe idhini kwa mhalifu ili wamchunguze?Kama mteja mwenye namba ya kampuni husika anafanya vitendo vya uharifu na Polisi wakagundua, Taratibu ziko wazi kabisa mkuu kwa mujibu wa sheria,
1) mteja imempasa afahamishwe
2)akikataa , kampuni husika wanatakiwa wapeleke maombi Mahakamani
Huyu jamaa kakataa kabisa kuwa wao sio kazi yao kuwalinda wateja kuhusiana na usili wao, na kwamba Polisi wakitaka details za wateja wao iwe kwa uchnguzi wa jinai au Laah wao wanatoa TU, kinyume na sheria 34
Polisi hata kukukamata inatakiwa kufuata utaratibu. Shida huku tunaishi porini.Kwa hiyo polisi waombe idhini kwa mhalifu ili wamchunguze?
Naendelea kuwashangaa usioona udhaifu wa maelezo ya Wakili wa Tigo Alfred Kapala. Tatizo si kutoa taarifa Polisi, tatizo kubwa ni maelezo yake kuwa;Naona kila mtu anazungumzia usiri kuhusu kutoa taarifa za wateja. Hili jambo sijaelewa, mfano ikitokea kuna jambo lolote baya linafanywa na mteja, kisheria imekaaje? Tigo inapaswa kumlinda mteja mmoja hata kama jambo lolote hatarishi linalenga wateja wengi?...
Mmmh
Hii ishu kama nilisikia kipindi, nadhani ilikuwa Americakuna ishu moja ili trend sana dunian hapo kati ya kigaidi, kuna gaidi mmoja wa mashariki ya kati huko alikamatwa na jeshi la marekani asa ushahidi ulikuwa kwenye iphone so ilibid iphone ifunguliwe ili ushaidi uonekane,. asa gaidi mwenyewe aligoma kufungua sim yake kwaiy jeshi la marekani liliomba kampuni ya apple wafungue passcode lkn mpka mwish apple waligoma kufungua kwa kuwa wenyewe wanatunza siri za wateja.. nafikir hapo utakuwa umelewa
Mfano wako mbona ni tofauti... Umeongezea facts mpya...!Mfano Kuna watu wanaka kukuua mleta mada wanawasiliana na simu kupanga wakuulie wapi unataka kampuni ya simu wasiripoti polisi kuhusu Hilo ili kunusuru maisha yako? Na wahusika wadakwe?
Ulinzi na Usalama wa watumiaji wa simu na wananchi ni wa kila mtu zikiwemo kampuni za simu
Jirani yako ukiona majambazi yamemvamia huhitaji kibali chake kuripoti polisi
Hapana sio sahihu hata kidogoNaendelea kuwashangaa usioona udhaifu wa maelezo ya Wakili wa Tigo Alfred Kapala. Tatizo si kutoa taarifa Polisi, tatizo kubwa ni maelezo yake kuwa;
1.Siri za wateja wao si kipaumbele chao.
2.Taarifa inaweza kutolewa kwa yeyote akitaka hata mtu binafsi isipokuwa kama anahtaji taarifa ya mtu mwingine. Yaani Leo wewe ukijifanya ni Mimi na ukawa na vielelezo ni Mimi unapata taarifa zangu. Hili ni kweli kabisa wala hajadanganya. Ndo maana Tigo na Voda zimetumiwa sana na wezi (Ile hela tuma kwenye Namba hii) kuibia wateja. Mtu anapiga simu huduma kwa wateja Tigo kwa Namba nyingine anaomba Namba yake nyingine (ya mtu mwingine) isitishwe kwa muda simu ina tatizo na wao bila kujiridhisha wanaistisha na wezi wanatumia muda huo kuihamisha kwenda line nyingine na kuitumia kuibia marafiki na ndugu wa mteja wa awali. Huyu MWIZI anajifanya ni wewe una shida ya laki 5 umekamatwa au unaumwa kumbe Tigo wamemsaidia MWIZI kusajili line ya ndugu yako.
3.Kwa maelezo yake hata Polisi wasipofuata matakwa ya sheria kuomba taarifa za wateja, Tigo itawapa tu. Ndo maana kipindi Fulani kiongozi mmoja akamwambia Mkuu wa wilaya wa kike Nina taarifa zako zote maana mawasiliano yako hata ya usiku wa manane ninayo.
NB; Bado unaona wako sahihi?
Huu upumbavu wako ulirithi au umeutafuta mwenyewe?Police ni chambo cha usalama na kudai taarifa za mtuhumiwa yeyote au mtu anayepelelezwa ni sawa kabisa ...achani ushabiki wa kisiasa..maana ya usalama nini sasa..kwa hiyo wasipewe huo uwezo ili nchi itekwe mara moja..achani ushabiki na ujinga..kwa hiyo police wakatufute order mahakani ili process ya kubaini wahalifu mara moja liwe complicated..acheni ushabiki
imenishangaza sana hiyo ,kwamba ofisa wa polisi anaweza tu kuamua kuomba taarifa zako tigo na akazipata kirahisi tu!!!! looh!!!Shaidi ambaye ni wakili katika kesi ya Mbowe kwa jina la Frank Kapara ameeleza kwa mlolongo mrefu uzoefu na utendaji wa kazi yake katika kampuni ya Tigo. Pia ameeleza jinsi gani anavyotoa taarifa za wateja kwa vyombo vingine pale anapohitajika kufanya hivyo. Maelezo yake anaonyesha ni rahisi sana kwa taarifa za wateja kutoka kampuni za simh kutolewa kwa vyombo kama polisi zinapotakiwa jambo ambalo si afya ksa faragha ya mawasiliano kwa wateja. Hali hiyo inaweza kuwa hivyo pia kwa mabenki.
Tatizo la upatikanaji kwa urahisi taarifa za wateja iwe kwenye mawasiliano, benki, hospitali au sehemu nyingine ni taarifa hizo kuweza kutumiwa vibaya na watu wenye nia ovu. Lakini pia kila binadamu anapenda na kuhusudu faragha. Hii ndio sababu imezifanya nchi nyingi zilizoendelea na kustaarabika kuweka sheria kali za kulinda siri za wateja hata za kawaida tu.
Pia duniani kuna ncho zinazotambulia kama nchi nzuri zaidi za watu kuhifadhi fedha zao na zimevutia watu wengi kutoka kila kona ya dunia kuhifadhi fedha zao. Nchi hizo ni pamoja na Panama, Cayman, Switzerland, Luxembourg, Seychelles,Singapore, Belize Ujerumani n.k. Sifa kuu katika nchi hizi ni utunzaji wa siri za wateja wao. Sifa hii imefanya nchi hizi kuwa na ukwasi mkubwa wa kifedha kwa njia ya mitaji inayotumika kuziendeleza. Ili upate taarifa za mteja katika nchi hizi ni lazima usote sana mahakamani na majaji wajiridhishe kwamba kweli kuna ulazima huo jambo ambalo huwa nadra sana majaji kukubali.
Kesi ya Mbowe inayoendelea iliamshe bunge kama mhimili na chombo cha kutunga sheria, kuweka sheria madhubuti za upatikanji taarifa za wateja katika simu, mabenki, hospitali na huduma nyingine. Hii itasaidia sana pia kuvutuia uwekezaji kutoka nje.
TRA wanajikwapulia tu fedha kiulaini...Hadi benki hakuna mtu wa katikati kama refa ambayo inapaswa kuwa mahakama kulinda haki za wateja! Tumechelewa sana.
Hilo liko wazi sasa na ndo maana Kibatala akatoa mfano wa kesi ya hela alizoibiwa mteja na wao Tigo wameshitakiwa japokuwa Wakili Msomi fake wa Tigo anajifanya hajui kitu.Kwa haya yanayozungumzwa na Wakili msomi wa TIGO ni dhahiri kabisa hawa ndio wanavujisha siri ya pesa zilizopo kwenye akaunti za watu kwa matapeli na wezi wa mtandaoni.